Wadudu watoboao meno

Wadudu watoboao meno

kiye

Senior Member
Joined
Apr 28, 2012
Posts
117
Reaction score
25
Habari wana JF.
Ni matumaini weng wetu ni wazima ila mimi hali si nzur sana.
Ndugu wana JF, naomba maelezo kwa wataalamu wa meno na kinywa. Kwa muda mrefu nilikua naumwa jino hatimaye leo nikaenda Clinic ya meno kwa lengo la kungo'a, katika uchunguzi daktari kaniambia zaidi ya meno 5 yametoboka na yanahitaji kuzibwa matundu. Baada ya kumuuliza huyu mdudu anyetoboa meno nawezaje kumuondoa? Amenijibu meno hayatobolewi na mdudu hata siku moja bali ni chakula chenye sukari ama kitamu.
Swali je meno hutobolewa na wadudu ama vyakula kama daktari alivosema?
 
Naona wataalam wako mbali
 
sasa majibu ya clinic hujaamini au unataka kupima uwezo wa madaktari humu ndani ?
 
Yeah inanifanya nisiamin kwan kuna dawa zipo pharmacy za maji na tube za kusukutulia ukizisoma zinaeleza zinaondoa wadudu wanaotoboa meno, so inachanganya hapo mkuu au we unaona inakaaje hapo.
 
Yeah inanifanya nisiamin kwan kuna dawa zipo pharmacy za maji na tube za kusukutulia ukizisoma zinaeleza zinaondoa wadudu wanaotoboa meno, so inachanganya hapo mkuu au we unaona inakaaje hapo.

Hukuelewana na dentist.
Kuna dhana kwamba kuna mdudu anayetoboa meno....kwa maana kula au kupekecha meno....ambayo sio kweli.

Kuna vijidudu vinatumia sukari na vinapatikana kinywani. Sasa hivi vijidudu vinatumia sukari ila vinatoa acid inayoozosha meno.....
Kwa hiyo kimsingi bacteria hawatoboi meno....ila wanafanya fermentation ya sukari na kupata acid inayoharibu meno.
 
Hukuelewana na dentist.
Kuna dhana kwamba kuna mdudu anayetoboa meno....kwa maana kula au kupekecha meno....ambayo sio kweli.

Kuna vijidudu vinatumia sukari na vinapatikana kinywani. Sasa hivi vijidudu vinatumia sukari ila vinatoa acid inayoozosha meno.....
Kwa hiyo kimsingi bacteria hawatoboi meno....ila wanafanya fermentation ya sukari na kupata acid inayoharibu meno.

Asante mkuu kwa maelezo mazuri, hivi mbali na kuacha kutumia vitu vya sukari ni dawa gani inaweza tumika kuweka kinywa sawa chenye meno yaliyoanza kutoboka?
 
Asante mkuu kwa maelezo mazuri, hivi mbali na kuacha kutumia vitu vya sukari ni dawa gani inaweza tumika kuweka kinywa sawa chenye meno yaliyoanza kutoboka?

Sijui.
Labda aje dentist.....mimi sio dentist wala anything close.
 
Asante mkuu kwa maelezo mazuri, hivi mbali na kuacha kutumia vitu vya sukari ni dawa gani inaweza tumika kuweka kinywa sawa chenye meno yaliyoanza kutoboka?
Week iliiyopita nilienda muhimbili kwalengo la kutoa jino lakini nilizibwa tuu. nikauliza nifanyeje meno yangu yasiharibike tena maana nilikuwa nikikumbuka maumivu niliyopitia hapana kwakweli sitaki kuumwa tena jino
Daktari alishauri ni muhimu kupiga mswaki usiku sana ni bora uache hata asubuhi lakini usiku ndiyo muda ambao mambo mengi yanafanyika hasa katika kinywa lakini kama umeswaki vizuri na dawa aina ya COLGATE na FOREVER ni dawa ambazo zina floride nyingi katika kuyakinga meno.
Epuka kula vitu vya sukari sana itakusaidia
 
Mabaki ya chakula mdomoni yakiwa yana decompose in presence of bacteria ndo meno utoboka

Ushauri;

Piga mswaki mara tu umalizapo kula asubuh, mchana na usiku.
 
Ushauri;

Piga mswaki mara tu umalizapo kula asubuh, mchana na usiku.[/QUOTE]
Asantee mkuu!
 
Mabaki ya chakula mdomoni yakiwa yana decompose in presence of bacteria ndo meno utoboka

Ushauri;

Piga mswaki mara tu umalizapo kula asubuh, mchana na usiku.

Asante Mkuu
 
Week iliiyopita nilienda muhimbili kwalengo la kutoa jino lakini nilizibwa tuu. nikauliza nifanyeje meno yangu yasiharibike tena maana nilikuwa nikikumbuka maumivu niliyopitia hapana kwakweli sitaki kuumwa tena jino
Daktari alishauri ni muhimu kupiga mswaki usiku sana ni bora uache hata asubuhi lakini usiku ndiyo muda ambao mambo mengi yanafanyika hasa katika kinywa lakini kama umeswaki vizuri na dawa aina ya COLGATE na FOREVER ni dawa ambazo zina floride nyingi katika kuyakinga meno.
Epuka kula vitu vya sukari sana itakusaidia

Asantee!
 
Mzoe kupiga mswaki anagalau mara mbili kwa siku ili uepuke kutoboka meno, yaani caries/cavities.
 
Ingia kwenye blog ya mzizimkavu mazee mwanzo-mwisho au kwenye fb yake mbona yuko doktar huyu.muulze mzizimkavu atakujibu kiprofeshino.
 
Back
Top Bottom