Wafamasia acheni kuwa kituko, simamieni taaluma

Wafamasia acheni kuwa kituko, simamieni taaluma

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Inashangaza kuona taaluma ambayo pengine ingetakiwa kua msaada kwa taifa letu lakini imegeuka kua ni kichaka cha vioja. Kuna mdau alikuja kulalamika humu siku moja ya kwamba Baraza la famasia na Chama cha wafamasia wamejikita kwenye kufungia maduka ya watu na kujiwekea ubinafsi wa wao pekee kufanya biashara ya dawa badala ya kujikita kwenye taaluma yao na kulisaidia taifa.Sasa nimemuelewa huyo mdau humu.

KUHUSU TUKIO LA TURIANI MFAMASIA KUMNWESHA MGONJWA DAWA YA UPELE.

Tunaposema chama cha wafamasia na baraza la famasia badala ya kushughulika na matatizo ya watu wao wanajikita kwenye ugomvi na fani ziingine nani auze dawa na nani asiuze dawa, wanaacha mambo muhimu katika kusimamia taaluma ili kulinda afya za watanzania.

Haya, walizoea kusema manesi na madaktari kwenye maduka ya madawa ndio wanaotoa dawa kimakosa,je, huko TURIANI Morogoro ni daktari au Nesi ndiye aliyetoa dawa? Ilikuwaje Mwanafunzi ambaye amefundishwa na Mfamasia aliyefunzwa akaiva akamywesha mgonjwa dawa ya upele? Huyu anayeitwa Mwanafunzi wa famasia ilikuwaje akatoa dawa peke yake?
Alaumiwe nani hapa?

Kukosekana kwa umakini katika taaluma hii na kujikita kwenye maslahi binafsi ndiyo matatizo yake haya. Kitendo kilichofanyika kule TURIANI ni cha aibu na kinaonyesha jinsi ambavyo katika taifa letu tuna watu wa ajabu. Kumnywesha mgonjwa dawa ya Upele ni kesi ya jinai na sijui ni kwanini hili jambo linachukuliwa poa.
 
Almost every professional mishaps happen..acha ujuaji... na ndege zinazoanguka unawashaurije marubani
 
ushaambiwa aliyekosea maelekezo kwa mgonjwa ni mwanafunzi aliekuwepo kwenye mafunzo ya vitendo, sasa kama ungekua unajua uhalisia wa vituo vya afya hapa nchini usingeandika uzi wa kipuuzi kama huu, kimsingi mwanafunz huyo alitakiwa kuwa chini ya uangalizi lakini sio rahisi kila muda wanafunzi watakua chini ya uangalizi hospitali kwasababu kiuhalisia wafanyakazi wenye taaluma ya dawa ni wachache mahospitalini na ninaimani muangalizi wake alikua na majukumu mengine, lakini pia usipende sana kugeneralize neno "wafamasia" kwa kuwa nina uhakika icho kituo cha afya tajwa hakina mfamasia pale bali wataalamu wa dawa wenye ngazi tofaut ya elimu ambayo haijafikia shahada ya famasia
 
Kuna binamu yangu kaenda India kusoma doctor of pharmacy. Hiiiiiiiii angejua ajira za wamafamasia Ni za mchongo na take home yenyewe magumashi kwa hapa bongo
 
Back
Top Bottom