Wafanya biashara katika huu mgomo hamko pamoja, shitukeni

Blac kid

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
6,686
Reaction score
7,497
Nyie wafanyabiashara katika mgomo wa leo napenda kuwataarifu kwamba hamko pamoja, Nikijikita zaidi katika mji wa Kahama Shinyanga ni kweli maduka hapa centre hayajafunguliwa, lakini wafanyabiashara wengi tu wanawasiliana na wateja wao na biashara wanafanyiana nyumbani kwenye maghala. Bahati mbaya kuna baadhi ya wafanyabiashara kama wenye feremu za autospares, lubricants, cosmetics n.k hawana maghala naona mtaathirika zaidi kama mgomo utachukua muda mrefu.

Jaribuni kufikiria sababu dhumuni la mgomo hoja zake ni vigumu kuzitetea, yaani ukimweleza mtu bila chenga kabisa inaonekana ni ukwepaji wa kodi!!
 
Hata leo naona mwendo ni uleule nyie businessman legezeni sababu hoja zenu hazina mashiko!!
 
Hivi tatizo ni mashine za TRA, bei ya mashine au kodi yetu inakwenda wapi? Napata shida sana katika hili!!!!
 
Hivi tatizo ni mashine za TRA, bei ya mashine au kodi yetu inakwenda wapi? Napata shida sana katika hili!!!!

Mkuu jana walikuwa wanahojiwa star tv, yaani walikuwa hata hawaeleweki mara ohh mashine zina bei kubwa, mara oh hizi mashine ni dili la mtu tushamjua. Ni bora wangejenga hoja hatuoni maendeleo ya kodi tunazolipa, sababu network ya miundombinu ni mbovu kiasi kwamba inawawia ugumu ktk biashara zao, nadhani hapo wangepata sapoti kubwa kwa watumiaji wa mwisho ambao ndo walipakodi!!
 
Wanakwepa kodi, mashine zinawafanya walipe kodi bila shuruti, wao hawataki, wamezoea kuburuzana na TRA na kutoa rushwa ili walipe kodi kidogo.
Wajenge hoja ya muhim ambayo inaeleweka na sio kugusagusa tu.
 
Wanakwepa kodi, mashine zinawafanya walipe kodi bila shuruti, wao hawataki, wamezoea kuburuzana na TRA na kutoa rushwa ili walipe kodi kidogo.
Wajenge hoja ya muhim ambayo inaeleweka na sio kugusagusa tu.

Kweli kabisa mkuu!!
 

hawakwepi kodi kama ccm wanataka kodi wagawe hizo mashine bure sababu ni kwa manufaa yao na co ye2
 
hawakwepi kodi kama ccm wanataka kodi wagawe hizo mashine bure sababu ni kwa manufaa yao na co ye2

Ukitumia hisia kuamua mambo ni shida sana.
Hao wafanya biashara wapewe masine bure kwani hizo mashine ni pp?
Unesema bei ipunguzwe sawa.
Na ukiwafuatilia wafanya biashara wanasema hawazitaki hizo mashine hata bure, je hapo anamaana gani?
 
ushauri wangu kwa TRA naomba sana wale wenye kupangisha maeneo ya biashara ni wakwepaji wakubwa wa kodi. Kodi wanazotoza kwa wapangaji/wafanyabiashara ni kubwa mno na za kutisha lakini hawalipi kodi. Ebu anzeni na wapangishaji wa maeneo ya biashara kwanza.
 
Halafu katika mgomo huu wengi ni wasindikizaji tu, walengwa wanafanya biashara zao kama kawaida,...wanaotakiwa kuwa na hizo mashine ni wale ambayo mapato yao kwa mwaka yapo juu ya milioni 40 TZS..sasa wafanyabiashara wadogo ndio wanaoongoza kwa mgomo...
 
Wafanyabiasharawengi hawana shule ndo mana hata mgomo wao uko kichizichizi
 
......sell the most luxurious ...however are not registered in tra no body including tra commissioner general can say anything for fear of retribution
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…