flood
Senior Member
- Jul 10, 2017
- 121
- 188
Leo naomba niongee na wafanyabiashara hasa hawa wa rejareja. Kuna hii tabia inaboa sana na inatufanya tusijiamini wakati wa kufanya manunuzi kama vile hukujiandaa maana ukijidai kupack kama vile uko Nakumati (sijui kama watarudi) unaweza ukaumbuka.
Kifupi ni kwamba unajua kabisa hiki kikombe ni Tsh 500 ila utaambiwa Tsh 2000 ukimuambia punguza atakuambia Tsh 1800 ukiondoka anakuita kwani wewe una shilingi ngapi?Ukimtajia anakuambia haifai ila mwisho atakuambia basi leta tu.
Hii tabia imenifanya nihamishie shopping zangu kwa wahindi na kiukweli hawa jamaa wanajua biashara kwanza bidhaa zao ni genuine zina ubora, upande wa bei vizuri sana na hata warrant zao ni za kuaminika.
Hebu tubadilike katika hili ukipata faida Tsh 200 na ukaletewa wateja wengine 10 utakuwa na faida ya Tsh 2000 kuliko kusubiri faida ya Tsh 500.
Kifupi ni kwamba unajua kabisa hiki kikombe ni Tsh 500 ila utaambiwa Tsh 2000 ukimuambia punguza atakuambia Tsh 1800 ukiondoka anakuita kwani wewe una shilingi ngapi?Ukimtajia anakuambia haifai ila mwisho atakuambia basi leta tu.
Hii tabia imenifanya nihamishie shopping zangu kwa wahindi na kiukweli hawa jamaa wanajua biashara kwanza bidhaa zao ni genuine zina ubora, upande wa bei vizuri sana na hata warrant zao ni za kuaminika.
Hebu tubadilike katika hili ukipata faida Tsh 200 na ukaletewa wateja wengine 10 utakuwa na faida ya Tsh 2000 kuliko kusubiri faida ya Tsh 500.