The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Wananchi na wafanyabiashara wa stendi mabasi ya Mlowo wamekoshwa na hatua za utekelezaji wa umaliziaji uliokuwa ukisua sua muda mrefu wa vibanda na miundo mbinu yake.
Wafanyabiashara hao, kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na Mkuu wa Mkoa aliopo sasa Mkoani Songwe, Daniel Chongolo, wamependeleza kituo hicho mpaka kuanza kutumika kwa stendi hiyo. Hivyo basi, wameomba kituo hicho kipewe jina la Stendi ya Mabasi ya Chongolo.
Wakipiga stori na Habari Jamii Tz, wamesema itakuwa busara na zawadi ya pekee kwa Chongolo kupewa jina la stendi hiyo, ikiwa kama shukrani kwao, Wanasongwe, kwake.
"Tumeona halmashauri mbalimbali Mkoani Songwe zikizipa shule majina ya Wakuu wa Wilaya, au wakurungezi, wabunge na wenyeviti wa Halmashauri. Nasi tunaiomba Halmashauri yetu ya mbozi stendi hii ya mlowo ipewe jina la chongolo ili kumuenzi kwa juhudi zake alizozifanya hapa."
Michael Punde, mfanyabiashara Machinga
Wafanyabiashara hao wamekwenda mbali zaidi kuwa bila Chongolo, stendi hiyo isingefanya kazi, kwani maagizo aliyatoa na usikivu wa Halmashauri ya mbozi ndio yamepelelekea stendi hiyo kuanza kutumika kwa kasi.
Imekuwa ni desturi ya halmashauri nyingi Tanzania kuwapa majina viongozi wenye mchango mzuri kwa Wananchi, kama vile kuwapa majina ya shule na maeneo mengine, hivyo kumuenzi kiongozi huyo kama alama ya kukumbukwa.
Wafanyabiashara hao, kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na Mkuu wa Mkoa aliopo sasa Mkoani Songwe, Daniel Chongolo, wamependeleza kituo hicho mpaka kuanza kutumika kwa stendi hiyo. Hivyo basi, wameomba kituo hicho kipewe jina la Stendi ya Mabasi ya Chongolo.
Wakipiga stori na Habari Jamii Tz, wamesema itakuwa busara na zawadi ya pekee kwa Chongolo kupewa jina la stendi hiyo, ikiwa kama shukrani kwao, Wanasongwe, kwake.
"Tumeona halmashauri mbalimbali Mkoani Songwe zikizipa shule majina ya Wakuu wa Wilaya, au wakurungezi, wabunge na wenyeviti wa Halmashauri. Nasi tunaiomba Halmashauri yetu ya mbozi stendi hii ya mlowo ipewe jina la chongolo ili kumuenzi kwa juhudi zake alizozifanya hapa."
Michael Punde, mfanyabiashara Machinga
Wafanyabiashara hao wamekwenda mbali zaidi kuwa bila Chongolo, stendi hiyo isingefanya kazi, kwani maagizo aliyatoa na usikivu wa Halmashauri ya mbozi ndio yamepelelekea stendi hiyo kuanza kutumika kwa kasi.
Imekuwa ni desturi ya halmashauri nyingi Tanzania kuwapa majina viongozi wenye mchango mzuri kwa Wananchi, kama vile kuwapa majina ya shule na maeneo mengine, hivyo kumuenzi kiongozi huyo kama alama ya kukumbukwa.