Wafanyabiashara Tanzania washauriwa kuanzisha Viwanda

MPadmire

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
3,957
Reaction score
3,245
Radio One taarifa ya habari -- WaTanzania wenye uwezo na wafanyabiashara wameshauriwa kuanzisha viwanda badala ya kuwa wachuuzi..

Nashangaa wafanyabiashara wakubwa Tanzania wanaenda China kubeba viatu vilivyotengenezwa kwa mabox na kuwauzia watanzania wenzao.....

Nguo za China ni hafifu mno,,,,, Tanzania tuna pamba nzuri na nyingi ajabu

Kuna bidhaa hafifu sana zinaingizwa Tanzania, TBS wako wapi?
 

NI NANI HUYO ANAWAAMBIA WAJENGE VIWANDA?
Nina wasi wasi na uraia wako maana hujui sera za nchi hii hazilengi kujenga viwanda bali kuuwa viwanda. sasa ndugu wakijenga viawanda wataenda kuuza wapi wakati wenye viwanda vya sukari wamekosa soko la kuuza sukari. yaani wakiwa kwenye majukwaa wanaonekana wanapenda watu wajenge viwanda.wakitoka hapo wao wenyewe wanaenda kuagiza bidhaa toka nje. fikiria tunazalisha mchele lakini wanaagiza limchele libovu toka nje
 
Li Pinda ndo liliongea hivyo. Yaani maneno yao na matendo yao havifanani kabisa.
 
Ni kweli wadau, hawa wanaongea kiunafiki maana maneno yao hayalingani na matendo.

Wanaagiza sukari nje, halafu bila kodi, wakati huo huo viwanda vyetu vinatozwa kodi kubwa... Embu shangaa mbolea kutoka China ni rahisi kuliko Mbolea ya Minjingu ambayo wamechimba sulphate hapa hapa

Cementi kutoka nje ni rahisi kuliko Cement ambayo wanachimba material hapa hapa

Wanaagiza Nguo China halafu pamba ya wasukuma wanaibeza...
 
Tufungue viwanda kwa umeme upi wa uhakika tulionao ? Na huo wa mgao tulionao ni ghali utafkiri umetokea mbinguni, ukishamaliza kuzalisha, mafuriko ya mchina yanakusubiri..
 
Je Magari 700 ya washa washa kununuliwa kwa ajili ya Polisi ni sahihi wakati huu?
 
Hii nchi inapenda kupata hela kupitia pale Bandarini wakiruhusu viwanda watakosa hela pale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…