Wafanyakazi: Kuna kazi aina nyingi duniani na zote zinategemeana

Wafanyakazi: Kuna kazi aina nyingi duniani na zote zinategemeana

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Nyingine zinahitaji ujuzi, elimu na tajriba ya kiwango cha juu ukilinganisha na nyingine.
Mifano​
1. Mhasibu: Mtaalamu wa kuweka hesabu ya fedha.
msahibu.JPG

2. Mhandisi/injinia: Mjuzi wa kutengeneza, kuhudumia na kuunda mitambo.
injinia.jpg

3. Tarishi/Katikiro: Anayehudumu ofisini kwa kutumwa kupeleka habari au ujumbe.
Tarishi.jpg

4. Bawabu: Alindaye mlangoni.
Bawabu.jpg

5. Topasi/chura: Asafishaye choo.


6. Tabibu/daktari/mganga: Mwenye ujuzi wa kutibu.
daktari.JPG

7. Muuguzi/mualisaji: Ahudumiaye wawele/wagonjwa
Wauguzi.jpg

8. Msarifu: Anayesimamia na kuidhinisha matumizi mazuri ya fedha katika shirika.
9. Dereva: Aendeshaye vyombo vya nchi kavu k.v. gari
dereva.JPG

10. Nahodha: Aendeshaye na kuongoza vyombo vya majini k.v. meli
nahodha.jpg



11. Rubani: Aendeshaye na kuongoza vyombo vya angani k.v.ndege
rubani.JPG

12. Utingo/taniboi: Mpakiaji na mpakuaji wa mizigo katika gari.
utingo.JPG

13. Hamali/mpagazi/mchukuzi: Abebaye mizigo kwa malipo.
mchukuzi.JPG

14. Machinga: Auzaye bidhaa rejareja kwa kuzungukazunguka.
machinga.JPG

15. Malenga: Mtunzi stadi wa mashairi na nyimbo.
malenga.JPG

16. Manju: Stadi wa kutunga na kuimba nyimbo katika ngoma.
manju.jpg

17. Kuli: Apakiaye na kupakua shehena za forodhani.
kuli.JPG

18. Dobi: Afuaye na kupiga nguo za watu pasi kwa malipo.
dobi.JPG
 
19. Sogora: Fundi wa kupiga ngoma.
sogora.JPG

20. Saisi: Atunzaye wanyama wanaopandwa k.v. punda na farasi.
Saisi_1.JPG



21. Msajili: Awekaye orodha ya kazi, vitu au viumbe.
View attachment 823781
22. Mkalimani/mtarijumani: Afasiriaye lugha moja hadi nyingine.
mkalimani.JPG

23. Sonara: Atengenezaye mapambo kwa kutumia madini.
sonara.jpg

24. Kinyozi: Anyoaye nywele.
kinyozi.JPG

25. Msusi/msosi: Asukaye watu nywele.
msusi.JPG

26. Ngariba: Apashaye wavulana tohara katika jando.
ngariba.JPG

27. Mkunga: Awasaidiaye wajawazito kujifungua.
mkunga.JPG

28. Kungwi: Afundishaye mwari wa kike au kiume.
29. Mhariri: Asomaye, kusahihisha na kusarifu makala, magazeti n.k.
mhariri.jpg

30. Mshenga: Atumwaye kupeleka habari za ndoa (posa).
mshega.jpg



31. Refa: Mwamuzi katika mchezo k.v. soka.
refa.jpg

32. Kasisi: Kiongozi wa kidini katika madhehebu fulani ya kikristo.
kasisi.JPG

33. Imamu: Kiongozi wa kidini katika madhehebu fulani ya kiislamu.
imamu.JPG

34. Hakimu: Aamuaye kesi katika mahakama.
hakimu.JPG

35. Kadhi: Hakimu wa kiislamu.
kadhi.JPG

36. Mlariba: Akopeshaye wengine pesa.
mlariba.jpg

37. Mwekezaji: Anayeweka mali au pesa katika mradi au biashara.
mwekezaji.jpg

38. Meneja: Msimamizi au kiongozi katika kampuni au shirika.
meneja.jpg
 
39. Karani: Afanyaye kazi ya kuandika k.m. barua na majarida.
karani.JPG

40. Kocha: Mwalimu wa mchezo k.v. soka.
kocha.JPG



41. Mkutubi: Ahifadhiye vitabu maktabani na kuviazimisha.
mkutubi.jpg

42. Mnajimu: Mwenye elimu ya nyota. Hutabiri mambo.
mnajimu.jpg

43. Mpigaramli: Abashiriaye kwa kupiga bao.
44. Mwajiri: Aandikaye mtu kwa kazi ya malipo au mshahara.
mwajiri.JPG

45. Mzegazega: Achotaye maji na kuyauza.
mzegazega.JPG

46. Dalali: Auzaye bidhaa katika mnada (soko la kushindania bei)
dalali.jpg

47. Manamba: Mfanyikazi wa muda katika shamba kubwa.
[resource: 2977, align: left]
48. Mnyapara: Msimamizi wa kazi.
mnyapara.jpg

49. Mhazili: Sekretari - Atunzaye barua na majarida na kuandika kwa mashine ofisini.
mhazili.jpg

50. Mhadhiri: Mwalimu katika chuo kikuu.
mhadhiri.jpg



51. Mwashi: Ajengaye nyumba kwa mawe.
mwashi.JPG

52. Mhunzi: Afuaye vitu vya madini ya chuma au bati.
Mhunzi.jpg

53. Seremala : Atengenezaye samani za mbao au miti.
Seremala.jpg

54. Mfinyanzi: Atengenezaye vyombo vya udongo k.m. vyungu.
mfinyanzi.JPG

55. Mvuvi: Afanyaye kazi ya kuvua samaki.
mvuvi.JPG

56. Mwanaanga: Afanyaye utafiti wa hali ya anga.
mwanaanga.JPG

57. Mkabidhi: Mtu atunzaye mali kwa ajili ya mwengine
58. Diwani: Anayewakilisha watu wake katika serikali za wilaya
59. Mzoataka: Anayeokota takataka
mzoataka.jpg

60. Kaimu: Anayeshikilia cheo au wadhifa fulani kwa muda


Zoezi A.
Zitaje kazi za wafuatao.
  • Mwalishi
  • Sarahangi
  • Mchuuzi
  • Mwamizi
  • Mfugaji
  • Mamantilie
  • Mlumbaji
  • Mgema
  • Mbunge
  • Baharia
  • Wakili
  • Mjumu
  • Diwani
  • Mrumba
  • Kandawala
  • Gambera


B. Taja watu wazifanyazo kazi hizi.
Aliyesomea diplomasia ni_________
Mtu afanyaye utafiti wa mambo ya sayari za juu__________
Mchezaji wa mpira wa miguu ni __________
Afanyaye kazi katika meli ni __________ .
Achezaye michezo ya riadha ni __________.
Raia anayejitolea kufanya kazi ya ulinzi ni __________
Askari katika jeshi la ulinzi __________
Anayeshughulika na sheria ni __________.
 
Back
Top Bottom