figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
Nyingine zinahitaji ujuzi, elimu na tajriba ya kiwango cha juu ukilinganisha na nyingine.
2. Mhandisi/injinia: Mjuzi wa kutengeneza, kuhudumia na kuunda mitambo.
3. Tarishi/Katikiro: Anayehudumu ofisini kwa kutumwa kupeleka habari au ujumbe.
4. Bawabu: Alindaye mlangoni.
5. Topasi/chura: Asafishaye choo.
6. Tabibu/daktari/mganga: Mwenye ujuzi wa kutibu.
7. Muuguzi/mualisaji: Ahudumiaye wawele/wagonjwa
8. Msarifu: Anayesimamia na kuidhinisha matumizi mazuri ya fedha katika shirika.
9. Dereva: Aendeshaye vyombo vya nchi kavu k.v. gari
10. Nahodha: Aendeshaye na kuongoza vyombo vya majini k.v. meli
11. Rubani: Aendeshaye na kuongoza vyombo vya angani k.v.ndege
12. Utingo/taniboi: Mpakiaji na mpakuaji wa mizigo katika gari.
13. Hamali/mpagazi/mchukuzi: Abebaye mizigo kwa malipo.
14. Machinga: Auzaye bidhaa rejareja kwa kuzungukazunguka.
15. Malenga: Mtunzi stadi wa mashairi na nyimbo.
16. Manju: Stadi wa kutunga na kuimba nyimbo katika ngoma.
17. Kuli: Apakiaye na kupakua shehena za forodhani.
18. Dobi: Afuaye na kupiga nguo za watu pasi kwa malipo.
Mifano
1. Mhasibu: Mtaalamu wa kuweka hesabu ya fedha.2. Mhandisi/injinia: Mjuzi wa kutengeneza, kuhudumia na kuunda mitambo.
3. Tarishi/Katikiro: Anayehudumu ofisini kwa kutumwa kupeleka habari au ujumbe.
4. Bawabu: Alindaye mlangoni.
5. Topasi/chura: Asafishaye choo.
6. Tabibu/daktari/mganga: Mwenye ujuzi wa kutibu.
7. Muuguzi/mualisaji: Ahudumiaye wawele/wagonjwa
8. Msarifu: Anayesimamia na kuidhinisha matumizi mazuri ya fedha katika shirika.
9. Dereva: Aendeshaye vyombo vya nchi kavu k.v. gari
10. Nahodha: Aendeshaye na kuongoza vyombo vya majini k.v. meli
11. Rubani: Aendeshaye na kuongoza vyombo vya angani k.v.ndege
12. Utingo/taniboi: Mpakiaji na mpakuaji wa mizigo katika gari.
13. Hamali/mpagazi/mchukuzi: Abebaye mizigo kwa malipo.
14. Machinga: Auzaye bidhaa rejareja kwa kuzungukazunguka.
15. Malenga: Mtunzi stadi wa mashairi na nyimbo.
16. Manju: Stadi wa kutunga na kuimba nyimbo katika ngoma.
17. Kuli: Apakiaye na kupakua shehena za forodhani.
18. Dobi: Afuaye na kupiga nguo za watu pasi kwa malipo.