Wafanyakazi wa serikali Kenya kulazimika kuvaa nguo zilizotengenezwa Kenya kila ijumaa

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
9,524
Reaction score
13,682
Ili kuinua uchumi na kukuza viwanda vya nguo vya Kenya serikali imeamuru wafanyakazi wote wa serikali na umma kuvaa nguo zilizotengenezwa Kenya kutokana na pamba iliyolimwa nchini humo kila ijumaa na siku za sikukuu. Kwa kufanya hivyo inategemewa kilimo cha pamba kukuzwa na pia kuvipatia soko viwanda vya nguo.

Je Tanzania tuige mfano huo ili kukuza zao la pamba na viwanda vya nguo?
 
Tanzania tuige Mfano ili kuinua uchumi wa Nchi yetu
 
Wasitutishe bhana na sisi waha huku kigoma tuna viwanda vya kutengeneza nguo za magome ya miti maarufu kwa jina la MPUZU na tunazivaa muda wowote,
kusupport viwanda vyetu!
 
Tuige mfano! Tuvae pamba ghafi? Tanzania hatiwezi kushindana na Kenya, Kenya inajengwa na wakenya wote bila kujali vyama, sisi CCM inataka iijenge nchi peke yake hiki ni kikwazo kuujenga uchumi wetu, viwanda vya nguo viko wapi?
Kwa ubishi basi!
 
Tuige mfano! Tuvae pamba ghafi? Tanzania hatiwezi kushindana na Kenya, Kenya inajengwa na wakenya wote bila kujali vyama, sisi CCM inataka iijenge nchi peke yake hiki ni kikwazo kuujenga uchumi wetu, viwanda vya nguo viko wapi?
Kwa ubishi basi!
Tuna pamba ya kutosha kwa nini tusifufue viwanda vyetu? Kwa nini serikali isitafute mwekezaji hata kwa ubia?
 
Tuna pamba ya kutosha kwa nini tusifufue viwanda vyetu? Kwa nini serikali isitafute mwekezaji hata kwa ubia?
Wakenya hawategemei wawekezaji kama sisi, wanajenga viwanda wenyewe.
Sisi tuendelee na majivuno na mbwembwe.
 
Ungeua km hakuna taifa lenye kutegemea wawekezaji km Kenya usingeongea hvyo.
Wakenya hawategemei wawekezaji kama sisi, wanajenga viwanda wenyewe.
Sisi tuendelee na majivuno na mbwembwe.
 
hatutaki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…