KERO Wafanyakazi wa SGR (Lot 3,4,5,6) tumerudishwa nyumbani na hawajaingiza michango ya NSSF kwa Miezi 14

KERO Wafanyakazi wa SGR (Lot 3,4,5,6) tumerudishwa nyumbani na hawajaingiza michango ya NSSF kwa Miezi 14

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Sisi wafanyakazi wa SGR kwa sasa tupo nyumbani tukiwa hatujui hatima yetu juu ya kinachoendelea kuhusu project hiyo hasa kuanzia Lot 3 na 4.

Ipo hivi, Lot 3 na 4 kwa sasa zimesimama, wafanyakazi tuliokuwa katika mradi huo kwa sasa tupo tu nyumbani, awali tuliambiwa tukae nyumbani hadi tutakapojulishwa, wengine wakaambiwa wakae home kwa wiki mbili.

Zilipoisha, tukarejea kazini, tukakutana na agizo lingine kuwa tunatakiwa kuendelea kuwa nyumbani kwa wiki mbili nyingine.

Upande wa wenzetu ambao wapo Lot 5 (Isaka - Mwaka) na 6 (Tabora - Kigoma) napo hali ni hivyohivyo kwa kuwa huko walikuwa katika mchakato wa kuanza, mambo yamesimama na hakuna kinachoendelea.

Pamoja na yote jambo la kushukuru ni kuwa tunaendelea kulipwa kama kawaida, japo tunalipwa basic salary bila nyongeza nyingine yoyote, wale ambao hawakuwa na mkataba wao hawalipwi.

Jambo la kusikitisha ni kuwa pamoja na yote hayo yanayoendelea maingizo ya fedha zetu za NSSF hayajaingizwa tangu Desemba 2022 licha ya kuwa watu tumekuwa tukikatwa kwenye mishahara yetu kwa muda wote huo.

Pia soma ~ Serikali yashindwa kulipa wakandarasi, mradi wa SGR Mwanza wasimama
 
Wafanyakazi wa Mkandarasi Yapi Merkez anayejenga Reli ya Kisasa ya SGR (Lot 2 km 444) upande wa Dodoma Station wamegoma kushinikiza kuingiziwa michango yao ya Mfuko wa Hifadhi wa NSSF ambayo wanadai hadi sasa ni mwaka mmoja na miezi mitano tangu walipingiziwa mara ya mwisho.

Wanadai mgomo huu umekuja baada ya kuvumilia kwa kipind kirefu kukiwa hakuna majibu yanayoeleweka kutoka kwa Mkandarasi zaidi ya kujulisha “Mtalipwa mwezi ujao”.

Wafanyakazi hao wamuamua kushikilia msimamo huo wakidai hawatafanya kazi hadi michango yao itakapoingizwa, wakidai kuwa wamekuwa wakikatwa kwenye mishahara yao lakini makato hayo hayafikishwi kwenye mamlaka husika (NSSF).

photo_2024-06-03_17-25-19.jpg

photo_2024-06-03_17-25-18.jpg

Pia soma ~ Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa kagua SGR, Treni kuanza kufanya kazi Juni 14 (Dar-Moro), Julai 25 (Dar-Dom)
 
Back
Top Bottom