Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
IDADI ya watu ambao bado haijafamika wamekufa baada ya kufunikwa na mlima uliosababishwa na mafuriko yaliyotokea usiku wa kuamkia leo huko kata ya Manka Wilayani Same mkoani Kilimanjaro. Msiba huo umetokea baada ya mlima mmoja kumeguka na kufunika zaidi ya nyumba kumi na inadaiwa watu wote waliokuwa wamelala ndani, wamepoteza maisha kufuatia tukio hilo na kudaiwa nyumba hizo zimesombwa kwa maji hayo.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo katika majira ya saa 7:00 usiku, katika kata ya Miamba kitongoji cha Manka wilayani Same.
Maafa hayo yametokana na mvua zilizonyesha mfululizo kwa siku tatu na kusababisha mlima huo kumeguka.
Na mvua huzo kubwa zimekuwa zikinyesha kwa siku tatu mfululizo katika majira ya usiku tu, hali hiyo imesababisha udongo na miamba kumeguka na kufunika nyumba kumi katika kitongoji cha Manka, huku watu wakiwa wamelala ndani.
Imedaiwa katika juhudi za kuwaokoa katika nyumba hizo hakuna mtu ambaye ameokolewa akiwa hai.
Mbunge wa jimbo la Same Mashariki Mhe. Anne Kilango amesema kuwa hadi sasa miili kumi na moja imeshatolewa chini ya kifusi na juhudi zaidi zinaendelea kuokoa miili hiyo.
Amesema hali ya uokoaji inakuwa ngumu kutokana na nyumba hizo kuwa chini ya milimani ambako sio rahisi kufikika kwa vyombo vya uokoaji.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=3523422&&Cat=1
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo katika majira ya saa 7:00 usiku, katika kata ya Miamba kitongoji cha Manka wilayani Same.
Maafa hayo yametokana na mvua zilizonyesha mfululizo kwa siku tatu na kusababisha mlima huo kumeguka.
Na mvua huzo kubwa zimekuwa zikinyesha kwa siku tatu mfululizo katika majira ya usiku tu, hali hiyo imesababisha udongo na miamba kumeguka na kufunika nyumba kumi katika kitongoji cha Manka, huku watu wakiwa wamelala ndani.
Imedaiwa katika juhudi za kuwaokoa katika nyumba hizo hakuna mtu ambaye ameokolewa akiwa hai.
Mbunge wa jimbo la Same Mashariki Mhe. Anne Kilango amesema kuwa hadi sasa miili kumi na moja imeshatolewa chini ya kifusi na juhudi zaidi zinaendelea kuokoa miili hiyo.
Amesema hali ya uokoaji inakuwa ngumu kutokana na nyumba hizo kuwa chini ya milimani ambako sio rahisi kufikika kwa vyombo vya uokoaji.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=3523422&&Cat=1