Waganga wa kienyeji kwenye TV station za Tanzania

Waganga wa kienyeji kwenye TV station za Tanzania

Nyati

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2009
Posts
2,521
Reaction score
1,906
Wakuu Salaam,

Jana usiku niliangalia kipindi cha Star TV ambapo mmoja wa waganga wa kienyeji alikuwa ananadi dawa zake pamoja na huduma nyingine anazozitoa. Kwa ujumla ni kama vile jamii yetu imechanganyikiwa na kila mtu anatumia kila njia kuhamisha umiliki wa fedha kutoka kila mahali hadi mfukoni mwake.

Jamaa anasema ukienda kwake yeye anaangalia kucha tu na kukutabilia maisha yako ya baadaye, anasema hata ukimpeleka mwanao yeye atakutabiria na kukupa ushauri na madawa ili afanikiwe maishani mwake kupitia kusoma KUCHA zake. Baadaye pia aliongelea kusoma macho na kutoa tabiri hizo hizo!!!

Alikuwa hana ajenda maalumu bali kurukia vitu mbali mbali kufanikiwa maishani, magonjwa ya macho, uzazi, nguvu za kiume, viagra, kupata watoto, n.k. Alikuwa anajitahidi kuongea kiingereza kwa shida

Kwa kweli nimesikitishwa na hali hii ambayo sasa imeshika kasi lakini nashangaa inakuwaje wamiliki wanatoa muda (hata kama ni kwa pesa ) kwa watu kama hawa???!!!!!!.

Huhitaji kupiga ramli kujua kuwa ni wapotoshaji wakubwa hawa. Kama kuna mwana JF ambaye anafanya kazi ktika vituo hivi, naomba atujuze hasa ni kwa nini wanaruhusiwa, Je uwa mnahakiki wanachoongea ama mnajali pesa tu.

Nawasilisha
 
siku za mwisho kila tv station ina mzee wa upako mtume sijui nni na kina manyaunyau ndani lol
 
Hivi yule kumbe alikuwa mganga wa kienyeji?
 
Hata mimi nilimshangaa alivosema unaweza kumjua mtu kwa kumuangalia kucha au macho.
 
Tunaomba wataalam watufafanulie juu ya "kucha na macho".Ila du!hata kama sijui kiingereza,jamaa aliniacha hoi
 
kuna point moja ngoja niikumbuke...bt hapa madaktari hawaijui anaijua yeye tu...ngoja kwanza manake kichwa kimestack kwanza
 
Mkuu Nyati, binafsi sidhani kama tatizo ni watu wa luninga(wamiliki,waandishi, waandaaji vipindi) kwani wao hufanya biashara, na inalipa.

Tatizo nadhani ni sisi wananchi, tusidanganyanye watanzania tunapenda sana njia za mkato(Short cut ways),
Kwa mfano mtu hataki kutumia dawa nyingi ingawa zitamtibu, kwa vile tu atatumia kwa muda mrefu na pengine katika maisha yake yote, ila anataka COMBINATION, anataka kusikia dawa fulani ya mitishamba ambayo atasikia "inatibu" Kisukari, Shinikizo la damu, UKIMWI, Matatizo ya figo n.k.. kwa experience yangu ndogo, utakutana na Wagonjwa wengi tayari wakiwa na Complications, wakiwa wameamviwa wasitumie dawa za hospitali bali kuendelea na hiyo mitishamba( SIKATAI kuna mitishamba inafanya kazi lakini si kaktika kiwango tuonacho kila leo katika habari)...

Ni lini unaona daktari akiwa katika luninga/radio akishawishi watu waende hospitali...HAKUNA, hiyo ni kwa sababu hakuna biashara katika uhai wa binadamu, lakini si kwa dawa tuzisikiazo.

Lakini Serikali pia ina tatizo hapa, kila leo utasikia dawa imethibitishwa na TFDA(Tanzania Food and Drug Authority) etc..lakini jambo tunalopaswa kujua ni hili dawa yeyote ile, ina madhara fulani(side effects) hata kama ni kidogo..nanachoshindwa kuelewa ni kwamba TFDA inaruhusu madawa haya kuuzwa ikiwa hakuna hata screening ya sumu(TOXICOLOGY SCREENING) hapa Tanzania..tulishuhudia wakati fulani "kikombe cha babu" na wengine kama hao, ambapo viongozi na wananchi walitumia, leo hii imesahaulika, na hakuna ajuaye long term side effects ya kutumia dawa ile..!!

Nadhani Serikali kwa upande wake ijaribu ku-moderate dawa hizi( Alternative/Harbal medicine) na wanananchi tusipende we should look for best solution and not the easy solution.
 
Mkuu Nyati, binafsi sidhani kama tatizo ni watu wa luninga(wamiliki,waandishi, waandaaji vipindi) kwani wao hufanya biashara, na inalipa.

Tatizo nadhani ni sisi wananchi, tusidanganyanye watanzania tunapenda sana njia za mkato(Short cut ways),
Kwa mfano mtu hataki kutumia dawa nyingi ingawa zitamtibu, kwa vile tu atatumia kwa muda mrefu na pengine katika maisha yake yote, ila anataka COMBINATION, anataka kusikia dawa fulani ya mitishamba ambayo atasikia "inatibu" Kisukari, Shinikizo la damu, UKIMWI, Matatizo ya figo n.k.. kwa experience yangu ndogo, utakutana na Wagonjwa wengi tayari wakiwa na Complications, wakiwa wameamviwa wasitumie dawa za hospitali bali kuendelea na hiyo mitishamba( SIKATAI kuna mitishamba inafanya kazi lakini si kaktika kiwango tuonacho kila leo katika habari)...

Ni lini unaona daktari akiwa katika luninga/radio akishawishi watu waende hospitali...HAKUNA, hiyo ni kwa sababu hakuna biashara katika uhai wa binadamu, lakini si kwa dawa tuzisikiazo.

Lakini Serikali pia ina tatizo hapa, kila leo utasikia dawa imethibitishwa na TFDA(Tanzania Food and Drug Authority) etc..lakini jambo tunalopaswa kujua ni hili dawa yeyote ile, ina madhara fulani(side effects) hata kama ni kidogo..nanachoshindwa kuelewa ni kwamba TFDA inaruhusu madawa haya kuuzwa ikiwa hakuna hata screening ya sumu(TOXICOLOGY SCREENING) hapa Tanzania..tulishuhudia wakati fulani "kikombe cha babu" na wengine kama hao, ambapo viongozi na wananchi walitumia, leo hii imesahaulika, na hakuna ajuaye long term side effects ya kutumia dawa ile..!!

Nadhani Serikali kwa upande wake ijaribu ku-moderate dawa hizi( Alternative/Harbal medicine) na wanananchi tusipende we should look for best solution and not the easy solution.
Mimi nimeandika kwa sababu juzi mwanangu umri miaka 2 na zaidi kidogo alinishangaza kwa kuniambia " Wewe Mbaya! " kama mara tatu hivi huku akinionyesha kidole, baadaye niliambiwa kuwa ameona kwenye KOMEDI ndipo kaiga.

Hivyo lazima tutafute jinsi ya kuwasaidia watoto wasioelewa, jamaa alikuwa akionyesha kuwa yeye akishakupa dawa basi huhitaji jitihada zozote zile wewe ni kulala tu maisha yatakuwa mazuri. Hii ni mbaya sijui kama kwa wenzetu kuna sheria ya kuzuia upotoshaji huu
 
Hata kuna waganga fulani ktk ch10 j2 asubuhi ni waongo sana wanajifanya wanajua mambo ya afya kumbe wanadanganya tu..na kibwana dachi wala hakufanya home work yake ya kuelewa masuala ya afya ambayo mgeni alikia anaongelea kwani alikua anadanganywa live bila chenga!
 
Back
Top Bottom