Wagombea Urais watakaopata kura asilimia 3-5 kuwa Wabunge

Wagombea Urais watakaopata kura asilimia 3-5 kuwa Wabunge

Regia Mtema

R I P
Joined
Nov 21, 2009
Posts
2,970
Reaction score
866

Wakuu
Nimeona ni vema niwaletee swali la Msingi la Mhonga Said (MB) VIti Maalum CHADEMA alilouliza kwenye Bunge Nov 4 Mwaka huu. Akitaka kufahamu yafuatayo na Jibu alilopewa na Waziri.

Jamani hivi kweli hii ni sahihi,kung'an'gania Katiba, Katiba,Kwani Katiba ni kitu gani mpaka isibadilishwe,Hivi CCM wanadhani watakuwa madarakani milele?

Swali lilikuwa kama ifuatavyo:

Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kuleta mabadiliko na Sheria ya Uchaguzi kufuatia taarifa iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu katika hotuba yake ya Bajeti; kawa kuwa Bunge ndiyo chombo kikuu kinachotunga Sheria na kuamua juu ya mustakabali wa maisha ya Watanzania:-

(a) Je, Serikali haioni kuwa kuna haja ya kuweka kifungu kinachoruhusu wagombea Urais wote watakaopata asilimia tatu hadi tano ya kura za Urais kuwa wawakilishi ndani ya Bunge kama nchi nyingine ili kutimiza matakwa ya demokrasia?

(b) Je , Serikali haioni kuwa Sheria hiyo ikiwaruhusu wagombea Urais hao kuwa wawakilishi itasaidia kuchangia mawazo katika yale yaliyowasukuma kugombea nafasi hiyo?


Na haya ndio Majibu ya Waziri Marmo Phillip

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhonga Said Ruhwanya, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-


Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali ina mpango wa kuleta Bungeni mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi. Mapendekezo ya Marekebisho hayo ya Sheria ya Uchaguzi yana lengo la kuondoa kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na chaguzi ndogo zilizofanyika baada ya Uchaguzi Mkuu huo. Madhumuni makubwa ya marekebisho hayo ni kuiwezesha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuendesha mchakato wa uchaguzi kwa wepesi na ufanisi zaidi hasa kwa kuwa Sheria za uchaguzi zinahusu zaidi mambo ya mchakato wa uchaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuweka kifungu kinachoruhusu wagombea Urais wote watakaopata asilimia tatu hadi tano ya kura za Urais kuwa wawakilishi ndani ya Bunge ni suala la Kikatiba. Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 inatamka bayana aina ya Wabunge na sifa za kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano.Namshauri Mheshimiwa Mbunge kukubali wagombea wajiimarishe kuwania ushindi na siyo kulenga kuwa wawakilishi wa vyama Bungeni kwa kuwa washindi wateule watakuwa wamepatikana na kujaza nafasi zote kwa mujibu wa Katiba.


Wakuu hebu tuajdili haya majibu yanaridhisha kweli?hayajakaa kukuandamizi na kbaka demokarsia kweli?hivi je kweli Tanzania ni democratic country?mbona upinzani uanakandamizwa sana?
 
Wakuu
Nimeona ni vema niwaletee swali la Msingi la Mhonga Said (MB) VIti Maalum CHADEMA alilouliza kwenye Bunge Nov 4 Mwaka huu. Akitaka kufahamu yafuatayo na Jibu alilopewa na Waziri.

Jamani hivi kweli hii ni sahihi,kung'an'gania Katiba, Katiba,Kwani Katiba ni kitu gani mpaka isibadilishwe,Hivi CCM wanadhani watakuwa madarakani milele?

Swali lilikuwa kama ifuatavyo:

Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kuleta mabadiliko na Sheria ya Uchaguzi kufuatia taarifa iliyotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu katika hotuba yake ya Bajeti; kawa kuwa Bunge ndiyo chombo kikuu kinachotunga Sheria na kuamua juu ya mustakabali wa maisha ya Watanzania:-

(a) Je, Serikali haioni kuwa kuna haja ya kuweka kifungu kinachoruhusu wagombea Urais wote watakaopata asilimia tatu hadi tano ya kura za Urais kuwa wawakilishi ndani ya Bunge kama nchi nyingine ili kutimiza matakwa ya demokrasia?

(b) Je , Serikali haioni kuwa Sheria hiyo ikiwaruhusu wagombea Urais hao kuwa wawakilishi itasaidia kuchangia mawazo katika yale yaliyowasukuma kugombea nafasi hiyo?

Na haya ndio Majibu ya Waziri Marmo Phillip

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhonga Said Ruhwanya, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-


Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali ina mpango wa kuleta Bungeni mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi. Mapendekezo ya Marekebisho hayo ya Sheria ya Uchaguzi yana lengo la kuondoa kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na chaguzi ndogo zilizofanyika baada ya Uchaguzi Mkuu huo. Madhumuni makubwa ya marekebisho hayo ni kuiwezesha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuendesha mchakato wa uchaguzi kwa wepesi na ufanisi zaidi hasa kwa kuwa Sheria za uchaguzi zinahusu zaidi mambo ya mchakato wa uchaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuweka kifungu kinachoruhusu wagombea Urais wote watakaopata asilimia tatu hadi tano ya kura za Urais kuwa wawakilishi ndani ya Bunge ni suala la Kikatiba. Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 inatamka bayana aina ya Wabunge na sifa za kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano.Namshauri Mheshimiwa Mbunge kukubali wagombea wajiimarishe kuwania ushindi na siyo kulenga kuwa wawakilishi wa vyama Bungeni kwa kuwa washindi wateule watakuwa wamepatikana na kujaza nafasi zote kwa mujibu wa Katiba.

Wakuu hebu tuajdili haya majibu yanaridhisha kweli?hayajakaa kukuandamizi na kbaka demokarsia kweli?hivi je kweli Tanzania ni democratic country?mbona upinzani uanakandamizwa sana?

Mie nafikiri iwe hivi
Mgombea urais aruhusiwe kugombea ubunge kwa wakati mmoja.
 
Mimi sidhani wagombea uraisi wanaopata kura 3-5% kupewa ubunge ni kitu cha maana sana. Italeta tofauti gani? Kama mtu ana jijua kabisa hata shinda uraisi kwa nini asiende kugombea ubunge moja kwa moja?

"Namshauri Mheshimiwa Mbunge kukubali wagombea wajiimarishe kuwania ushindi na siyo kulenga kuwa wawakilishi wa vyama Bungeni..."

Waziri katoa jibu zuri sana. Wagombea uraisi wajiimarishe na kulenga ushindi. Sheria hiyo ikiwekwa basi kutakua na wagombea ambao wana jua kabisa hawata weza kushinda bali wana tafuta kujipatia ubunge. Be competitive, go for the gold not bronze.
 
Mie nafikiri iwe hivi
Mgombea urais aruhusiwe kugombea ubunge kwa wakati mmoja.

And the reason for that being....? Ita saidia nini haswa? Je hii itakua na manufaa kwa nchi au huyo mgombea mwenyewE?
 
Wakiwapa hili watu watataka kugombea urais ili wapate ubunge. Pathetic.
 
Mie nafikiri iwe hivi
Mgombea urais aruhusiwe kugombea ubunge kwa wakati mmoja.

Ndio hoja inayozungumziwa hapa.Kwamba Mgonbea Urais aruhusiwe kugombea na Ubunge pia na hasa akipata kura hizo alizopendekeza Mhonga Said(MB) kwenye swali lake
 
Mimi sidhani wagombea uraisi wanaopata kura 3-5% kupewa ubunge ni kitu cha maana sana. Italeta tofauti gani? Kama mtu ana jijua kabisa hata shinda uraisi kwa nini asiende kugombea ubunge moja kwa moja?

"Namshauri Mheshimiwa Mbunge kukubali wagombea wajiimarishe kuwania ushindi na siyo kulenga kuwa wawakilishi wa vyama Bungeni..."

Waziri katoa jibu zuri sana. Wagombea uraisi wajiimarishe na kulenga ushindi. Sheria hiyo ikiwekwa basi kutakua na wagombea ambao wana jua kabisa hawata weza kushinda bali wana tafuta kujipatia ubunge. Be competitive, go for the gold not bronze.

nafikiri cha maana hapa ni kwamba kama mtu kagombea urais na akapata asilimia tatu mpaka tano ya kura zote nchini basi mtu huyo ana ushawishi fulani kwa wananchi na kuna kitu wamekisikia wananchi mpaka wakampa asilimia hizo.sasa je kwa nini tumpoteze mtu huyu kwani mi nadhani ni sahihi kabisa kuwa kweli akiingia bungeni atakuwa na manufaa sana

ndugu yangu kama mtu kagombea urais na kapata asilimia tano mi nadhani he was right to aim for the gold,kwani mtu huyu asingekuwa na shida kupata kiti cha ubunge kama angegombea.lakini demokrasia sio kuangalia tu kuwa utashinda,kwani kama ingekuwa hivyo basi wapinzani bongo wasingethubutu kabisa kuingiza mguu kwenye kugombea urais,kwani CCM bado ngangali kwelikweli na sioni ikitoka karibuni.kikubwa ni kuimarisha mwamko wa siasa za kidemokrasia.jibu la waziri haliko sawa kabisa kwamba watu wajiimarishe katika kushinda urais na sio ku-aim kuwa wawakilishi bungeni.amesahau kuwa demokrasia ya kweli inaanzia bungeni.mi nadhani ni wazo zuri sana kuwa wagombea wa urais kulingana na percentage yake aweze kupewa kiti cha ubunge.anasema kuwa katiba imeeleza wazi jinsi ya upatikanaji wa wabunge...!tukumbuke kuwa katiba hiyohiyo haikuwa inasema chochote kuhusu wabunge wa viti maalum,sasa kwa nini hili nalo ambalo mi naliona lina mantiki sana lisifanyiwe marekebisho kikatiba.....!fikiria wangekuwapo wakina Mrema,Mtikila,Lipumba bungeni ni bunge la namna gani tungekuwa nalo...
 
Back
Top Bottom