Wagombea Urais Zanzibar wanapaswa kumlazimisha Bashiru awaambie nani kati yao ametumwa na "mabeberu" la sivyo akiri kauli yake ni potofu sana kisiasa

Wagombea Urais Zanzibar wanapaswa kumlazimisha Bashiru awaambie nani kati yao ametumwa na "mabeberu" la sivyo akiri kauli yake ni potofu sana kisiasa

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Mara nyingi nimesema sana humu JF kwamba kuna wakati nazishangaa sana kauli za wanasiasa wetu zinazotolewa kama vile hawana uwezo wa kufikiri. Sasa hili la Bashiru, Katibu Mkuu wa CCM kupiga kelele mbele ya jumuiya kwamba haelewi kwa nini hadi wakati huo wanachama 12 wajitokeze kugombea uraisi Zanzibar ni mojawapo ya kauli potofu sana kufanywa na kiongozi wa juu wa kisiasa kwa sababu zifuatazo;
  1. Kauli ya Bashiru inaashiria kuwa tayari CCM wana mtu wao ambae "ameshateuliwa" na huyo peke yake ndie anapaswa kuchukua form za uraisi wa Zanzibar
  2. Kauli ya Bashiru ni wonyesho wazi kwamba ndani ya CCM hawajali demokrasia wala kufuata katiba yao wenyewe, viongozi wa juu waliopo madarakani ndio wanaamua nani apewe uongozi wengine wote hawatasikilizwa
  3. Kauli ya Bashiru ina maana kwamba isipkuwa mtu mmoja, wengine wote waliochukua form za Uraisi Zanzibar wanatumiwa na "mabeberu" na CCM inajua hilo japo imewaacha waendelee kuwa katika nafasi zao katika chama
  4. Kwamba kama wewe sio mtu wa kundi la "CCM ya wenyewe" basi ndani ya CCM hata ufanyeje hutafanikiwa, na kugombea nafasi za uongozi ni kujipotezea muda
Mwisho napenda kutoa wito kwa viongozi wote wa Tanzania katika siasa na serikali, muwe mnatafakari kabla ya kutoa kauli za kuropoka kwa kuwa nyie ni kioo cha jamii. Kuna kauli mnazitoa kwa mihemuko tu ya kuhutumia umati wa watu lakini zinaweza kuwa na athari kubwa sana kwa nchi hii. Kauli ya Bashiru juu ya wagombea wa Uraisi wa Zanzibar ni mojawapo ya kauli za kitoto sana kutolewa na kiongozi wa juu wa kisiasa, na haingii akilini kwamba inaweza kutoka kwa kiongozi mwenye kiwango cha elimu cha Bashiru. NI kauli yeye kumdhalilisha kwa jamii.

Think before you talk.

 
Atakaye thubutu kuhoji tunamkata mapema?
 
Wahenga walisema LINALOJAMBA NI TUMBO, KULE KWINGINE NI SPIKA TU... Sasa msifikiri Bashiru ametoa kauli Ile yeye....
 
Nitashangaa sana kama hawa waliochukua form, au hata CCM Zanzibar kwa ujumla, watakaa kimya. Bashiru asiwapangie mambo yenu, raisi ni wa kwenu sio wa Bashiru
 
Mara nyingi nimesema sana humu JF kwamba kuna wakati nazishangaa sana kauli za wanasiasa wetu zinazotolewa kama vile hawana uwezo wa kufikiri. Sasa hili la Bashiru, Katibu Mkuu wa CCM kupiga kelele mbele ya jumuiya kwamba haelewi kwa nini hadi wakati huo wanachama 12 wajitokeze kugombea uraisi Zanzibar ni mojawapo ya kauli potofu sana kufanywa na kiongozi wa juu wa kisiasa kwa sababu zifuatazo;
  1. Kauli ya Bashiru inaashiria kuwa tayari CCM wana mtu wao ambae "ameshateuliwa" na huyo peke yake ndie anapaswa kuchukua form za uraisi wa Zanzibar
  2. Kauli ya Bashiru ni wonyesho wazi kwamba ndani ya CCM hawajali demokrasia wala kufuata katiba yao wenyewe, viongozi wa juu waliopo madarakani ndio wanaamua nani apewe uongozi wengine wote hawatasikilizwa
  3. Kauli ya Bashiru ina maana kwamba isipkuwa mtu mmoja, wengine wote waliochukua form za Uraisi Zanzibar wanatumiwa na "mabeberu" na CCM inajua hilo japo imewaacha waendelee kuwa katika nafasi zao katika chama
  4. Kwamba kama wewe sio mtu wa kundi la "CCM ya wenyewe" basi ndani ya CCM hata ufanyeje hutafanikiwa, na kugombea nafasi za uongozi ni kujipotezea muda
Mwisho napenda kutoa wito kwa viongozi wote wa Tanzania katika siasa na serikali, muwe mnatafakari kabla ya kutoa kauli za kuropoka kwa kuwa nyie ni kioo cha jamii. Kuna kauli mnazitoa kwa mihemuko tu ya kuhutumia umati wa watu lakini zinaweza kuwa na athari kubwa sana kwa nchi hii. Kauli ya Bashiru juu ya wagombea wa Uraisi wa Zanzibar ni mojawapo ya kauli za kitoto sana kutolewa na kiongozi wa juu wa kisiasa, na haingii akilini kwamba inaweza kutoka kwa kiongozi mwenye kiwango cha elimu cha Bashiru. NI kauli yeye kumdhalilisha kwa jamii.

Think before you talk.



Kinachokushangaza ni nini hasa wakati dunia yote inajua kuwa kwa mfano Maalim Seif ndiye aliyekuwa mgombea pekee wa Urais Zanzibar enzi zile za CUF na sasa ni kama hivyo ACT Wazalendo. Kwani wananchi wote ama wanachama wote wa vyama hivyo walipiga kura lini kumteua awe mgombe wa kudumu wa Urais Zanzibar??? Huko nako si kuidharirisha jamii?

Chama makini huwaandaa makada wa kushika nyadhifa mbalimbali, na si kwa kubahatisha, na maandalizi hayo huchukua muda na hufanywa kwa umakini mkubwa na uzingativu wa mambo mbalimbali kupitia mifumo ya chama husika.
 
Kinachokushangaza ni nini hasa wakati dunia yote inajua kuwa kwa mfano Maalim Seif ndiye aliyekuwa mgombea pekee wa Urais Zanzibar enzi zile za CUF na sasa ni kama hivyo ACT Wazalendo. Kwani wananchi wote ama wanachama wote wa vyama hivyo walipiga kura lini kumteua awe mgombe wa kudumu wa Urais Zanzibar??? Huko nako si kuidharirisha jamii?

Chama makini huwaandaa makada wa kushika nyadhifa mbalimbali, na si kwa kubahatisha, na maandalizi hayo huchukua muda na hufanywa kwa umakini mkubwa na uzingativu wa mambo mbalimbali kupitia mifumo ya chama husika.
Mkuu, mie sina ushabiki na CCM, lakini kila nikisiliza hii kauli ya Bashiru nashindwa kuelewa huyu mtu ana mawazo gani. Ni kama anasema kuna mtu mmoja tu alitakiwa kuchukua form. Sasa hao wengine wasiotakiwa watajuaje? Je waliambiwa? Mie nadhani angekuwa na busara sana kama angekaa kimya, hata kama wanajua kuna mtu wanaemtaka. Kwani vikao vya CCM si vitachuja watu, sasa kiherehere cha nini kukasirikia wengine wanaochukua form?
 
Mara nyingi nimesema sana humu JF kwamba kuna wakati nazishangaa sana kauli za wanasiasa wetu zinazotolewa kama vile hawana uwezo wa kufikiri. Sasa hili la Bashiru, Katibu Mkuu wa CCM kupiga kelele mbele ya jumuiya kwamba haelewi kwa nini hadi wakati huo wanachama 12 wajitokeze kugombea uraisi Zanzibar ni mojawapo ya kauli potofu sana kufanywa na kiongozi wa juu wa kisiasa kwa sababu zifuatazo;
  1. Kauli ya Bashiru inaashiria kuwa tayari CCM wana mtu wao ambae "ameshateuliwa" na huyo peke yake ndie anapaswa kuchukua form za uraisi wa Zanzibar
  2. Kauli ya Bashiru ni wonyesho wazi kwamba ndani ya CCM hawajali demokrasia wala kufuata katiba yao wenyewe, viongozi wa juu waliopo madarakani ndio wanaamua nani apewe uongozi wengine wote hawatasikilizwa
  3. Kauli ya Bashiru ina maana kwamba isipkuwa mtu mmoja, wengine wote waliochukua form za Uraisi Zanzibar wanatumiwa na "mabeberu" na CCM inajua hilo japo imewaacha waendelee kuwa katika nafasi zao katika chama
  4. Kwamba kama wewe sio mtu wa kundi la "CCM ya wenyewe" basi ndani ya CCM hata ufanyeje hutafanikiwa, na kugombea nafasi za uongozi ni kujipotezea muda
Mwisho napenda kutoa wito kwa viongozi wote wa Tanzania katika siasa na serikali, muwe mnatafakari kabla ya kutoa kauli za kuropoka kwa kuwa nyie ni kioo cha jamii. Kuna kauli mnazitoa kwa mihemuko tu ya kuhutumia umati wa watu lakini zinaweza kuwa na athari kubwa sana kwa nchi hii. Kauli ya Bashiru juu ya wagombea wa Uraisi wa Zanzibar ni mojawapo ya kauli za kitoto sana kutolewa na kiongozi wa juu wa kisiasa, na haingii akilini kwamba inaweza kutoka kwa kiongozi mwenye kiwango cha elimu cha Bashiru. NI kauli yeye kumdhalilisha kwa jamii.

Think before you talk.


Beberu wa siku hizi unamjua? Anatoka chattle!
 
Back
Top Bottom