Wagonjwa 6,847 Watibiwa Hospitali ya Wilaya ya Handeni

Wagonjwa 6,847 Watibiwa Hospitali ya Wilaya ya Handeni

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WAGONJWA 6,847 WATIBIWA HOSPITALI YA WILAYA HANDENI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema wagonjwa wapatao 6,846 wamepata huduma za Afya Katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni tangu ilipokamilika na kuanza kutoa huduma.

Waziri Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Hospitali hiyo iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Tanga.

Amesema ujenzi wa hospitali hiyo umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 7.3 ambapo Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 4.3 na wadau wa Islamic Help wametoa kiasi cha shilingi Bilioni 3.

Amesem mpaka sasa jumla ya majengo yaliyokamilika ni 15 amesema Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga hadi sasa imeshapokea wajawazito 900 na kati yao 300 walijifungua kwa njia ya upasuaji ndani ya miaka mitatu(3).

Rais Samia amefanya uzinduzi wa hospitali hiyo akiwa katika ziara mkoani Tanga ambayo ameanza leo Februari 23, 2025 hadi Machi 1, 2025 kwa lengo la kukagua na kuzindua miradi mbaliambali iliyotolewa fedha na Serikali.
 

Attachments

  • Gkfrgi2XMAAjMWl.jpg
    Gkfrgi2XMAAjMWl.jpg
    469.5 KB · Views: 1
  • Gkfrgi0X0AEeyt1.jpg
    Gkfrgi0X0AEeyt1.jpg
    521.3 KB · Views: 2
  • GkfrgiyWYAACc-D.jpg
    GkfrgiyWYAACc-D.jpg
    478.7 KB · Views: 1
  • Gkfrgi7WcAAtEXf.jpg
    Gkfrgi7WcAAtEXf.jpg
    430.4 KB · Views: 1
Back
Top Bottom