Wagonjwa wanateseka hospitali ya Temeke

Wagonjwa wanateseka hospitali ya Temeke

MwakiIV

Member
Joined
Aug 31, 2018
Posts
79
Reaction score
138
IMG_4233.jpg

IMG_4234.jpg

Siku ya leo 17/03/2023

Kuna ajali imetokea asubuhi ya leo ambayo imesababisha majeruhi wawili, majeruhi hao walipata huduma ya kwanza kwenye Zahanati ya Kigamboni na baadae tupewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Temeke.

Baada ya kupokelewa ukawa na changamoto ya Umeme ambapo hata Jenereta lililopo hapa limeshindwa kuwaka hivyo kupelekea huduma kusimama kwa zaidi ya masaa 3.

Wagonjwa waliendelea kuja kwa wingi, lakini mfumo wa hospitali haukuwa unafanya kazi kuanzia kwenyeusajili, malipo, vipimo na matibabu.

Hivyo waudumu na madaktari ni kama walikuwa wanazurura tu.

SWALI:
1. Kitu kinachoitwa mfumo ni suala la upeo wa binadamu kwa nini hakuna njia mbadala ya mfumo endapo digitali ikafeli?

2. Hadhi ya hii hospitali inakosaje jenereta la kuwezesha huduma zikaendelea?
 
Ni aibu kubwa sana kwakweli kwa Hospital kubwa kama hiyo, wanasababisha watu kwenda kuzikwa kwa uzembe tu.
 
Swali kuu lingekuwa "Kwa nini Hospitali ya Rufaa ikatiwe umeme?"
 
Wale watoto wanaozaliwa premature wanawekwa kwenye mashine inakuaje?
Walio ICU?
Kama kweli hii inatisha sana
 
Kuwakatia umeme nayo ni shida, labda iwe kwa muda mfupi tu ambao nao wanapaswa kuwa na standby generator. Hizi huduma za wananchi ndo za kuwekeza pesa nyingi badala ya kuendelea kununua magari ya kifahari ma VXR ya viongozi...
 
Swali kuu lingekuwa "Kwa nini Hospitali ya Rufaa ikatiwe umeme?"
Kukatiwa umeme ni swala moja ambalo jibu lake ni mtambuka kidogo as wanaweza Sema ni swala liko nje ya uwezo wao ila ishu ya hospitali ya rufaa kukosa standby generator ni kitu kuanzia mkuu wa mkoa hadi waziri wa Afya Wana la kujibu. Huu ni uzembe Sana na nakuhakikishia watu wote ambao wako responsible na hiyo hospitali kuwa na hilo generator wao na jamaa zao hawatibiwi hapo wanatibiwa London clinic, Sali, Aga Khan na Hindu Mandal ambako hayo ma standby generators yapo.

Ni dhambi Sana kwa Mungu
 
Back
Top Bottom