Wahamiaji haramu wote wasakwe nchi nzima.tusiishie kwa Wanyarwanda tu na wengine wote waondoke

ambagae

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2009
Posts
3,334
Reaction score
1,385
Zoezi la kuwaondoa wahamiaji haramu wa kutoka Rwanda likimalizika ni vyema na wahamiaji haramu kutoka nchi zingine nao wakasakwa na kutakiwa kuondoka. Zoezi lisiishie kwa hao tu. watanzania tunajuana nani Mzaramo na nani Msukuma au Mgogo
 
Kwa usalama wetu na nchi yetu ni bora zoezi hili liwe endelevu. Muhimu tusiwaachie watu wa uhamiaji, polisi na usalama wa taifa bali sote wananchi tushirikiane na vyombo hivi kwani wahamiaji haramu hawaishi mbinguni bali tumewapangisha kwenye nyumba zetu wenyewe
 
kwani alikuwaambia ni wanyaruanda tuuuuuuuuu
 
Wahamiaji haramu wengine ni viongozi ndani ya serikali,wengine ndani ya vyama vya siasa ni pagumu hapo.
 
Zoezi la kuwaondoa wahamiaji haramu wa kutoka Rwanda likimalizika ni vyema na wahamiaji haramu kutoka nchi zingine nao wakasakwa na kutakiwa kuondoka. Zoezi lisiishie kwa hao tu. watanzania tunajuana nani Mzaramo na nani Msukuma au Mgogo

Kuna Wakenya hapa wamekuja kumiliki ardhi huko kwao ardhi inamilikiwa na matajiri, cha ajabu wakifika hapa wanarefusha midomo kujifanya ujuaji. hawa waondoke. juzi hao hao wakenya wameuua dereva taxi hapo gymkhana, wakati wanajaribu kuuficha mwili wake bahati nzuri Polisi wakawaona wakiuburuza mwili tayari kuutelekeza hapo wakanaswa. Hakika sasa ni wakati wa kuwaondoa hawa manyang'au waende kwao.
 
mi naona Wakenya wangerudishwa kwao kama wanyarwanda kwanza wamejaa kwenye shule za watu binafsi pitia shule zote za english medium hapa jijini wengi wao ni wakenya i think its now for kenyans to go back to their origin.
 
wamalawi kibao huku mikoa ya mbeya na wilaya zake ili kama ni msimamo wahamiaji wote kaskazni mpaka kusini na mashariki mpaka magharibi msako hatuwataki:
itifaki izingatiwe
 
Nani kakudanganya kwamba zoezi la kuwaondosha wahamiaji haramu linahusu wanyarwanda peke yao?,pia tumia muda kidogo kujifunza kuhusu masuala ya uraia.Inaonyesha uelewa wako ni mdogo sana kuhusu citizenship na jinsi uraia wa nchi unavyopatikana na aina zake.Suala la kabila la mtu linaweza lisiwe na uhusiano na uraia wake mfano kuna wasukuma,wagogo na wazaramo ambao si raia wa TZ baada ya kuukana uraia wa Tanzania,wakirejea nchini na kuishi bila kufuata utaratibu wanakuwa wahamiaji haramu.Mfano mwingine ni kwamba kuna watu walikuwa raia wa nchi nyingine lakini baada ya kuishi TZ kwa kipindi fulani na kutimiza masharti mengine muhimu waliamua kuomba uraia wa TZ,moja ya masharti ni kuukana uraia wa nchi zao kwani hapa TZ hakuna uraia wa nchi mbili,hata hivyo watu hawa hawayakani makabila yao wanabaki kuwa wahutu,watusi,waasia,nk raia wa TZ.
 
mi naona Wakenya wangerudishwa kwao kama wanyarwanda kwanza wamejaa kwenye shule za watu binafsi pitia shule zote za english medium hapa jijini wengi wao ni wakenya i think its now for kenyans to go back to their origin.
wakenya ni wengi sana, wamekuja tz wameoa watz na kujimilikisha ardhi. Wapo Mwanza, Arusha na Dar es salaam kwa wingi. Wasakwe kwani muda wa kuondoka wenyewe walishapewa. Wanaziba fursa za ajira. Tanzania ni ya watanzania
 
Hadi sasa (leo tarehe 15.09.2013) wahamiaji haramu 24,000 wamerudishwa makwao katika nchi za DRC, Rwanda, Burundi na Zambia (Source: Habari Maelezo).
 
Zoezi la kuwaondoa wahamiaji haramu wa kutoka Rwanda likimalizika ni vyema na wahamiaji haramu kutoka nchi zingine nao wakasakwa na kutakiwa kuondoka. Zoezi lisiishie kwa hao tu. watanzania tunajuana nani Mzaramo na nani Msukuma au Mgogo

Kwanza shule yenu ndogo wakenya kibao wamechukua kazi mahotel kwenye vyombo vya habari na sehemu nyingi tu furahia wewe mwenye elimu ya chini utapata nafasi ya kufanya kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…