Wahariri wahoji ongezeko la kodi kugharamia miradi isiyo na tija

Wahariri wahoji ongezeko la kodi kugharamia miradi isiyo na tija

Naipendatz

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2011
Posts
5,096
Reaction score
8,234
Dar es Salaam. Baadhi ya wahariri wanaounda Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) wamehoji mpango wa Serikali kuendelea kugharamia miradi waliyodai haina tija kwa kuongeza kodi na tozo kwenye bajeti ya Serikali.

Wakizungumza leo Jumamosi Juni 19, 2021 katika mjadala wa uchambuzi wa bajeti ya Serikali ulioongozwa na makamu mwenyekiti wa TEF, Bakari Machumu, wahariri hao wametaja ujenzi wa daraja la Tanzanite na uwanja wa ndege wa Geita-Chato wakisema haina tija kwa Taifa.

“Kuna miradi haina tija, kwa mfano daraja la Tanzanite. Wakati linajengwa walisema ni kwa ajili ya kupunguza msongamano kwa jiji la Dar es Salaam, lakini tukiangalia watu wengi wa Masaki wameshahamia Dodoma, labda kama tunataka kulitumia kupigia picha za harusi,” amesema Joseph Kulangwa ambaye ni mhariri wa gazeti la Raia Mwema.

“Kuna uwanja wa ndege wa Geita, nikashindwa kuelewa kuwa ni wa Geita au ni wa Chato? Wanasema umekamilika kwa asilimia 95 na unahitaji fedha zaidi kuukamilisha, sasa najiuliza tija ya huu uwanja ni nini?”

Maoni hayo yameungwa mkono na Abdallah Majura akisema daraja la Tanzanite lingejengwa eneo la Dumila mkoani Morogoro ambako hujaa mafuriko wakati wa mvua.

“Nilitegemea daraja kama lile la Dumila ambapo hutokea foleni kubwa wakati wa mafuriko tunakwenda kuzungukia Kilosa. Sasa unakuja kuwakamua wananchi kwa ajili ya daraja la Tanzanite ambalo nikiangalia Masaki hakuna foleni kubwa kiasi hicho,” amesema.

Majura amegusia mafuriko katika eneo la Jangwani jijini Dar es Salaam akisema manufaa ya fedha za wananchi yangeonekana.

“Ni mara 100 wangejenga lile daraja la juu kutoka Magomeni Mapipa mpaka Fire. Kwa hiyo Mtanzania akikamuliwa ajue ni kwa ajili ya maendeleo,” amesema Majura.

Kwa upande wake Imma Mbuguni ambaye ni mhariri wa Majira amesema bajeti hiyo haijaeleza jinsi itakavyoikwamua sekta binafsi ili kuongeza uzalishaji na kukuza kipato.

“Ili Serikali ikusanye mapato inabidi sekta binafsi iwe vizuri. Ukiangalia sekta binafsi imeathirika. Kwa mfano vyombo vya habari ambavyo havipati mapato, utaona ajira zitapungua. Bila sekta binafsi hatuwezi kukuza uchumi,” amesema.

Akizungumzia ongezeko la kodi, mhariri Charles Misango ameitaka Serikali kuweka ukomo wa makusanyo ya tozo kama za simu na kuweka malengo ya matumizi yake.

“Baada ya vita ya Tanzania na Uganda, Mwalimu (Julius) Nyerere alitangaza miezi 18 ya kufunga mikanda. Hii pia tungweka muda, kwamba hii kodi lengo ni kukusanya shilingi ngapi. Hata barabara zitakazojengwa tujue zimejengwa vipi,” amesema.

Kuhusu punguzo la faini ya bodaboda kutoka Sh30,000 hadi 10,000, Misango amesema haina faida yoyote.

“Sioni mantiki ya kupunguza faini ya bodaboda. Ningeshauri iongezeke tena ifike hata Sh50,000 kwa sababu bodaboda ni kama wana nchi yao, wana utawala wao na hawana makosa. Ikitokea wamesababisha ajali wanaweza kuchoma hata gari lako. Kwa sababu wataona Sh10,000 ni kitu gani?” amehoji.

Awali wakichokoza mada katika mjadala huo, wataalamu wa uchumi wameipongeza bajeti hiyo na kukosoa katika baadhi ya maeneo.

“Kwanza niipongeze sana hii bajeti kwa sababu ni bajeti ya matumaini na inakwenda kumgusa kila mwananchi. Inatusogeza kufanya biashara kwenye uchumi wa kati,” amesema Lawrence Mlaki ambaye mchambuzi wa masualoa ya uchumi na fedha.

Naye mkufunzi wa udhibiti wa fedha binafsi, Edmund Munyagi amesema hatua ya Serikali kuongeza kodi na tozo itapunguza walipa kodi.

Chanzo: Mwananchi
 
Hao TEF waache kuhojihoji kwanza chama Chao TEF si chama cha haki na wala si chama cha Wahariri Tanzania kwa sababu hakiwakilishi Wahariri wote kutoka vyombo vyote Tanzania ni kakikundi tu ka editors hasa wa Print media ndio walaji humo.

Uanachama wa TEF the so called eti "Jukwaa la Wahariri" wa Tanzania. Are you sure linawakilisha vyombo vyote vya habari Tanzania!?

Nadiriki kusema hako ni kakikundi ka waandishi wa Habari wachache akina Neville Meena na wenzake hasa kutoka 'print media' ambao wamejikusanya ili kupiga fedha huku chama Chao tangu kuasisiwa kwake kikikosa uwakilishi wa Wahariri wote wa Tanzania.

Hivyo basi,TEF sio Jukwaa la Wahariri Tanzania. Ni chama cha wahariri mikoa ya Dar na Dodoma.

Nchi hii media hazipo Dar na Dodoma tu.

Badala yake waliite Jukwaa la Wahariri Dar es salaam na Dodoma maana ndiko members wa hicho chama cha kimkoa wanakotoka.

Msijifanye wasaafii sana rekebisheni kwanza hicho chama chenu kiwe inclusive kiwajumuishe editors wote wa Tanzania kutokea media za Tunduru, Katavi, Mbulu, mpaka Mtwara na kote nchini.

Waandishi wa Habari hii Tanzania ni wabinafsi sana ndio maana hata MCT iliyopo imefeli that's why serikali itawaundia independent MCT. Mnaboa mnaojiita eti TEF.
 
Vyombo vya habari na wahariri,mmefanya vizuri Leo.
Tanzanite bridge tayari asilimia 80 tulishachemka.
Pazeni sauti uwanja wa MSALATO kwasasa sioni tija,nikweli makao makuu.Tuna uwanja tayari uliopanuliwa na unatumika,SGR inaendelea
Ulazima wakuwa na kipaumbele wa Msalato nikuumizana tu.Jiji maji ni shida hatuna kipaumbele.
Vyombo vya habari nitegemeo
Binge ni kelele na kudemka tu
 
Nimemsikia kijana anaitwa Mlaki, nadhani ni mtoto wa Mhe. Rita Mlaki
  • Amelezea uwanja wa Chato ukitumika vizuri mfano kusafirisha madini, samaki nk
  • Nimeona sijui ni nani ameelezea madaraja yana muda fulani wa ukomo ambapo unatakiwa kufanye reinforcement au kujenga jipya kama wanavyofanya sasa China, Marekani nk
  • Daraja la Salender lilijengwa lini? Je! Muda wake umeisha au la? Je! Siku lingebomoka au kupata shida ingekuwaje?
  • Kuhusu Dumila na Jangwani ni muhimu sanaaaaaaaa!!!

Queen Esther
 
wahariri hao wametaja ujenzi wa daraja la Tanzanite na uwanja wa ndege wa Geita-Chato wakisema haina tija kwa Taifa.
Pamoja na daraja la Busisi litakalotumiwa na wanaKIJIJI 300 halafu eti tupoteze mabilioni ya shilingi hapo
 
Hii ni sawasawa na mtu kutumia risasi ya kuulia tembo kwenda kuwindia ndege...
 
Hao TEF waache kuhojihoji kwanza chama Chao TEF si chama cha haki na wala si chama cha Wahariri Tanzania kwa sababu hakiwakilishi Wahariri wote kutoka vyombo vyote Tanzania ni kakikundi tu ka editors hasa wa Print media ndio walaji humo.

Uanachama wa TEF the so called eti "Jukwaa la Wahariri" wa Tanzania. Are you sure linawakilisha vyombo vyote vya habari Tanzania!?

Nadiriki kusema hako ni kakikundi ka waandishi wa Habari wachache akina Neville Meena na wenzake hasa kutoka 'print media' ambao wamejikusanya ili kupiga fedha huku chama Chao tangu kuasisiwa kwake kikikosa uwakilishi wa Wahariri wote wa Tanzania.

Hivyo basi,TEF sio Jukwaa la Wahariri Tanzania. Ni chama cha wahariri mikoa ya Dar na Dodoma.

Nchi hii media hazipo Dar na Dodoma tu.

Badala yake waliite Jukwaa la Wahariri Dar es salaam na Dodoma maana ndiko members wa hicho chama cha kimkoa wanakotoka.

Msijifanye wasaafii sana rekebisheni kwanza hicho chama chenu kiwe inclusive kiwajumuishe editors wote wa Tanzania kutokea media za Tunduru, Katavi, Mbulu, mpaka Mtwara na kote nchini.

Waandishi wa Habari hii Tanzania ni wabinafsi sana ndio maana hata MCT iliyopo imefeli that's why serikali itawaundia independent MCT. Mnaboa mnaojiita eti TEF.

Mkuu anzisha chama chako cha waandishi wa habari wa nchi nzima, kisha wafanye utakavyo. Ila kwa sasa acha hawa walioanzisha cha kwao wahoji mambo ya msingi.
 
Mkuu anzisha chama chako cha waandishi wa habari wa nchi nzima, kisha wafanye utakavyo. Ila kwa sasa acha hawa walioanzisha cha kwao wahoji mambo ya msingi.
Bado ukweli unabaki kuwa hilo sio jukwaa la kitaifa la editors injinia nianzishe chama cha mahkl kivipi jibu hoja acha hisia
 
Bado ukweli unabaki kuwa hilo sio jukwaa la kitaifa la editors injinia nianzishe chama cha mahkl kivipi jibu hoja acha hisia

Punguza utoto dogo, engineer unajichanganya na siasa majitaka, au nyie ndio wale maengineer mnaojenga majengo ndani ya mwaka yamejaa nyufa?
 
Punguza utoto dogo, engineer unajichanganya na siasa majitaka, au nyie ndio wale maengineer mnaojenga majengo ndani ya mwaka yamejaa nyufa?
Kujibizana na popoma ni kibarua acha ninyamaze
 
Pamoja na daraja la Busisi litakalotumiwa na wanaKIJIJI 300 halafu eti tupoteze mabilioni ya shilingi hapo
Acha kuwaza ujinga mkuu, nisamehe bure 300 unamaanisha nini? Kama ferry zote zinakesha kwahiyo wanaobebwa ni 300 tu.
Mwanza ni jiji la pili TZ. Acha dharau kabisa.
 
Pamoja na daraja la Busisi litakalotumiwa na wanaKIJIJI 300 halafu eti tupoteze mabilioni ya shilingi hapo
si kweli busisi ni njia inayotumiwa sana na hata nchi jirani licha ya kuunganisha wilaya ya sengema ,Geita na mkoa mwanza
 
Back
Top Bottom