Wahaya wote inawahusu!!!

JERUSALEM 2006

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
527
Reaction score
596
Wasalaam wana Jamvi.Kama wewe ni muhaya au ulizaliwa katika mkoa wa Kagera au una ndugu yako aliyefanikiwa kujiunga na chuo kikuu mwaka 2012/13 basi hii inakuhusu.Binafsi nimeona ni busara kuwakutanisha wahaya wote tulioko vyuoni na tuliochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu au taasisi za elimu ya juu,ili.:1.Tuweze kupanga mikakati ya kuendeleza wenzetu(wahaya) walioko chini yetu.2. Tuweze kupanga mikakati ya kuendeleza na kuwasaidia wahaya wenzetu kielimu walioko vijijini na waweze kuwa kama sisi.3. UPDATES:Napenda kutoa taarifa ya hatua tulizo zifikia katika uhamasishaji. Mwaka jana September nilileta mada ya uhamasishaji wa wahaya waliopo vyuoni kuungana na kuweka mikakati ya kuendeleza wenzao walioko vijijini. Nilipata majibu mbalimbali, yakiwa ni yakutia moyo lakini pia ya kukatisha tamaa. Wengi walio nijibu hovyo hawakunielewa nia yangu, ila walinishutumu kuwa mimi ni mkabila.Lahasha mimi sio mkabila, ila sina uwezo wakuhamasisha vikundi vyote katika nchi hii. Nilichagua kuhamasisha watu wa nyumbani(WAHAYA) na mchakato umeenda vizuri sana, kwani nimepewa ushirikiano mkubwa sana hapa chuoni.(UDSM).Napenda kutoa shukrani za dhati kwa wahaya wote walio onesha ushirikiano na kunipa nguvu ki hali na mali. Hakika umoja ni nguvu.Mpaka sasa tumesha unda vikundi kazi vy uhamasishaji, na lengo kuu ni kwamba tunataka ifikapo 2020, angalau kila kaya iwe na kichwa kimoja chenye elimu ya chuo kikuu.Pia malengo mapya ni kuendeleza mkoa wetu wa Kagera na tuna malengo ya kufanya mji wa Bukoba kuwa jiji ndani ya miaka michache ijayo. Hii itatokana na sisi wana chuo kuwekeza zaidi kwetu pindi tunapomaliza elimu yetu ya juu.Kuna minong'ono inayoendelea mitaani kuwa rais wa nchi hii haawezi kuwa Muhaya. Basi sisi kama wana Kagera tunataka kuwaondolea mawazo hayo watanzania hasa kizazi cha sasa. Hata ikitokea tukapata mgombea urais kutoka Kagera basi ukabila isiwe kikwazo.Tuna panga kufanya mkutano mkuu mwishoni mwa semister hii hapa chuoni ili kuona ni vipi tunaweza kufanikisha mipango yetu.Nitaendelea kuwapa taarifa kwa yale yote tutakayo afikiana.NATOA WITO KWA MAKABILA MENGINE KUIGA MFANO HUU, KWANI NI NJIA RAHISI KUFIKIA MAENDELEO.
 
MKUU WA KAYA(MUHAYA) AKITOA MAELEKEZO KWA DADA WA KAZI KABLA YA KUONDOKA NYUMBANI ASUBUHI:

Mimi natoka watu wa sensa wakiulizia nimeenda wapi waambieni nimeenda bank kuchukua milioni thelathini kwa ajili ya ada za kaka zenu wawili wanaosoma PHD uingereza, wakiuliza jumla mu wangapi waambieni tuko nane, ila Bibi mzaa Baba ameenda India kutibiwa na yupo huko mwezi sasa, na imetucost mpaka dakika hii milioni sabini, mama yenu muwaambie yupo site, anasimamia ushushwaji wa vifaa vya ujenzi 'kwa ajili ya finishing' vimetoka China ambavyo vimetugharimu milioni 600, halafu na watoto wengine waliobaki waambieni wameenda kutembea serengeti na rafiki zao wametoka Australia, na wanatumia gari mbili Range Rover na Hummer, kama watahitaji kuongea namimi wapeni namba zangu za Blackberry tu, zile Samsung Galax waambieni huwa natumia kwa family Issues tu ...
 
ukabila nyerere alikataza , huoni hata aibu kuongea mambo ya ukabila mwaka huu wa 2012????!!! mimi nadhani ni ushamba tu unakusumbua na mawenge ya kuchaguliwa chuo kikuu , ndo unaanza kujidai eti unataka kuendeleza wenzako.. kama kweli una dhamira ya kweli , fanya mipango ya kuiendeleza tanzania nzima na sio hao wahaya wenzako........ ni hayo tu kaka , , , na sijui hicho chuo umechaguliwa chuo gani kinachokupa mawenge namna hiyo....
 

Asante kwa ushauri wako. Hapa sijaonesha ukabila wowote, linapokuja suala la kijamii kama hili lazimi tuwajibike kwa nafsi zetu.
Nimechaguliwa Bsc. Electrical Engineering, UDSM.
 
Kijana mawazo yako ni mazuri sana kosa tu umekimbilia nyumbani. Baada ya kuona umuhimu wa elimu ya juu ungewaambia watanzania wote kuwa kila kijiji kiwe na wahitimu 20 wa shahada ya kwanza mwaka 2020 halafu utupe mkakati wa kufikia hayo malengo hapo ningekupa heko!
 
Asante kwa ushauri wako. Hapa sijaonesha ukabila wowote, linapokuja suala la kijamii kama hili lazimi tuwajibike kwa nafsi zetu.
Nimechaguliwa Bsc. Electrical Engineering, UDSM.

Ndo yale yale waambie nimeenda kuchukua milioni 30 ha ha ha !! Wahaya bana si ungesma 2 umechaguliwa UDSM mpaka utwambie Bsc aseeeeh!!!
 
Asante kwa ushauri wako. Hapa sijaonesha ukabila wowote, linapokuja suala la kijamii kama hili lazimi tuwajibike kwa nafsi zetu.
Nimechaguliwa Bsc. Electrical Engineering, UDSM.
Hata mimi nipo UDSM , ni sehemu ya kawaida sana chalii wangu.. ningekuomba hata unibebe wewe ila inaonyesha wewe ni mkabila tu , na istoshe nyie wahaya nawafahamu nyie... tabia zenu sio mchezo.. na pale chuo ndo mnajaza kile chuo... anyway lakini HONGERA sana.. na nakupa heshima yako maana unakuja UDSM-COET ,,,,, bila hivyo ningekuona mshamba...... CONGRATS once again....
 
Ndo yale yale waambie nimeenda kuchukua milioni 30 ha ha ha !! Wahaya bana si ungesma 2 umechaguliwa UDSM mpaka utwambie Bsc aseeeeh!!!

inaonyesha huyu jamaa ni mtu wa kujidai sana ndo maana hata kubebwa na mtu kama huyu sitaki , wala hata kufahamiana nae , sijui anadhani watu wengine wanasomea nini!!!! na istoshe hiyo degree program yake anayoebda kuisomea ni ya kawaida sana pale COET ,,,, atuulize sisi kaka zake ,,, bora tu angekaa kimya
 

kwa upande wangu nasoma agricultural engineering sua, pamoja sana mkuu.
 
Ukabila hivi bado upo?

ukabila bado upo ,, na hawa wahaya ndo wenyewe.... pale mlimani wamejazana kama uchafu ,,, kila depertment imejaa wahaya ,,,,, sehemu ambayo wameshindwa kupenya ni UDBS tu peke yake....
 
kwa upande wangu nasoma agricultural engineering sua, pamoja sana mkuu.

mshamba tu na wewe , huna lolote... na nyie majamaa mnapendaga sana kujionyesha na kuwa na maringo na kujitangazia tangazia,,,.... sijui hata mna shida gani , kweli jiungeni angalau mmfanye mpango wa kubadilishana
 
mshamba tu na wewe , huna lolote... na nyie majamaa mnapendaga sana kujionyesha na kuwa na maringo na kujitangazia tangazia,,,.... sijui hata mna shida gani , kweli jiungeni angalau mmfanye mpango wa kubadilishana

mshamba ww na familia yako, pumb....., zako, huna jipya wivu tu umekujaa, umeambiwa kila muhaya yuko hivyo hivi wewe umelazimishwa kuchangia lolote, wee soma kama halikuhusu kula kona, mwehu mkubwa.
 

Eti eeh? Thought you could do better than this!
Electrical Engineering is currently the best field in construction and technology industries. Kwani wewe ulitaka nikasome nini ili uone ni field ya maana?
Every where needs electricity and else where reforms with electronics.
Think big. Think to create jobs and not beg for them.
"WAHAYA ELIMU KWANZA"
 
its not amatter of fighting, arguing, prouding, seggregation, discrimination, regionalism, tribalism but it is one for all and all for one.
 
Mbona wachaga hatuongei wakati tuna elimu tuna hela tofauti na nyie wahaya masifa tu yani mhaya yupo tayari awe bosi alipwe elfu 20 lakini mchaga atakuwa mlinzi lakini alipwe milioni
 
Wazo kama hili lilipaswa kutolewa mwaka 1200 lakini siyo 2012. Hata hivyo ni wazo hata kama lina walakini maana kuwaza na kuwazua ni haki ya mtu. Nimefurahi kuona watu bado wana mawazo yanayokwenda nyuma badala ya kwenda mbele. Endleeni hivyo ila wenzenu wanawaacha kwa mbali sana jamani.
 
Asante kwa ushauri wako. Hapa sijaonesha ukabila wowote, linapokuja suala la kijamii kama hili lazimi tuwajibike kwa nafsi zetu.
Nimechaguliwa Bsc. Electrical Engineering, UDSM.
kumbe ndo kiform one unaanza chuo sasaivi, ndo maana akili ya ukabila haijakutoka bado umetoka nayo uhayani...kwa kifupi ni muhimu kama utaweka kikao hicho, ili mfundishane kukata magovii msije nayo hapa dsm, huku sisi wenzenu huwa tunakata mikono ya sweta. kifupi, ile miaka ya kuamini kuwa wahaya ndio wasomi wengi imepita, siku hizi hata wasukuma wasomi wengi mno, hadi masai...acha ukabila hautakufikisha popote zaidi ya kuumia moyo.
 

endelea kuwa mpayukaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…