JERUSALEM 2006
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 527
- 596
Wasalaam wana Jamvi.Kama wewe ni muhaya au ulizaliwa katika mkoa wa Kagera au una ndugu yako aliyefanikiwa kujiunga na chuo kikuu mwaka 2012/13 basi hii inakuhusu.Binafsi nimeona ni busara kuwakutanisha wahaya wote tulioko vyuoni na tuliochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu au taasisi za elimu ya juu,ili.:1.Tuweze kupanga mikakati ya kuendeleza wenzetu(wahaya) walioko chini yetu.2. Tuweze kupanga mikakati ya kuendeleza na kuwasaidia wahaya wenzetu kielimu walioko vijijini na waweze kuwa kama sisi.3. UPDATES:Napenda kutoa taarifa ya hatua tulizo zifikia katika uhamasishaji. Mwaka jana September nilileta mada ya uhamasishaji wa wahaya waliopo vyuoni kuungana na kuweka mikakati ya kuendeleza wenzao walioko vijijini. Nilipata majibu mbalimbali, yakiwa ni yakutia moyo lakini pia ya kukatisha tamaa. Wengi walio nijibu hovyo hawakunielewa nia yangu, ila walinishutumu kuwa mimi ni mkabila.Lahasha mimi sio mkabila, ila sina uwezo wakuhamasisha vikundi vyote katika nchi hii. Nilichagua kuhamasisha watu wa nyumbani(WAHAYA) na mchakato umeenda vizuri sana, kwani nimepewa ushirikiano mkubwa sana hapa chuoni.(UDSM).Napenda kutoa shukrani za dhati kwa wahaya wote walio onesha ushirikiano na kunipa nguvu ki hali na mali. Hakika umoja ni nguvu.Mpaka sasa tumesha unda vikundi kazi vy uhamasishaji, na lengo kuu ni kwamba tunataka ifikapo 2020, angalau kila kaya iwe na kichwa kimoja chenye elimu ya chuo kikuu.Pia malengo mapya ni kuendeleza mkoa wetu wa Kagera na tuna malengo ya kufanya mji wa Bukoba kuwa jiji ndani ya miaka michache ijayo. Hii itatokana na sisi wana chuo kuwekeza zaidi kwetu pindi tunapomaliza elimu yetu ya juu.Kuna minong'ono inayoendelea mitaani kuwa rais wa nchi hii haawezi kuwa Muhaya. Basi sisi kama wana Kagera tunataka kuwaondolea mawazo hayo watanzania hasa kizazi cha sasa. Hata ikitokea tukapata mgombea urais kutoka Kagera basi ukabila isiwe kikwazo.Tuna panga kufanya mkutano mkuu mwishoni mwa semister hii hapa chuoni ili kuona ni vipi tunaweza kufanikisha mipango yetu.Nitaendelea kuwapa taarifa kwa yale yote tutakayo afikiana.NATOA WITO KWA MAKABILA MENGINE KUIGA MFANO HUU, KWANI NI NJIA RAHISI KUFIKIA MAENDELEO.