Wahitimu wa vyuo wanajitolea Serikalini na mashirika yake wapewe kipaumbele ajira

Wahitimu wa vyuo wanajitolea Serikalini na mashirika yake wapewe kipaumbele ajira

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Kuna vijana wahitimu wa vyuo vikuu wengi wameajiriwa kwa mikataba ya kujitolea serikali za mitaa serikali kuu na mashirika ya umma.

Hakika inauma sana unapoona mtu amesota miaka miwili halafu nafasi imetoka anaomba halafu anapewa mtu mpya hajatoa jasho lolote kujitolea.

Kwa vyovyote yafaa mwenye kujitole na uzoefu wake kupewa uzito wa alama kwenye usaili au aliyejitolea uwepo utaratibu wa tofauti ili nafasi zikitoka aweze kuajiriwa.

Vinginevyo kwa hakika serikali kama watu binafsi haiwezi kuepa lawama ya kuonekana inashiriki kunyonya nguvu kazi ya vijana wahitimu na kufanya upendeleo wakati zikitokea nafasi za ajira.
 
Wajiunge betting wamlize mhindi, kuacha kubet na kutegemea ajira ni uoga wa maisha🤣
 
Hakuna sheria inayotaka anayejitolea ndiyo aajiriwe. Mkitaka hivyo nendeni bungeni mkabadiri sheri kwanza. Hayahaya ndiyo tulikuwa tunakataa kwa jiwe.
 
Nakumbuka kujitolea kwa mwaka mmoja na nusu ndio kulifungua fursa ya ajira yangu katika shirika moja kubwa na nyeti la umma hapa nchini.. Acheni Mungu aitwe Mungu.
 
Kwa nchi za wenzetu kujitolea ina maana kubwa na kuongeza thamani isipokuwa kibongo bongo ni udhaifu, kujipendekeza, kutumika pia kuzalisha wezi na kuchochea matendo ya rushwa.

Usipo mlipa anayefanya kazi basi ujue kuna namna ya ambavyo anajilipa.
 
Back
Top Bottom