Wahudumu wa Mwendokasi Kivukoni jirekebisheni, muwe na kauli nzuri na tafuteni tiba ya kukosa "chenji", ni kero kwa Abiria

Bado Hujasema

Member
Joined
Dec 1, 2024
Posts
12
Reaction score
14
Pale Kivukoni sehemu ya kukatia tiketi katika Kituo cha Mwendokasi pa hovyo sana.

Kwanza abiria ni wengi wanasongamana mno wanagombea tiketi. Mtu unakomaa kwenye foleni hadi unafanikiwa kufika dirishani, hapo unakuwa umepambana hasa.

Sasa unafika dirishani unataka ukate tiketi fasta fasta uwahi usafiri unakutana na mhudumu ambaye furaha yake ni kukuharibia siku.

Leo nimekutana na mkaka amekaa dirisha la kushoto, kijana jeuri sana yule na anaonesha hana adabu wala hajali kuhusu sisi wateja, anahudumia Watu kama tunasafiri bure au anatupa msaada. Anatoa majibu ya jeuri wala hajali kumkosea mtu heshima mbele ya wengine.

Anasema hana chenji, nikamuuliza kwahiyo nifanyeje? Akajibu "Kaa pembeni kama unaona nakuchelewesha, kapange foleni nyingine"

Acheni kufanyia watu wazima dharau tena mnawajibu kama mnaongea na wahuni kijiweni.

Hii sio mara ya kwanza kutokea changamoto ya chenji, kila mara nimeshuhudia hali hiyo ambayo imekuwa chanzo cha ugomvi na kupishana kauli baina ya Abiria na Wakatishaji tiketi.

Kwani hao wahusika hawawezi kutafuta njia mbadala badala ya kumpa kazi Abiria awe anatafuta chenji mwenyewe? Hawaoni kama suala hilo ni kero kubwa?

 

Attachments

  • Snapchat-479243513.jpg
    314.8 KB · Views: 3
Ndiomaana mimi nikisikiaga watu wamepata ajali mbaya kama ile ya gorofa kuanguka huwa sionagi hata huruma,sababu miongoni mwao yapo mashetani yamekufa katika wema waliokufa,au kulionea huruma jitu linalopitia maswaibu fulani,wengine Mungu anawapitisha kwenye moto hapahapa duniani sababu walikuwa na nyodo na kibri enzi zao mafanikio yao au wakati walipokuwa hai.
 
Wana tabia za hovyo sana, sijaona uafadhali wa kubadili system ya uendeshaji bado mambo ni yale yale tu. Kuna siku nna haraka nimepanga foleni nimefika pale naomba tiketi anasema hana chenchi ilikuwa ni buku, nikamwambia baki na chenchi nipe tiketi lakini bado halikuelewa likasema sogea dirisha la katikati.
 
Wanataka chenchi kamili
 
Huu mradi wa kitapeli hakustahili kabisa Kwa Nchi yetu ambayo vilaza kama hao wahudumu ndiyo wanaosimamia shughuli za Kila siku za mradi.Mradi ambao ungefaa ni reli tu.Reli angalau hawana upuuzi kama wa mwendokasi
 
J
Sasa mimi niliona wasinicheleweshe nikaomba nipewe tiketi chenchi wabaki nayo, bado tabu
uzi Nampa teni, kahesabu bukubuku,

Nikazikunja hata sijahesabu..... nawahi gari..... Ile nafika mbona haikamilki na sio mara moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…