Waimbaji wa kilokole wanaongoza kwa kuvaa vibaya kwenye video zao

mitale na midimu

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2015
Posts
10,420
Reaction score
17,735
Ukiangalia waimbaji wa nyimbo za kiimani angalau wakatoliki na wasabato na baadhi ya kwaya kubwa hasa AIC na KKKT.

Nikiangalia hii channel inaitwa Star Religion wanaonyesha nyimbo za injili nagundua...

1: Waimbaji karibu 90% wanajivalia ovyoovyo kana kwamba hakuna mstari wa kimaadili unaowatenganisha na waimbaji wa nyimbo za kidunia. Viduku, suruali zilizochanikachanika, vimini, milegezo.

2: Wengi inaonekana wanaiga nyimbo na mitindo ya nyimbo ambazo sio za dini.

3: Ukimute mtu mwingine akaingia atasema unaangalia Bongoflavour au RnB.


Taratibu mstari unaotenganisha mambo ya kiimani na ya kidunia unaenda unafutika....
 
Hahaha kuvaa kuvaa nako kuna dini jamani?! Mnataka wavae majoho ya kanisani kila kona mtawaua kwa joto jamani.
 
Kweli kabisa inabidi wabadilike wameanza kujisahau

Kwaya za Zaman walikuwa wanavaa kwa staha sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…