Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 12,675
- 25,924
Sikuona lililotokea, je mtu anathibitisha aje na anathibitisha nini?Hujanielewa. Mahakamani,na kwenye uandishi wa viapo vya kisheria,kwa mujibu wa dini yao Waislam huthibitisha,hawaapi. Ila wakristo huapa. Sasa leo aliyethibitisha ni mchengerwa peke yake ambaye ni mwanasheria,alikuwa hakimu zamani. Wengine woote ameapa. Na siamini kama typing ya kiapo kile cha mchengerwa kiliandikwa kuapa au kuthibitisha. Ila yeye kwasababu anaijua sheria na dini yake amefanya kile dini inataka. Wengine wameapa wakati kisheria walitakiwa kuthibitisha.
Kuna exception kisheria kwamba kama muislam akiapa badala ya kuthibitisha hakuna tatizo?
Mahakamani ukipeleka affidavit ya muislam akiwa ameapa mahakama inaitupilia mbali,anatakiwa kuthibitisha. Pamekaaje hapo?
Hili ni suala la kisheria. Kwa mujibu wa dini ya kiislam,huwezi kuapa lwa mungu, unathibitisha.Sikuona lililotokea, je mtu anathibitisha aje na anathibitisha nini?
Ahsante kwa ufafanuzi.Hili ni suala la kisheria. Kwa mujibu wa dini ya kiislam,huwezi kuapa lwa mungu, unathibitisha.
Ndio maana ukiandika kiapo/afdidavit za mahakamani,au ukitakiwa kuapishwa kama shahidi, sheria inasema wakristo wataapa ila waislam watathibitisha. Hii ipo dunia yote.hata ukienda Uingereza utakuta ipo hivyo.
Yaani ukifika pale ukapewa Biblia kama wewe ni mkristo utasema "naapa kwamba....Mungu nisaidie". Ila ukiwa muislam utapewa Quran utanyoosha juu na hutakiwi kuapa kwa quran,unathibitisha,ndio dini inavyosema, utasema " walah bilah wataalah,nathibitisha kwamba...." Hozo ndio aina za viapo kwa wakristo na waislam kisheria.
Usipofanya hivyo,hujaapa kisheria.
Sasa jana Mchengerwa peke yake ambaye ni muislam na anafahamu hili kwasababu amekuwa hakimu kwa muda mrefu huko nyuma,walipompa quan hakusema naapa,alisema nathibitisha. Yeye tu ndio alikuwa sahihi.
Waislam wengine woote waliapa. Sasa swali ni je, kiapo chao ni sahihi? Hao walioapa badala ya kuthibitisha.
Mchengerwa peke yake ndio amethibitisha kwa waislam wote walioapishwa leo, naye ni kwasababu alikuwa hakimu, anaelewa. Kisheria, waislam tumezoea huwa hawaapi, wanathibitisha. Wakristo ndio wanaapa. Au kuna exception?