Waislam na Wakristo tunaiangamiza Tanzania

Waislam na Wakristo tunaiangamiza Tanzania

Hi tech

Member
Joined
Oct 21, 2013
Posts
31
Reaction score
9
Habari Great thinkers

Ninajua kila mtu anaamini dini yake na kuamini kila kitu kipo sahihi kuhusiana na mambo yanayohusu dini yake. Lakini mimi ninasikitishwa sana na kuchokozana baina ya Wakristo na Wailslamu Tanzania. Leo hii ninataka nibainishe mapungufu ya hizi pande mbili kila mmoja achukue nafasi yake kwani bila ya hivyo ipo siku tutajuta na Tanzania haitakalika.

Mapungufu ya Wakristo Tanzania
(1)Wanaamini lazima taasisi au makampuni yote waongoze wao akiongoza Muislam ata taasisi au idara moja kati ya kumi kwao ni shida, wataanza dharau kejeli na underground campaign ata kama anayeongoza ana perform.
(2)Wana maneno ya kejeli kwa Waislam utasikia mara mikanzu yake mara mi kandambili mbaya zaid wanalitumia kwenye kejeli zao jina la Mtume Muhammad bila ya kufikiri ni jinsi gani inawaumiza Waislam hasa hapa JF.
(3)Matajiri, Wafanyabiashara na Waajiri wa Kikristo wana ubaguzi wa wazi katika taasisi ambazo si za dini,mfano Reginald Mengi amewapendelea Wakristo katika ajira na media zake za IPP, kama EATV unaweza zani ni tv ya kanisa kwa kwaya na mambo mengine, mbona hapigi Qasida kila mara kama anavyopiga kwaya.
(4)Siku za hivi karibuni kila kitu wanakitafsiri kwa misingi ya dini.
(5)Wapo viongozi wa zamani na sasa walitumia nafasi yao kudhoofisha Waislam.
(6) Wana ujanja ujanja wa kutumia mali za umma au serekali kusaidia makanisa au ukristo.

Mapungufu ya Waislam
(1)Hawana mipango madhubuti ya kuwaendeleza katika elimu ambayo inaweza wafanya wawe suitable katika usimamizi wa makampuni au taasisi mbali mbali, matokeo wanalazimisha lazima waongoze wao ata kama hawana vigezo.Ninajua wapo wenye vigezo lakini kwa asilimia ndogo ukilinganisha na Wakristo.
(2)Wana maneno ya kejeli na kujiona wao wanajua ustarabu na ubinadamu kuliko wenzao utasikia mara kafiri mara kile mara bwasha.
(3)Matajiri Wafanyabiashara na waajiri Waislam wanaubaguzi wa dhahiri, mfano Bakhresa ameajiri kwa upendeleo kwa Waislam sana kiasi kwamba kuna watu wanabadilisha majina waonekane ni Waislam ili kupata kazi ata ya udereva kwenye kampuni zake, hali hii pia ipo Oilcom kiasi fulani.
(4)Siku za hivi karibuni kila kitu wanakitafsiri kwa misingi ya dini.
(5)Wanaacha na kushabikia baadhi ya watu kama Shehe Ponda wanahubiri chuki na ugomvi baadala ya kushawishi watu wajiunge na Uislam pia uongozi wa Bakwata hauko madhubuti na hawako Tayari kubadilika.
(6) Dunia nzima Waislam ni rahisi kuwagawanya, kuwagombanisha na kuwatumia kwa maslahi binafsi mifano mnayo.
(7) Baadhi ya familia za Kiislam hawako tayari kuingia gharama au kuwa committed ili watoto wao waende mbele Kielimu, ni wazi elimu zote mbili wako nyuma vyuo vikuu vyetu ni wachache na ata elimu ya dini hawapo kwenye mfumo rasmi pamoja na kuwepo na uwezo wakiamua.
(8) Baadhi ni wabishi kila kitu hawataki kutafakari katika mambo yanayotokea.

Jambo baya zaidi katika mambo ambayo Waislam na Wakristo wangeletwa pamoja na Serikali kama miaka michache ya nyuma hali imekua tete kwani wenye madaraka kwenye idara za serikali wameshindwa kuficha hisia zao,na kufanya maamuzi yenye element za udini.

Karibuni wanajukwaa kwa kuchngia ukizingatia malengo Mawili, (1) Dini yako iweze songa mbele na kuwa na nguvu na waumini wengi (2) Tanzania iwe sehemu salama kwa binadamu yeyote ata yule ambaye si wa dini yako. Kubwa zaidi jitahidi kuwa muwazi na mkweli lakini epuka kejeli na dharau kwa mwenzio. Tujadili ili miaka michache ijayo tukiwa kama Nigeria au Misri, tuzisute nafsi zetu.
 
Nimeufurahia msemo k uwa wote wana ubaguzi katika ajira.
kuhusu Kwaya EATV mbona hujiulizi Qasidwa Abood TV.

Bazazi!
 
hizi dini zote misingi yake ni ulafi hazina tija na uwongo wao wa dhahiri eti ukifa unaenda mahali nk.... hatuziitaj na as long as bado zipo kwenye jamii zetu mitafaruku haitaweza isha kwan zimejengwa ktk misingi ya kupata waumin zaidi na kila moja anataka abaki peke yake akicontrol maisha ya wanadam kwa teaching zao hewa!!! enzi na enzi mababu zetu waliishi kwa amani kabisa bila kubaguana na kuendelea kama jamii moja!!!
 
tatizo ni content ya dini zimebanguliwa na kuleta mambo yasiyo ya dini
 
Habari Great thinkers

Ninajua kila mtu anaamini dini yake na kuamini kila kitu kipo sahihi kuhusiana na mambo yanayohusu dini yake. Lakini mimi ninasikitishwa sana na kuchokozana baina ya Wakristo na Wailslamu Tanzania. Leo hii ninataka nibainishe mapungufu ya hizi pande mbili kila mmoja achukue nafasi yake kwani bila ya hivyo ipo siku tutajuta na Tanzania haitakalika.

Mapungufu ya Wakristo Tanzania
(1)Wanaamini lazima taasisi au makampuni yote waongoze wao akiongoza Muislam ata taasisi au idara moja kati ya kumi kwao ni shida, wataanza dharau kejeli na underground campaign ata kama anayeongoza ana perform.
(2)Wana maneno ya kejeli kwa Waislam utasikia mara mikanzu yake mara mi kandambili mbaya zaid wanalitumia kwenye kejeli zao jina la Mtume Muhammad bila ya kufikiri ni jinsi gani inawaumiza Waislam hasa hapa JF.
(3)Matajiri, Wafanyabiashara na Waajiri wa Kikristo wana ubaguzi wa wazi katika taasisi ambazo si za dini,mfano Reginald Mengi amewapendelea Wakristo katika ajira na media zake za IPP, kama EATV unaweza zani ni tv ya kanisa kwa kwaya na mambo mengine, mbona hapigi Qasida kila mara kama anavyopiga kwaya.
(4)Siku za hivi karibuni kila kitu wanakitafsiri kwa misingi ya dini.
(5)Wapo viongozi wa zamani na sasa walitumia nafasi yao kudhoofisha Waislam.
(6) Wana ujanja ujanja wa kutumia mali za umma au serekali kusaidia makanisa au ukristo.

Mapungufu ya Waislam
(1)Hawana mipango madhubuti ya kuwaendeleza katika elimu ambayo inaweza wafanya wawe suitable katika usimamizi wa makampuni au taasisi mbali mbali, matokeo wanalazimisha lazima waongoze wao ata kama hawana vigezo.Ninajua wapo wenye vigezo lakini kwa asilimia ndogo ukilinganisha na Wakristo.
(2)Wana maneno ya kejeli na kujiona wao wanajua ustarabu na ubinadamu kuliko wenzao utasikia mara kafiri mara kile mara bwasha.
(3)Matajiri Wafanyabiashara na waajiri Waislam wanaubaguzi wa dhahiri, mfano Bakhresa ameajiri kwa upendeleo kwa Waislam sana kiasi kwamba kuna watu wanabadilisha majina waonekane ni Waislam ili kupata kazi ata ya udereva kwenye kampuni zake, hali hii pia ipo Oilcom kiasi fulani.
(4)Siku za hivi karibuni kila kitu wanakitafsiri kwa misingi ya dini.
(5)Wanaacha na kushabikia baadhi ya watu kama Shehe Ponda wanahubiri chuki na ugomvi baadala ya kushawishi watu wajiunge na Uislam pia uongozi wa Bakwata hauko madhubuti na hawako Tayari kubadilika.
(6) Dunia nzima Waislam ni rahisi kuwagawanya, kuwagombanisha na kuwatumia kwa maslahi binafsi mifano mnayo.
(7) Baadhi ya familia za Kiislam hawako tayari kuingia gharama au kuwa committed ili watoto wao waende mbele Kielimu, ni wazi elimu zote mbili wako nyuma vyuo vikuu vyetu ni wachache na ata elimu ya dini hawapo kwenye mfumo rasmi pamoja na kuwepo na uwezo wakiamua.
(8) Baadhi ni wabishi kila kitu hawataki kutafakari katika mambo yanayotokea.

Jambo baya zaidi katika mambo ambayo Waislam na Wakristo wangeletwa pamoja na Serikali kama miaka michache ya nyuma hali imekua tete kwani wenye madaraka kwenye idara za serikali wameshindwa kuficha hisia zao,na kufanya maamuzi yenye element za udini.

Karibuni wanajukwaa kwa kuchngia ukizingatia malengo Mawili, (1) Dini yako iweze songa mbele na kuwa na nguvu na waumini wengi (2) Tanzania iwe sehemu salama kwa binadamu yeyote ata yule ambaye si wa dini yako. Kubwa zaidi jitahidi kuwa muwazi na mkweli lakini epuka kejeli na dharau kwa mwenzio. Tujadili ili miaka michache ijayo tukiwa kama Nigeria au Misri, tuzisute nafsi zetu.


Nina mashaka na kujua na kuamini kwako maana unamjua kila mtu kwenye dini yake....na si wote kwenye dini yoyote ile wanajua na kuamini dini zao na ndiyo maana ni wachache tu wanaoendana na maadili ya dini zao hivyo napinga mawazo yako ya kila mtu kujua na kuamini kile anachoamini wengine hawajui wanachoamini.

Pia dini kama njia ya kimaadili yenye kumwongoza mtu afikie lengo lake la kimbingu watu wengi hawawezi kuijua njia sahihi si wakristo wala waislamu maana Mungu si mwenye taahira ya akili aweke njia(dini) nyingi zenye kupingana kimawazo hata kama wanamtamka Mungu.

Mwisho serikali haina vitabu vikubwa vya teolojia au taalimumungu vyenye uwezo wa kuwaongoza watu wamjue Mungu zaidi ya vitabu vya wanateolojia wa dini mbalimbali ndiyo maana serikali inatumia sheria zake zenyewe na hata vyombo vya habari vya kiislamu haviwezikutangazwa namtu asiyejua quran vizuri:A S-key:AKILI.
 
Mkuu uliyeleta uzi nakupongeza sana, umesahau moja kuwa dini zote hizo mbili zimeletwa na mbaya zaidi zinatudharau sisi watu wa dini za jadi eti "wapagani". Jibu lao Afande Sele keshajibu katika wimbo wake wenye maudhui wa dini hizo mbili ulizozitaja. Acha sisi wapagani tuendelee kuabudu mizimu, la maana hatutafuti wafuasi kama hao wengine.
 
Ahsante kwa mchango wako,ila katika kila jambo nililoandika na wewe kulijadili umenielewa tofauti
Nina mashaka na kujua na kuamini kwako maana unamjua kila mtu kwenye dini yake....na si wote kwenye dini yoyote ile wanajua na kuamini dini zao na ndiyo maana ni wachache tu wanaoendana na maadili ya dini zao hivyo napinga mawazo yako ya kila mtu kujua na kuamini kile anachoamini wengine hawajui wanachoamini.

Pia dini kama njia ya kimaadili yenye kumwongoza mtu afikie lengo lake la kimbingu watu wengi hawawezi kuijua njia sahihi si wakristo wala waislamu maana Mungu si mwenye taahira ya akili aweke njia(dini) nyingi zenye kupingana kimawazo hata kama wanamtamka Mungu.

Mwisho serikali haina vitabu vikubwa vya teolojia au taalimumungu vyenye uwezo wa kuwaongoza watu wamjue Mungu zaidi ya vitabu vya wanateolojia wa dini mbalimbali ndiyo maana serikali inatumia sheria zake zenyewe na hata vyombo vya habari vya kiislamu haviwezikutangazwa namtu asiyejua quran vizuri:A S-key:AKILI.
 
Mapungufu ya Wakristo Tanzania
(1)Wanaamini lazima taasisi au makampuni yote waongoze wao akiongoza Muislam ata taasisi au idara moja kati ya kumi kwao ni shida, wataanza dharau kejeli na underground campaign ata kama anayeongoza ana perform.
(2)Wana maneno ya kejeli kwa Waislam utasikia mara mikanzu yake mara mi kandambili mbaya zaid wanalitumia kwenye kejeli zao jina la Mtume Muhammad bila ya kufikiri ni jinsi gani inawaumiza Waislam hasa hapa JF.
(3)Matajiri, Wafanyabiashara na Waajiri wa Kikristo wana ubaguzi wa wazi katika taasisi ambazo si za dini,mfano Reginald Mengi amewapendelea Wakristo katika ajira na media zake za IPP, kama EATV unaweza zani ni tv ya kanisa kwa kwaya na mambo mengine, mbona hapigi Qasida kila mara kama anavyopiga kwaya.
(4)Siku za hivi karibuni kila kitu wanakitafsiri kwa misingi ya dini.
(5)Wapo viongozi wa zamani na sasa walitumia nafasi yao kudhoofisha Waislam.
(6) Wana ujanja ujanja wa kutumia mali za umma au serekali kusaidia makanisa au ukristo.

Nashindwa hata haya madai yako niyaiteje
Kwa uungwana tu nakuomba unipe ushahidi wa haya madai yako,ukishindwa tutake radhi!
 
Mtoa maada hii ni rahisi kukujua unapoegemea,great thinker yeyote atagundua tu kuwa umejaribu kutoa NEGATIVE CRITICISM upande mmoja na POSITIVE CRITICISM upande mwingine.
 
Back
Top Bottom