Pre GE2025 Wait, hili Taifa lina sera isiyoandikwa wala kuandikika kuhusu nafasi za urais wa Taifa hili?

Pre GE2025 Wait, hili Taifa lina sera isiyoandikwa wala kuandikika kuhusu nafasi za urais wa Taifa hili?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Kwa chama tawala tayari tumeona ndugu Nchimbi yupo pale kuchukua nafasi ya Dkt. Mpango, ambapo Rais aliyepo ni ndugu Samia. Aliyemtangulia ni Hayati Magufuli. Au tuweke hivi;
1. Rais wa kwanza Nyerere - Karume, Jumbe, Mwinyi
2. Rais wa pili Mwinyi -
3. Rais wa tatu Mkapa - Omar, Shein
4. Rais wa nne Kikwete - Shein, Bilal
5. Rais wa tano Magufuli - Samia
6. Rais wa sita Samia - Dr Mpango, Dr Nchimbi

Hapo juu aliyetia doa ni wa awamu ya nne. Sasa tunapokuja kwa upande wa upinzani, tunaenda kushuhudia Mbowe na Lissu wakienda kuchuana kuhusu nani awe mwenyekiti wa CHADEMA. sasa no hivi, kwa mujibu wa takwimu na sera isiyoandikwa kuhusiana na uongozi wa Taifa hili, ni wazi anayekwenda kuwa Mweyekiti wa CHADEMA ni Mbowe.

Kadhalika kama nilivyowahi kuandika awali, na hapa busara itumike sana. Licha ya busara, pia wapo watu nyuma ya pazia wanaopanga karata zao vyema sana. Hivyo basi, akishashinda na kuwa mwenyekiti, nafasi ya kugombea urais atapewa Lissu.

Hivyo basi hali halisi itategemea na upepo utakaokuwepo katika uchaguzi mkuu. Kama Lissu aliweza kumpa tumbo joto Magufuli, ni wazi kwamba Samia atakuwa 'mboga' kwa Lissu. Hapo wafanya maamuzi wa Taifa wataamua kuikabidhi nchi kwa Lissu kama ikibidi. Kama Lissu anataka kugombea urais ni lazima akubali kuukosa uenyekiti. Japo huu ni mtazamo wangu, ndio uhalisia.
 
Zipo kozi za urais zisizozidi miezi 6. Pia kwa mtizamo wa kibinadamu inawezekana isiwezekane

Nafikiri hujui msingi wa hii nchi umejengwa wapi na umejengwaje.

Lisu hawezi kuwa Rais wa hii nchi bila kuvunja huo msingi
Na Akiwa Rais Wakuu wanajua huo msingi utavunjwa. Nani yupo tayari kuangamizwa?
 
Nafikiri hujui msingi wa hii nchi umejengwa wapi na umejengwaje.

Lisu hawezi kuwa Rais wa hii nchi bila kuvunja huo msingi
Na Akiwa Rais Wakuu wanajua huo msingi utavunjwa. Nani yupo tayari kuangamizwa?
Karibu ndugu Mtibeli kwa darasa maridhawa kuhusiana na msingi wa Taifa hili. Kadhalika wapo waliotangulia na kuwa marais kwa hiyo misingi kukiukwa (ila si kwa kupenda). Wapo marais kama Mwinyi, Magufuli, na Samia. Hawa kwa mujibu wa misingi unayoizungumzia, hawakuwepo kwenye orodha ila ilitokea la kutokea na wakawa marais.

Kuhusu kuangamizwa, japo sijajua kiundani, tayari tumeangamizwa vya kutosha kwa sera za uwekezaji zinazoendelea
 
Karibu ndugu Mtibeli kwa darasa maridhawa kuhusiana na msingi wa Taifa hili. Kadhalika wapo waliotangulia na kuwa marais kwa hiyo misingi kukiukwa (ila si kwa kupenda). Wapo marais kama Mwinyi, Magufuli, na Samia. Hawa kwa mujibu wa misingi unayoizungumzia, hawakuwepo kwenye orodha ila ilitokea la kutokea na wakawa marais.

Kuhusu kuangamizwa, japo sijajua kiundani, tayari tumeangamizwa vya kutosha kwa sera za uwekezaji zinazoendelea

Lisu hawezi kuwa Rais wa nchi hii bila umwagaji wa damu kutokea.

Chama cha Upinzani chochote hakitaweza kushika Dola nchi hii bila umwagaji wa damu kutokea.
 
Lisu hawezi kuwa Rais wa nchi hii bila umwagaji wa damu kutokea.

Chama cha Upinzani chochote hakitaweza kushika Dola nchi hii bila umwagaji wa damu kutokea.
Usemalo lina ukweli. CCM ni kama imejimilikisha hili Taifa. Tumeona hilo juzi na jana. Sasa kwa kuwa kauli ya Baba wa Taifa haitimii (upinzani wa kweli utatokea ccm), sisi ni kina nani tuukwepe huo mwelekeo?
 
Marais walioibuka tu bila formula ilivyotakiwa iwe wapo ndio but aliyepata baraka kwa watanzania pamoja na kuibuka kwake ni jpm ndo mana wengine wakaenda mbali sana na kusema hapo ni nguvu ya MUNGU imemtumia nabii musa kwa wana wa israel sasa bhc mwingne ambae amebeba hyo nyota ni LISSU ikiwa atapita na akawa presidential naamini watanzania watasahau machungu ya hayati jpm..
WASALAAM
 
Marais walioibuka tu bila formula ilivyotakiwa iwe wapo ndio but aliyepata baraka kwa watanzania pamoja na kuibuka kwake ni jpm ndo mana wengine wakaenda mbali sana na kusema hapo ni nguvu ya MUNGU imemtumia nabii musa kwa wana wa israel sasa bhc mwingne ambae amebeba hyo nyota ni LISSU ikiwa atapita na akawa presidential naamini watanzania watasahau machungu ya hayati jpm..
WASALAAM
Yah, hope tupo na mtizamo mmoja
 
Back
Top Bottom