Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Leo Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara alikuwa kwenye kipindi cha 'Morning Trumpet' cha Azam TV na amegusia mambo mbalimbali ikiwemo hasara ATCL, ujenzi bandari ya Bagamoyo, ujenzi reli ya SGR na uagizaji wa mabehewa pia ujenzi bwawa la Nyerere
===
Mtangazaji: Umezungumza kuhusu hali ya viwanja vya ndege, vipi kuhusiana na hali ya shirika letu la ndege? Ripoti ya CAG imesema shirika hili limekuwa likiendeshwa kwa hasara na bodi ya wakurugenzi haina wataalam wa masuala ya anga. Mnafanya nini ili shirika la ndege kutengeneza faida au basi kupunguza hasara
Waziri Waitara: Ripoti tuliiona na tuliisoma, tulielekeza wataalam watupe majibu ya zile hoja kabla ya kwenda kwa CAG. Jana nimekaa na watu wa ATCL, tukawaambia mojawapo ya sintafahamu ni jinsi zile ndege zinavyo-operate.
Sisi hatupati faida ya moja kwa moja, vile viwanja vya ndege na ndege zenyewe ni vitu vinavyowezesha lakini wale abiria na hasa watalii wanapoingia, zile shughuli wanazoenda kufanya kule, wamepanda mlima Kilimanjaro, wamelala kwenye mahoteli. Yote yale kwa ujumla ndio unaweza ukajumuisha ile faida, sasa hicho kitu watu wengi hawaelewi, duniani kote watakwambia tunapata hasara kwa sababu ile faida sio ya moja kwa moja.
BWAWA LA NYERERE
Waitara: Huwezi kutaja bwawa la Mwalimu Nyerere bila kumtaja hayati Magufuli na mama Samia mwenye na Majaliwa, hawa ndio viongozi wa nchi ambao walikaa na kuamua.
Mradi huu ulikuwa na makandokando mengi, kwasababu kwanza hawakutaka uanze kabisa, wakasema hii habari ya mazingira lakini kulikuwa na hoja huko nyuma, tukipewa sisi watanzania kuna hoja ya mazingira lakini wakipewa wao wakatekeleza hoja ya mazingira inakufa ndio maana viongozi wakasema hapana, tutumie rasimali ambayo tunayo na unaambiwa hiyo ni asilimia 1, sehemu kubwa zaidi ya asilimia 98 imebaki kuwa hifadhi
===
Mtangazaji: Umezungumza kuhusu hali ya viwanja vya ndege, vipi kuhusiana na hali ya shirika letu la ndege? Ripoti ya CAG imesema shirika hili limekuwa likiendeshwa kwa hasara na bodi ya wakurugenzi haina wataalam wa masuala ya anga. Mnafanya nini ili shirika la ndege kutengeneza faida au basi kupunguza hasara
Waziri Waitara: Ripoti tuliiona na tuliisoma, tulielekeza wataalam watupe majibu ya zile hoja kabla ya kwenda kwa CAG. Jana nimekaa na watu wa ATCL, tukawaambia mojawapo ya sintafahamu ni jinsi zile ndege zinavyo-operate.
Sisi hatupati faida ya moja kwa moja, vile viwanja vya ndege na ndege zenyewe ni vitu vinavyowezesha lakini wale abiria na hasa watalii wanapoingia, zile shughuli wanazoenda kufanya kule, wamepanda mlima Kilimanjaro, wamelala kwenye mahoteli. Yote yale kwa ujumla ndio unaweza ukajumuisha ile faida, sasa hicho kitu watu wengi hawaelewi, duniani kote watakwambia tunapata hasara kwa sababu ile faida sio ya moja kwa moja.
BWAWA LA NYERERE
Waitara: Huwezi kutaja bwawa la Mwalimu Nyerere bila kumtaja hayati Magufuli na mama Samia mwenye na Majaliwa, hawa ndio viongozi wa nchi ambao walikaa na kuamua.
Mradi huu ulikuwa na makandokando mengi, kwasababu kwanza hawakutaka uanze kabisa, wakasema hii habari ya mazingira lakini kulikuwa na hoja huko nyuma, tukipewa sisi watanzania kuna hoja ya mazingira lakini wakipewa wao wakatekeleza hoja ya mazingira inakufa ndio maana viongozi wakasema hapana, tutumie rasimali ambayo tunayo na unaambiwa hiyo ni asilimia 1, sehemu kubwa zaidi ya asilimia 98 imebaki kuwa hifadhi