Naagiza simu na vifaa vya simu hasa hasa samsung ambapo kwa kawaida ukienda Kariakoo vifaa vyake huwa vina gharama sana...Nilianza kuagiza vifaa ivi mara tu baada ya simu yangu Samsung S9+ kuharibika kioo, nilipoenda Kariakoo nikaambiwa ya kwamba kioo ni 410,000...Nilipoagiza online nikapata kioo kwa 212,000 pamoja na usafiri...Ndipo niliposhtuka na kuanza kuagizia watu wengine..Kwa iyo nilianza kwa ajili ya matumizi yangu binafsi..Sina mtaji nilioanza nao..Kwa sasa ni mjasiliamali,watu wameniamini,, nafanya biashara nikiwa kwenye ajira yangu bila stress..
Kazi zipo ishu ni ubunifu tu wa mtu binafsi..Tupambane