Wajasiliamali wa chini kabisa na sakata la mikopo

Wajasiliamali wa chini kabisa na sakata la mikopo

majoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
2,595
Reaction score
4,775
Wandugu tupeane A BC za kumaintain biashara ndogo ndogo ili tuwasaidie wenzetu wanaotaabika na mikopo ya kausha damu. Hapa tuwaongelee wale wajasiliamali wa chini kabisa. Kundi hili linateseka mno mno kwa kujitahidi kujikwamua lakini hawajui jinsi ya kujikwamua.

Nimeumia sana kuna ndugu zangu wanateseka mnoooo na mikopo jamani hadi wanafikia stage ya kujificha au kuhama mtaa usiku kisa kakopa uli aanzishe biashara ya kuuza mbogamboga kabla ya kujua soko na biashara inavyokwenda. Mwingine kakopa ili anunue mfuko wa Azam ngano ili auze maandazi.

Mwingine ndio kaniacha hoi kabisa eti biashara yake ya bagia ilikuwa inaenda vizuri ila kuna mtu jirani anamroga... ukichunguza unagundua anatumia fedha za biashara hadi mitaji inakata deni na riba vinamsonga! Ukimuuliza ilikuwaje hii biashara unaijua... anakujibu niliambiwa inalipa.

Wanawake mtaani wanahaha na mikopo.... akisikia kuna mkopo huku yumo.... anakopa huku analipa huku biashara inakata ili mradi tafrani.
 
Kama mwanaume hakikisha ndio producer mkuu kwenye familia yako,,,, usitegemee pesa ya mwanamke kama ana kipato,,, akitoa its OK, asipotoa its OK pia !

Hakikisha pia mkeo hajihusishi na huu ujinga wa kausha damu, vikoba, sijui michezo n.k ! Sana sana ni kuidhalilisha familia tu hakuna kingine cha maana ! Najua wanacheza kwa siri, mpe onyo kali, ikitokea umemkamata take action !
 
Kama mwanaume hakikisha ndio producer mkuu kwenye familia yako,,,, usitegemee pesa ya mwanamke kama ana kipato,,, akitoa its OK, asipotoa its OK pia !

Hakikisha pia mkeo hajihusishi na huu ujinga wa kausha damu, vikoba, sijui michezo n.k ! Sana sana ni kuidhalilisha familia tu hakuna kingine cha maana ! Najua wanacheza kwa siri, mpe onyo kali, ikitokea umemkamata take action !

Huu mchezo huwa wanauanza kwa siri sana. Hadi ukija kujua utashangaa kundi limekuja kubeba makochi yaliyowekwa dhamana
 
Wandugu tupeane A BC za kumaintain biashara ndogo ndogo ili tuwasaidie wenzetu wanaotaabika na mikopo ya kausha damu. Hapa tuwaongelee wale wajasiliamali wa chini kabisa. Kundi hili linateseka mno mno kwa kujitahidi kujikwamua lakini hawajui jinsi ya kujikwamua.

Nimeumia sana kuna ndugu zangu wanateseka mnoooo na mikopo jamani hadi wanafikia stage ya kujificha au kuhama mtaa usiku kisa kakopa uli aanzishe biashara ya kuuza mbogamboga kabla ya kujua soko na biashara inavyokwenda. Mwingine kakopa ili anunue mfuko wa Azam ngano ili auze maandazi.

Mwingine ndio kaniacha hoi kabisa eti biashara yake ya bagia ilikuwa inaenda vizuri ila kuna mtu jirani anamroga... ukichunguza unagundua anatumia fedha za biashara hadi mitaji inakata deni na riba vinamsonga! Ukimuuliza ilikuwaje hii biashara unaijua... anakujibu niliambiwa inalipa.

Wanawake mtaani wanahaha na mikopo.... akisikia kuna mkopo huku yumo.... anakopa huku analipa huku biashara inakata ili mradi tafrani.
Hiii mikopo kwakwel wanawake inawaua, njaa imezidi yote hiyo ni katika kuponya njaa
 
Hiii mikopo kwakwel wanawake inawaua, njaa imezidi yote hiyo ni katika kuponya njaa
Inawaua kweli. Tatizo wanakurupuka tu bila kufikiria jinsi watakavyoweza lipa hii mikopo. wengine wanafuata mkumbo tu kwa kuwa shost kakopa naye anakopa bila kujipanga. tuwasaidie kwa kweli
 
Inawaua kweli. Tatizo wanakurupuka tu bila kufikiria jinsi watakavyoweza lipa hii mikopo. wengine wanafuata mkumbo tu kwa kuwa shost kakopa naye anakopa bila kujipanga. tuwasaidie kwa kweli
wanapigika hatari, pande huu kuna Muha anahitaji marejesho ya buku lake kila siku, upande wa kulia alikopa kijora kwa mama mwajuma, mbele kuna kausha damu, lazima ukimbie usiku usiku
 
wanapigika hatari, pande huu kuna Muha anahitaji marejesho ya buku lake kila siku, upande wa kulia alikopa kijora kwa mama mwajuma, mbele kuna kausha damu, lazima ukimbie usiku usiku
Inabidi itafutwe mbinu ya kuwaelimisha. hawajielewi kabisa
 
Bongo wenye mikopo ya maana ni wachache mno, sema ugumu wa fursa ndio unasababisha mtu mwenye mkopo wa mil 10 kuona nae anadaiwa pesa ya maana.
 
wanapigika hatari, pande huu kuna Muha anahitaji marejesho ya buku lake kila siku, upande wa kulia alikopa kijora kwa mama mwajuma, mbele kuna kausha damu, lazima ukimbie usiku usiku
Cmu zinazimwa kwa muda!
 
Ukiacha wale wanawake wanaokopa kwa sababu ya tamaa na show off za mtaani, kuna kundi la wanawake ambao wamebeba mizigo ya familia zao walizotokea (baba,mama,wadogo zake etc). Unakuta yeye mwenyewe familia yake hawezi kuimudu peke yake bado nyumbani nako wanamtegemea. Hii inaumiza watu wengi wengi, na huwezi sema wazee uwaache wajifie bila msaada. Ndio mtu analazimika kuingia mikopo hatarishi.
 
Back
Top Bottom