Wajasiriamali wanaofanya biashara pembezoni mwa msikiti wa Mtoro Kariakoo watimuliwa

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Wajasiriamali wanaofanya biashara pembezoni mwa msikiti wa Mtoro wameitaka serikali kuingilia kati mgogoro unaoendelea kati yao na uongozi wa msikiti huo ambapo umewataka wafanyabiashara kuondoka eneo la barabara ambalo wanafanyia biashara kabla na baada ya matengenezo ya barabara.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa wafanyabiashara hao, Simba Lichanda amesema eneo hilo ndilo wanategemea kufanya biashara ili kutunza familia zao na wapo hapo kwa muda mrefu na viongozi wengi wanaswali na hakukuwahi kuwa na tofauti yoyote walipohitajika kupisha kwa ajili ya shughuli mbalimbali za msikiti huo.

Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…