Wajumbe wa BMK wanaozomea na kumtukana Mwenyekiti tuwafanye ili kuwa discipline?

Wajumbe wa BMK wanaozomea na kumtukana Mwenyekiti tuwafanye ili kuwa discipline?

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Ninadhani mmeshaona kuwa kuna wajumbe wachache katika bunge maalum la katiba IQ zao zina hitilafu na wamekuwa wakimzomea na kumtukana wazi wazi Mwenyekiti wa muda Mzee kificho ambaye hata kwa umri wake tu walipaswa kumheshimu kama baba yao. Wanalifanya Bunge letu maalum la katiba lionekane kama bunge la makangaroo au la vijiweni. Bunge hili halina mamlaka ya kuwashughulikia wajumbe hawa kwani ni wateule (kama ilivyojionyesha kwenye kanuni za bunge hili), na yule aliyewateua sheria haikumpa mamlaka ya kuwashughulikia.

Vyombo vya habari (media) ikiwemo JF, kama mhimili wa nne wa serikali nadhani vinapaswa kwa niaba ya Watanzania wote wenye nia njema kuwaadabisha wajumbe hawa wachache wanaojifanya ma 'much know' kwa kuwasema, kuwazomea n.k. Tuanze kwa kuwataja majina yao hapa. Mmoja niliyembaini anatoka mkoa wa Kigoma, jina lake bado sijalifahamu.
 
JK aliteua kundi la Ze Komedi! Ngoja watuburudishe hofu yangu ni kupata katiba safi!
 
Mimi nilisikia sauti ya kike ikipaza.." mtoto mdogo huna adabu" baadae ya kiume ikajibu kwa kupaza " kubwa zima ila jinga"......mwenyekiti akasimama na kumuomba radhi kwa kutompa muongozo mkosamali.......ikazuka sauti nyingine" wacha kumuomba mtoto mdogo radhi wewe"......kuona hivyo mkosamali nae akajibu " hakuna mtoto mdogo aliyeishinda CCM....".......hakika nilistaajabu.
 
Back
Top Bottom