Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 5,119
- 4,569
Kilichotokea jana saa 11 jioni kwenye kikao cha Bunge Maalum kiwe fundisho kwa M/Kiti na wengineo kwamba wajumbe wa Bunge hilo wasichakachuliwe kwa semina za kufua vifua n.k. na wala kwa hotuba ya Mzee Waryoba ya masaa kadhaa ya kuwakilisha rasimu yake. Rasimu iwakilishwe kwa muda usiozidi dakika 3 na ifuatiwe na nasaha (hotuba) toka kwa Mh. Rais wa Zanzibar na Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Wajumbe hawa wana vifua vinavyojitosheleza, hawahitaji semina toka kwa watu wengine ndani au nje ya nchi. Kama kuna kitu watakachohitaji watakiomba wenyewe kwenye kamati zao. Mbona kanuni zinaelekeza vizuri tu.
Wajumbe hawa wana vifua vinavyojitosheleza, hawahitaji semina toka kwa watu wengine ndani au nje ya nchi. Kama kuna kitu watakachohitaji watakiomba wenyewe kwenye kamati zao. Mbona kanuni zinaelekeza vizuri tu.