Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 49,390
- 152,301
Mimi nafikiri tumefanya kosa kubwa kuruhusu hawa wajumbe wa Bunge la katiba kuanza mchakato huu ikiwa ni pamoja na kuandaa kanuni za kuendesha Bunge hilo kabla ya kuwapatia semina maalumu juu ya utungaji na uandikaji wa katiba.
Semina hiyo ingekuwa na mada mbalimbali kama vile nini maana ya katiba,misingi ya katiba,kwanini wao wako pale,nini hasa jukumu na wajibu wao kwenye kuandika na kutunga katiba hiyo,miiko ya katiba, n.k.
Semina hiyo ingeendeshwa na watalaamu wa mambo ya katiba na pengine wangetoa elimu ambayo ingewasaidia katika jukumu lao hilo.Hii mivutano na kutoekewana ndani ya Bunge hili kumechangiwa na kukosekana kwa elimu juu uandikaji na utungaji wa katiba kwa wajumbe hawa
Kwa maneno mengine,wajumbe hawa hawajaandaliwa kisaikolojia kujua wajibu na jukumu lao katika kazi hiyo waliopewa kuifanya.
Labda niulize tu,hivi kama mawaziri waliandaliwa semina kule Ngurudoto Hotel,inakuwaje wajumbe hawa wenye jukumu nyeti kama hili hawakupewa semina ya kuwaweka sawa katika kazi yao?!
Kama swala ni gharama,hivi kuna gharama inayolingana na kupata katiba mbovu?
Semina hiyo ingekuwa na mada mbalimbali kama vile nini maana ya katiba,misingi ya katiba,kwanini wao wako pale,nini hasa jukumu na wajibu wao kwenye kuandika na kutunga katiba hiyo,miiko ya katiba, n.k.
Semina hiyo ingeendeshwa na watalaamu wa mambo ya katiba na pengine wangetoa elimu ambayo ingewasaidia katika jukumu lao hilo.Hii mivutano na kutoekewana ndani ya Bunge hili kumechangiwa na kukosekana kwa elimu juu uandikaji na utungaji wa katiba kwa wajumbe hawa
Kwa maneno mengine,wajumbe hawa hawajaandaliwa kisaikolojia kujua wajibu na jukumu lao katika kazi hiyo waliopewa kuifanya.
Labda niulize tu,hivi kama mawaziri waliandaliwa semina kule Ngurudoto Hotel,inakuwaje wajumbe hawa wenye jukumu nyeti kama hili hawakupewa semina ya kuwaweka sawa katika kazi yao?!
Kama swala ni gharama,hivi kuna gharama inayolingana na kupata katiba mbovu?