Wajuzi wa mambo wanisaidie kwa ushauri, nifanyeje ili niwe na afya njema

Dr.philosophy

Senior Member
Joined
Oct 12, 2012
Posts
122
Reaction score
27
Habar zenu wakuu..ndugu yenu Nina tatizo la kiafya huu Sasa ni mwaka wa Tisa...

Tatizo hili Lilianza mwaka 2010 nikiwa kidato Cha pili nikiwa shule mwili wngu ulianza kuwa na joto Kali Sana yaani napata homa flan kali mpaka mtu akinishika anashangaa kwann nachemka hivi.nikaanza kukonda na afya yangu ikawa inadhoofika siku Hadi siku...mara kwa mara niliokuw naenda hospital nilikuwa nakutwa na tyfhod,UTI au maralia hayo ndo yalikuwa magonjwa yngu Kila niendapo kupima...

Sasa ikafika wakati haipiti miezi miwili sjapima na kutumia dawa za magonjwa hayo,ndugu zangu nimekunywa Sana dawa za maralia UTI na typod yaan sanaa..wakat huo afya yngu ilikuw inaendlea kudhoofika Sana...ikafka wakti nkaamua kupimwa na maradhi makubwa Kama kisukari,presha,na HIV, Mara kwa Mara Kila nilipoenda hospital kupima ilikuwa lazma nipime na magonjwa hayo cjawahi kukutwa nayo...mpaka leo hii saiv karibu Kila mwez lazma niende hospital kupimwa na wakat mwngine sikutwi naugonjwa wowote lakin bdo najihis numwa,nadhoofika sna nakonda Sana na kiukwel Sina raha kabisa mwenzenu...Nina urefu wa sm.176 lakin uzito mdogo sana Jana nmepimwa Nina kilo 61.

Samahani kwa maelezo marefu ya kuchosha,naomba wajuzi wa mambo wanisaidie kwa ushauri wa kiafya nifanyeje ili niwe na afya njema mwenzenu.natanguliza shukrani
 
Siyo Dengu hiyo jua kweli kapome homa ya Dangue maana hiyo siyo hospital zote wanaweza kuooma na kugundua ugonjwa
 
Elimu elimu elimu elimu.

Yani miaka 10 ukienda hospitali wanapima uti na typhoid tuu? Like seriously? Na ww umeridhika kabisa hayo ndio magonjwa yanayokusumbua?

Kama kweli ndio magonjwa yanayokusumbua, je walikubadilishia dozi ya dawa ama waliendelea kukupa zilezile?

Na je ulienda kupima hospitali tofauti tofauti au unaendaga the same hospital since then?

Ebu jaza nyama kwenye maelezo yako usaidiwe mkuu.
 
Nimekuwa nikienda hospital tofaut tofaut mkuu na Kila nikienda huwa natoa same explanation wanaanza na vipomo hivyo Kwanza then ukikutwa na maradhi wanakupa dawa afu wanakwmbia tumia ukmalza doz rudi tuangalie Kama ugonjwa umeisha....nkirud tena let say baada ya mwezi nakutwa nao wanabadili dawa natumiatena kwa usahih Ila bado after quet period tatizo linaanza Tena....unakuta Kuna wakati wanapima vipimo vyoote common hawakuti tatizo lolote but mm nakuwa najiskia mgonjwa
 
Nenda kafanye checkup hospitali kubwa hasa za serikali.

Hasahasa Muhimbili,Mloganzila,KCMC,Bugando,Benjamini Mkapa,Mbeya n.k.
 
Punguza mawazo jiamini na jitahidi uwe unawaza mambo mengine. Inawezekana huna tatizo ila unakua na tatizo kwa sababu unahisi una tatizo. Punguza mawazo. Many things do harm only because people think they are harmful.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…