Bitcoinbase
JF-Expert Member
- Jul 17, 2016
- 319
- 285
Habarini za jioni. Poleni na majukumu.
Naomba wataalamu wanisaidie kunipa mwanga juu ya hili lililonisibu.
Jioni hii nilikuwa nimeenda Kutoa pesa kwenye ATM,, baada ya kufanya transactions na kucomand withdrawal. Nikiwa nasubiri bahati mbaya ikapigwa Simu nikapokea nikasahau kuvuta pesa kwenye mashine, baadae nashtuka ndo zinaishia kurudi kwenye machine.
Na ile nikarudisha kadi tena kucheck balance Hamna ,, So naomba Kujua taratibu za kufuata ili ziweze kusoma kwenye account.. Nifanyaje, ?