Wajuzi wa sheria: Tuhuma za ubakaji na ulawiti zina dhamana?

Wajuzi wa sheria: Tuhuma za ubakaji na ulawiti zina dhamana?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Nimesoma taarifa ya kuachiliwa kwa dhamana mahakamani aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Simuyu, Yahaya Nawanda kwa tuhuma zinazomkabili za ulawiti.

Zaidi soma: Dkt. Yahaya Nawanda apandishwa Kizimbani kwa Tuhuma za Ulawiti, aachiwa kwa dhamana

Kwa wajuzi wa sheria, Tuhuma za ubakaji na ulawiti zina dhamana?

Muda mrefu nimekuwa nikisikia haya ni mojawapo ya makosa yasiyo na dhamana.

Kwa kuzingatia Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022. Kifungu Na. 148 (5)(a) kimeorodhesha makosa ambayo siyo ya dhamana yakiwemo;
  1. mauaji, uhaini, unyang'anyi wa kutumia silaha, au unajisi wa mtoto;
  2. Usafirishaji haramu wa madawa ya kulevya dhidi ya Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya;
  3. Kosa linalohusisha heroini, kokeini, opium etc;
  4. Makosa ya ugaidi kwa kuzingatia Sheria ya Kuzuia Ugaidi.
  5. Uhujumu uchumi kwa makosa kadhaa chini ya Sheria ya Utakatishaji Fedha Haramu.
  6. Usafirishaji haramu wa binadamu kwa kuzingatia Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu.

Kwa kuzingatia taarifa zilizopo ni kwamba mshtakiwa anatuhumiwa kwa kosa la kumwingilia kinyume na maumbile 'kumlawiti' kinyume na kifungu namba 154 (1) (a) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16.
Hivyo ni sahihi kwa mahakama kumuachia kwa dhamana mshtakiwa.

Sababu nyingine ambazo zinaweza kupelekea mtuhumiwa kunyimwa dhamana ni pamoja na:
  1. Sababu za usalama wa mtuhumiwa mwenyewe akirudi uraiani
  2. Endapo mtuhumiwa alishawahi pewa dhamani na akaruka masharti ya dhamana.
  3. Endapo kosa linahusu pesa au mali yenye thamani zaidi ya milioni kumi unless mtu huyo atoe dhamani ya milioni kumi au mali yenye thamni hiyo.
 
Ndiyo
Makosa yasiyo na dhamana ni mauaji, uhaini na ujambazi wa kutumia silaha
Mbona aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Tabora marehemu Ditopile Ramadhan Mwinyishehe Ukiwaona Mzuzuri aliyekuwa akituhumiwa kumuua kondakta wa daladala jijini Dar es s salaam hadi mauti yanamkuta bwana Ditopile alikuwa nje kwa dhamana haliyakuwa ana tuhuma za mauaji?!
 
Mbona aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Tabora marehemu Ditopile Ramadhan Mwinyishehe Ukiwaona Mzuzuri aliyekuwa akituhumiwa kumuua kondakta wa daladala jijini Dar es s salaam hadi mauti yanamkuta bwana Ditopile alikuwa nje kwa dhamana haliyakuwa ana tuhuma za mauaji?!
Alibadilishiwa kosa kutoka mauaji (murder) hadi kuua bila kukusudia (manslaughter)
 
Kwa kuzingatia Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022. Kifungu Na. 148 (5)(a) kimeorodhesha makosa ambayo siyo ya dhamana yakiwemo;
  1. mauaji, uhaini, unyang'anyi wa kutumia silaha, au unajisi wa mtoto;
  2. Usafirishaji haramu wa madawa ya kulevya dhidi ya Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya;
  3. Kosa linalohusisha heroini, kokeini, opium etc;
  4. Makosa ya ugaidi kwa kuzingatia Sheria ya Kuzuia Ugaidi.
  5. Uhujumu uchumi kwa makosa kadhaa chini ya Sheria ya Utakatishaji Fedha Haramu.
  6. Usafirishaji haramu wa binadamu kwa kuzingatia Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu.

Kwa kuzingatia taarifa zilizopo ni kwamba mshtakiwa anatuhumiwa kwa kosa la kumwingilia kinyume na maumbile 'kumlawiti' kinyume na kifungu namba 154 (1) (a) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16.
Hivyo ni sahihi kwa mahakama kumuachia kwa dhamana mshtakiwa.

Sababu nyingine ambazo zinaweza kupelekea mtuhumiwa kunyimwa dhamana ni pamoja na:
  1. Sababu za usalama wa mtuhumiwa mwenyewe akirudi uraiani
  2. Endapo mtuhumiwa alishawahi pewa dhamani na akaruka masharti ya dhamana.
  3. Endapo kosa linahusu pesa au mali yenye thamani zaidi ya milioni kumi unless mtu huyo atoe dhamani ya milioni kumi au mali yenye thamni hiyo.
 
Police wao wanabadilishaje kosa bila Mahakama kusema hii ni murder au ni manslaughter!?
ILE KESI HAIKUWA MURDER, DPP ALIIPELEKA MAHAKAMANI KAMA MANSLAUGHTER. MAANA WAKATI AKIWA ANATOKA NA SILAHA YAKE NYUMBANI KUSUDIO HALIKUWA KWENDA KUFANYA JINAI ( MAUAJI).
 
Back
Top Bottom