Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,278
- 797
Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Said Othman Yakub amekutana na kufanya mazungumzo na wakala rasmi wa Air Tanzania hapa Comoro ComAir waliowakilishwa na Ndugu Kamarouddine Waziri Zamane pamoja na Maafisa wa ATCL walioko Comoro Bi. Esther J Mahiga na Bw. Boudra Fahit.
Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbali mbali ya operesheni za Air Tanzania hapa Comoro na namna ubalozi kama wawakilishi rasmi wa Serikali wanavyoweza kusaidia. Pia, Balozi Yakubu alitumia fursa hiyo kuwapongeza kwa kujali wateja wa Comoro ambapo hivi sasa ATCL wanafanya safari tatu kwa wiki baina ya Dar es salaam na Moroni na ndege ya nne ya mizigo pekee inatarajiwa kuanza safari zake tarehe 13 Septemba, 2024.
Jitahada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuifungua Tanzania kibiashara ni pamoja na uwezeshaji mkubwa anaoufanya katika shirika la ATCL.
Pia soma:Watanzania Waishio Comoro Wakutana na Balozi Yakubu
Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbali mbali ya operesheni za Air Tanzania hapa Comoro na namna ubalozi kama wawakilishi rasmi wa Serikali wanavyoweza kusaidia. Pia, Balozi Yakubu alitumia fursa hiyo kuwapongeza kwa kujali wateja wa Comoro ambapo hivi sasa ATCL wanafanya safari tatu kwa wiki baina ya Dar es salaam na Moroni na ndege ya nne ya mizigo pekee inatarajiwa kuanza safari zake tarehe 13 Septemba, 2024.
Jitahada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuifungua Tanzania kibiashara ni pamoja na uwezeshaji mkubwa anaoufanya katika shirika la ATCL.
Pia soma:Watanzania Waishio Comoro Wakutana na Balozi Yakubu