Wakali wa Hisabati Part II

Miaka kumi iliyopita umri wa Salum ulikuwa 1/5 ya umri wa baba yake wakati huo.
Miaka mitano ijayo umri wa Salumu utakuwa 1/2 ya umri wa baba yake wakati huo. Tafuta umri wa Salumu wa sasa.
Karibuni wadau.
SLN
Let the age of salum be x and that of father be y

Given:
x-10=y/5 .............(i)
x+5=y/2 ..............(ii)

Solving the two eqn simultaneously
from eqn i
x=y/5+10 (substitute this eqn into eqn ii)
y/5+10+5=y/2
y/5+15=y/2
then
y/2-y/5=15
3y/10=15
y=150/3
y=50
now from x=y/5+10
x=50/5+10
x=20

Therefore currently salum is 20 years and his father is 50 years
 
Chukulia umri wa Salum wa sasa kama S
Chukulia umri wa Baba wa sasa kama B.
Miaka 10 iliyopita umri wa Salum ulikuwa S-10 na wa baba yake ulikuwa B-10.
Miaka 10 iliyopita umri wa Salum ulikuwa 1/5 ya umri wa baba yake,hii ni sawa na kusema S-10=(B-10)/5 ..............(i)
Miaka 5 ijayo umri wa Salum utakuwa S+5 na umri wa baba yake utakuwa B+5
Miaka mitano ijayo umri wa Salum utakuwa 1/2 ya baba yake,hii ni sawa na kusema S+5=(B+5)/2 ...............(ii)
Sasa kokotoa milinganyo (i) na (ii)
5x(i) ni 5(S-10)=5S-50=B-10 .......(iii)
2x(ii) ni 2(S+5)=2S+10=B+5 ........(iv)
(iii)-(iv) ni
3S-60=-15
3S=-15+60
3S=45
S=15
Umri wa Salum wa sasa ni miaka 15.
 
Maswali ya Primary tulikuw tunachukua point tatu za muhimu za kukamata watoto^^………
 
source ya swali ni (Msemwa, P.B. Mitihani 12 ya Hisabati kwa darasa la 5, 6 na 7, Taaluma Publishers, mtihani wa 7, swali la 48, uk 21.

Huyu jamaa P.B Msemwa vitabu vyake vizuri sana.Watu wanasema vigumu,hasa kile cha CSBM form 3&4.Binafsi maswali magumu katika hiki kitabu ni PROBABILITY,APPLICATIONS OF VECTORS na THE EARTH AS SPHERES
 

Mkuu Kibishi pokea salute zote.
Ahsante sana.
Ubarikiwe sana
 
Last edited by a moderator:

ahsante sana mkuu bahati30.
Pamoja katika kupanua bongo.
 
Last edited by a moderator:
Mbona Swali rahisi LA darasa LA nane? Saumu ana Miaka 15 na babake ana miaka 35.

miaka kumi iliyopita, saumu alikuwa na miaka 5 na babake 25. hiyo ni 1/5

miaka tano ijayo, saumu atakuwa na miaka 20 na babake miaka 40. Hiyo ni 1/2
 
MIAKA 10 ILIYOPITA
baba=x ,Salum=x/5

HALI YA SASA
Baba=x+10, Salum=x/5+10

MIAKA 5 IJAYO

Baba=x+10+5 ,Salum=x/5+10+5

MLINGANYO(EQUATION)
Salum=(1/2)(Baba)
x/5+10+5=(1/2)(x+10+5)
x/5+15=(1/2)(x+15)

Mungu akiwa upande wako unapata x=25

UMRI WA SALUM SASA=x/5+10=25/5+10
unapata miaka 15
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…