Wakamaria (gamblers) ni miongoni mwa watu wasio na furaha hapa duniani.

Wakamaria (gamblers) ni miongoni mwa watu wasio na furaha hapa duniani.

Tipstipstor

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2021
Posts
1,528
Reaction score
3,352
Ahlan wa sahlan

Wakamaria aka (gamblers) ,ni miongoni mwa watu wasio na furaha hapa ulimwenguni. Mwanadam ameumbwa akiwa na sifa ya kupenda umiliki na anachukia sana kitu ambacho amekimiliki kikimtoka.

Uchezaji wa kamari ni jambo ambalo limeharibu maisha ya watu wengi sana hapa duniani.Kamari imepelekea matajiri kufilisika, biashara kuharibika, mitaji kupotea na mbaya zaidi ni uharibifu wa familia nikimaanisha mchezaji kamari na watu wake wa karibu wanaomzunguka.

Watu wengi sana wanaocheza kamari huwa wanaficha uhalisia wa tatizo walilonalo yaani Uraibu wa kamari ( gambling addiction) , ni ngumu sana kumtambua mraibu wa kamari (gambling addict) kwasababu hakuna ishara yoyote ya nje ambayo inamuonesha kuwa huyu mtu ni mraibu wa kamari. Tofauti na uraibu mwingine ,kama ulevi wa pombe, ulevi wa madawa ya kulevya n.k

Kwavile hakuna ishara yoyote ambayo mtu anaweza kumtambua mkamaria, wakamaria wengi hulificha tatizo hili kiasi kwamba hata mke wake anaelala nae kitanda kimoja hawezi kujua kuwa mumewe ni mraibu wa kamari.

Binadamu anachukia sana kupoteza, iwe pesa,nyumba,mke,watoto n.k hakuna nwanadamu atakaesema kuwa anapata furaha pindi anapopoteza. Mraibu wa kamari huwa anapitia nyakati ngumu sana za msongo wa mawazo, mood swings...yaani kuna muda akishinda anajihisi afadhali na muda mwingi anapopoteza hali yake huwa ni mbaya sana. Huwa hana furaha kabisa na anatamani kuwa ifike siku aachane na uchezaji wa kamari ila kuna nguvu inamrudisha ikimpa matumaini mapya kuwa anaweza kurudisha kile alichopoteza na hapa ndipo anapoendelea kupoteza.

Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kuwa tujiepushe sana na uchezaji wa kamari. Kamari imeharibu maisha ya wagu wengi sana hapa duniani na kuna takwimu zinazoonesha kuwa kila dakika moja kuna mtu anajiua kutokana na uraibu wa kucheza kamari.
 
Labda ni wewe tu mkuu! Mbona mimi ni punter na nina furaha kabisa! Inategemeana kama unaweka 500 kila siku kuitafuta m25 furaha itoke wapi?
You are living in denial ila deep down unajua uhalisia ulivyo.Hakuna mwanadamu anafurahia kupoteza na kamari ni mchezo wa kupoteza.
 
Mtoa mada hivi kati ya mapenzi na kamari kipi kinatia stress
 
You are living in denial ila deep down unajua uhalisia ulivyo.Hakuna mwanadamu anafurahia kupoteza na kamari ni mchezo wa kupoteza.
Mkuu inaonesha gambling ilikufanya vibaya sana maana naona similar thread huku chini zimejaa zako tu, unalalamika hadi kupigwa laki 6 kwa siku 30.
Inaonesha uliwekeza sana kwenye kamari.

Raha ya kamari (hasa betting ya mpira) uwe na kazi yako kabisa halali ya kukuingizia kipato. Kisha unatenga kiasi kidogo ambacho hata ukipoteza hakitakuathiri wewe au wanaokutegemea.

Kisha unatandika majamvi yako bila kimuhemuhe, nakuhakikishia hutakuja kulalamika hapa.

Shida inakuja pale mtu anapobetia hela ya kula yeye mwenyewe ya nauli ya watoto asubuhi, yaani anataka aidabo ili wapate wote. Matokeo yake mhindi anawatwanga halafu watoto wake ndio wanaenda shule kwa school bus.
 
K
Mkuu inaonesha gambling ilikufanya vibaya sana maana naona similar thread huku chini zimejaa zako tu, unalalamika hadi kupigwa laki 6 kwa siku 30.
Inaonesha uliwekeza sana kwenye kamari.

Raha ya kamari (hasa betting ya mpira) uwe na kazi yako kabisa halali ya kukuingizia kipato. Kisha unatenga kiasi kidogo ambacho hata ukipoteza hakitakuathiri wewe au wanaokutegemea.

Kisha unatandika majamvi yako bila kimuhemuhe, nakuhakikishia hutakuja kulalamika hapa.

Shida inakuja pale mtu anapobetia hela ya kula yeye mwenyewe ya nauli ya watoto asubuhi, yaani anataka aidabo ili wapate wote. Matokeo yake mhindi anawatwanga halafu watoto wake ndio wanaenda shule kwa school bus.
Kwa mawazo yako kila anaeongea kuipinga kamari basi ana shida?
 
Nasapoti mawazo ya mtoa mada .
Shukrani, hata wazungu walikaa kimya wakati huu uovu unaanzishwa kwenye mataifa yao ila sasa hv wanajuta sana kwann hawakukatazan mapema. Uraibu wa kamari umekuwa ni janga.

Takwimu zinasema mraibu wa kamari ana asilimia kubwa ya ku-commit suicide kuliko waraibu wa vilevi vingine.
 



sikilizeni hiki kisa cha aliyekuwa major katika jeshi la uingereza jinsi kamari ilivyomuharibia maisha yake
 
Naunga mkonyo hoja.

Usisikie makampuni ya betting wamelipa kodi mabilioni ya shilingi,ni watu hao wamechezea vipigo. Wakiwemo waajiriwa.

Mtu akiliwa nusu ya mshahara ndio akili inamrudia.
 
Naunga mkonyo hoja.

Usisikie makampuni ya betting wamelipa kodi mabilioni ya shilingi,ni watu hao wamechezea vipigo. Wakiwemo waajiriwa.

Mtu akiliwa nusu ya mshahara ndio akili inamrudia.
Bado akili haimrudii cuz anakuwa na hasira ya kupoteza na tamaa ya kurudisha pesa zake so anaendelea kupambana ktk system ile ile ili arudishe pesa zake matokeo yake anazidi kupotezwa na ugonjwa wa uraibu wa kamari unaendelea kumtawala
 
Nilishakutana na jamaa anahuzunika sana na kumlaumu mtu aliyemfundisha kubeti, jamaa anasema kuwa hawezi kukaa hata na sh 10000 mfukoni, pesa ikiingia tu anawaza aende kubeti. Mbaya zaidi yupo tayari hata kuweka bond vitu vyake vya thamani ili abeti.


Huu ni ugonjwa ndugu zangu na si hali ya kawaida kwa mwanadamu
 
Huu ni ubongo wa MKAMARIA (gambler) unavyokuwa pindi anabeti

 
Ahlan wa sahlan

Wakamaria aka (gamblers) ,ni miongoni mwa watu wasio na furaha hapa ulimwenguni. Mwanadam ameumbwa akiwa na sifa ya kupenda umiliki na anachukia sana kitu ambacho amekimiliki kikimtoka.

Uchezaji wa kamari ni jambo ambalo limeharibu maisha ya watu wengi sana hapa duniani.Kamari imepelekea matajiri kufilisika, biashara kuharibika, mitaji kupotea na mbaya zaidi ni uharibifu wa familia nikimaanisha mchezaji kamari na watu wake wa karibu wanaomzunguka.

Watu wengi sana wanaocheza kamari huwa wanaficha uhalisia wa tatizo walilonalo yaani Uraibu wa kamari ( gambling addiction) , ni ngumu sana kumtambua mraibu wa kamari (gambling addict) kwasababu hakuna ishara yoyote ya nje ambayo inamuonesha kuwa huyu mtu ni mraibu wa kamari. Tofauti na uraibu mwingine ,kama ulevi wa pombe, ulevi wa madawa ya kulevya n.k

Kwavile hakuna ishara yoyote ambayo mtu anaweza kumtambua mkamaria, wakamaria wengi hulificha tatizo hili kiasi kwamba hata mke wake anaelala nae kitanda kimoja hawezi kujua kuwa mumewe ni mraibu wa kamari.

Binadamu anachukia sana kupoteza, iwe pesa,nyumba,mke,watoto n.k hakuna nwanadamu atakaesema kuwa anapata furaha pindi anapopoteza. Mraibu wa kamari huwa anapitia nyakati ngumu sana za msongo wa mawazo, mood swings...yaani kuna muda akishinda anajihisi afadhali na muda mwingi anapopoteza hali yake huwa ni mbaya sana. Huwa hana furaha kabisa na anatamani kuwa ifike siku aachane na uchezaji wa kamari ila kuna nguvu inamrudisha ikimpa matumaini mapya kuwa anaweza kurudisha kile alichopoteza na hapa ndipo anapoendelea kupoteza.

Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kuwa tujiepushe sana na uchezaji wa kamari. Kamari imeharibu maisha ya wagu wengi sana hapa duniani na kuna takwimu zinazoonesha kuwa kila dakika moja kuna mtu anajiua kutokana na uraibu wa kucheza kamari.
Hatuna hisia, tuna furaha na kinyume chake hivyo ni vitu viwili tofauti kabisa usichanganye.
 
Back
Top Bottom