Wakamatwa wakijifanya wauza madini

Wakamatwa wakijifanya wauza madini

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Watu wawili wanaoshukiwa kuwa ni matapeli wamekamatwa katika Taasisi ya Saratani Ocean Road walipokuwa wakijaribu kumtapeli moja ya kati ya ndugu wa wagonjwa hospitalini hapo.

Akisimulia kuhusu kisa hicho, mwanamke huyo ambaye jina lake limehifadhiwa amesema watu hao ambao majina yao ni Bakari Rajabu na Twaha walijifanya kuwa ni wachimbaji wadogo wa madini na kutaka kuoneshwa mahali linapopatikana duka la kuuzia madini hayo ya dhahabu.

Hata hivyo, baada ya kushtukiwa njama zao walitaka kutoroka ndipo alipotoa taarifa kwa askari wa usalama wa taasisi hiyo na watu hao kukamatwa.

Kwa upande wa watuhumiwa wamekiri kufanya tukio hilo wakijitetea kuwa pilika pilika za maisha ndizo zimefanya kujaribu kufanya utapeli huo.
 
Back
Top Bottom