Wakati EAC inavunjika, nani alipata nini?

Wakati EAC inavunjika, nani alipata nini?

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Nasikia hii ilivunjika mwaka 1977. Nimekuwa nikisikia hadithi nyingi kuwa watu waligawana mali kama washenzi(barbarians). Hili limewapa baadhi ya watu vinyongo hadi leo kuwa walidhulumiwa, naomba kujua kwenye kugawana huko, Uganda alipata nini, Kenya alipata nini na Tanzania alipata nini?

Ufafanuzi uliyotolewa na Wadau
(1)Azimio la Arusha halikuwa na athari kubwa katika uchumi wa Tanzania kabla ya EAC kuvunjika na nchi kuingia vitani. Mashirika mengi yaliyoundwa kumiliki mali zilizokuwa zimetaifishwa yalikuwa yakifanya vizuri sana; hiyo ni pamoja na STC, TCC, NDC, NMC, Mamlaka ya Mkonge, Mamlaka ya Tumbaku, mamlaka ya Pamba, etc. Athari za umiliki huo zilianza wakati wa vita baada ya uhaba wa bidhaa kutokea na kusababisha rushwa pamoja "bei za kuruka" kuanza. Ni wakati huo ambapo faida za kuwa na biashara binafsi zilianza kuonekana!

(2) Operation vijiji ilikuwa mwaka 1972-1973 hivi nikiwa primary school. Hii ilisababisha njaa kubwa sana mwaka 1974 na kuifanya serikali ipitishe sera ya Siasa ni Kilimo ili kuhamamasisha kilimo tena; njaa ile ndiyo iliyoleta mahindi ya yanga. Kufuatana na Siasa ni kilimo, mwaka 1976 nchi ilikuwa na chakula cha kutosha sana na khali ya kilimo cha mazo mbalimbali ilirudi katika msingi wake kabla ya mwaka 1973; kwa hiyo wakati EAC inavunjika mwaka 1977, Tanzania haikuwa na matatizo ya kilimo tena.

(3) Kuvunjika kwa EAC kuliathiri sana usafiri Tanzania kwa kiasi cha kutosha kuathiri uchumi. Usafiri wa ndege ulikufa kabisa kwa vile ndege zote zifungiwa Kenya kasoro ile iliyotorosha na kapteni mapunda. Usafiri wa meli kwenye ziwa Victoria ulikufa kabisa, ikabidi serikali inunue MV Butiama na MV Bukoba katika mazingira ambayo hayakuwa mipango ya serikali wakati huo, na usafiri wa reli pia uliathiriwa sana kwa vile karakana kuu ya reli ilikuwa Nairobi na mabehewa pamoja na vichwa vyote vilivyokuwa kwenye matengezo havikurudi, na mwisho hata usafiri wa barabara ulithirika sana kwa vile mabasi mengi ya masafa marefu wakati huo yalikuwa ya EAR yakisaidiwa na yale ya DMT
 
Nasikia hii ilivunjika mwaka 1977. Nimekuwa nikisikia hadithi nyingi kuwa watu waligawana mali kama washenzi(barbarians). Hili limewapa baadhi ya watu vinyongo hadi leo kuwa walidhulumiwa, naomba kujua kwenye kugawana huko, Uganda alipata nini, Kenya alipata nini na Tanzania alipata nini?

Kenya ndyo ilipata vingi
 
Nasikia hii ilivunjika mwaka 1977. Nimekuwa nikisikia hadithi nyingi kuwa watu waligawana mali kama washenzi(barbarians). Hili limewapa baadhi ya watu vinyongo hadi leo kuwa walidhulumiwa, naomba kujua kwenye kugawana huko, Uganda alipata nini, Kenya alipata nini na Tanzania alipata nini?
Kwa Kuanzia Shirika la Ndege La KQ Nimali ya EAC
Walibadili Jina Tu
 
Baada ya EAC kuvunjika nchi wanachama zilimteua, Dr.Victor Umbricht, raia wa Uswizi, kuwa msuluhishi wa kugawa mali na madeni ya jumuiya.

Kwa msingi huo, siyo sahihi kusema kwa nchi fulani ilidhulumiwa, au kuwa na chuki na nchi fulani kwamba imeiba mali za jumuiya.

Kwa upande mwingine, serikali ya Tanzania ilipewa fedha za pensheni za watumishi waliokuwa wakifanya kazi ktk taasisi mbalimbali za jumuiya. kwa bahati mbaya serikali ilizipangia fedha hizo matumizi mengine na kusababisha malalamiko na mgogoro mkubwa wa "wastaafu wa jumuiya ya afrika mashariki."

cc Nguruvi3, Mohamed Said
 
Baada ya EAC kuvunjika nchi wanachama zilimteua, Dr.Victor Umbricht, raia wa Uswizi, kuwa msuluhishi wa kugawa mali na madeni ya jumuiya.

Kwa msingi huo, siyo sahihi kusema kwa nchi fulani ilidhulumiwa, au kuwa na chuki na nchi fulani kwamba imeiba mali za jumuiya.

Kwa upande mwingine, serikali ya Tanzania ilipewa fedha za pensheni za watumishi waliokuwa wakifanya kazi ktk taasisi mbalimbali za jumuiya. kwa bahati mbaya serikali ilizipangia fedha hizo matumizi mengine na kusababisha malalamiko na mgogoro mkubwa wa "wastaafu wa jumuiya ya afrika mashariki."


cc Nguruvi3, Mohamed Said
Na wale wazee mpaka wamekufa wamedhulumiwa hela zako

Nakumbuka kuna kipind walikua wanaandamana sana hapo mjini enzi za Gewe/Tibaigana.

Saivi naona walishakata tamaa
 
..baada ya EAC kuvunjika nchi wanachama zilimteua, Dr.Victor Umbricht, raia wa Uswizi, kuwa msuluhishi wa kugawa mali na madeni ya jumuiya.

..kwa msingi huo, siyo sahihi kusema kwa nchi fulani ilidhulumiwa, au kuwa na chuki na nchi fulani kwamba imeiba mali za jumuiya.

..kwa upande mwingine, serikali ya Tanzania ilipewa fedha za pensheni za watumishi waliokuwa wakifanya kazi ktk taasisi mbalimbali za jumuiya. kwa bahati mbaya serikali ilizipangia fedha hizo matumizi mengine na kusababisha malalamiko na mgogoro mkubwa wa "wastaafu wa jumuiya ya afrika mashariki."

cc Nguruvi3, Mohamed Said
Shukrani sana mkuu. Kwahiyo kusema kuwa Kenya walifaidika au kuwa kuna Rubani alitorosha ndege na kutufaidisha si sahihi, wala kumbe hatukugawan mali kama washenzi, bali kwa utaratibu na usawa. Umenitoa tongotongo. Na hii ishu ya wastaafu wa EAC serikali kwakweli inapaswa kuwajibika na kuomba radhi.
 
Shukrani sana mkuu. Kwahiyo kusema kuwa Kenya walifaidika au kuwa kuna Rubani alitorosha ndege na kutufaidisha si sahihi, wala kumbe hatukugawan mali kama washenzi, bali kwa utaratibu na usawa. Umenitoa tongotongo. Na hii ishu ya wastaafu wa EAC serikali kwakweli inapaswa kuwajibika na kuomba radhi.

Kulikuwa na crisis baada ya jumuiya kuvunjika, na ktk crisis hiyo ndiyo unasikia habari za rubani kutoroka na ndege. pia nimewahi kusikia habari ya mpaka wa Tz na Kny kufungwa, etc etc.

Lingine unalopaswa kukumbuka ni kwamba kila nchi mwanachama ilikuwa ina-host taasisi za Jumuiya kama vile bandari, reli, posta, shirika la ndege, pamoja na mali na miundombinu ya taasisi hizo. Kwa hiyo kila nchi ilirithi taasisi za jumuiya na kuzifanya za kitaifa.

Vilevile kulikuwa na wafanyakazi wa Jumuiya. Wako waTz walikuwa wakifanya kazi Kenya, au Uganda, na pia walikuwepo raia toka nchi majirani waliokuwa wakifanya kazi Tz. kutokana hali hiyo ilibidi kila nchi ichukue raia wake na kuwarejesha nyumbani.

Lakini baada ya hapo nchi wanachama zilimteua Dr.Victor Umbricht ambaye alifanya kazi kubwa ya kuhakikisha mali na madeni ya jumuiya yanagawanywa kwa haki. Binafsi sijasikia popote pale serikali yetu ikilalamikia utendaji na kazi iliyofanywa na Dr.Umbricht.

Kuhusu nchi gani iliumia zaidi, nadhani ilitegemea nchi husika ilikuwa imara kiasi gani wakati wa kuanzishwa kwa jumuiya. Kama nchi A ilikuwa na uchumi mdogo kuliko nchi B wakati wa kuanzisha jumuiya basi hali ilikuwa hivyohivyo wakati jumuiya inavunjika.
 
..lingine unalopaswa kukumbuka ni kwamba kila nchi mwanachama ilikuwa ina-host taasisi za Jumuiya kama vile bandari, reli, posta, shirika la ndege, pamoja na mali na miundombinu ya taasisi hizo. Kwa hiyo kila nchi iliridhi taasisi za jumuiya na kuzifanya za kitaifa.
Kwanza, ahsante Joka, Dr Victor Umbricht aliteuliwa kuwa msuluhishi wa mali na madeni ya EAC ( assets and liabilities). Kwa Tanzania AICC ilikuwa ndio makao makuu ya EAC ikijulikana kama Community centre
Hii meli ya MV Victoria ilikuwa ya EAC, Tanzania wakapewa. Kenya na Uganda nao wali host taasisi kadha
..Lakini baada ya hapo nchi wanachama zilimteua Dr.Victor Umbricht ambaye alifanya kazi kubwa ya kuhakikisha mali na madeni ya jumuiya yanagawanywa kwa haki. Binafsi sijasikia popote pale serikali yetu ikilalamika utendaji na kazi iliyofanywa na Dr.Umbricht.
The late Dr Umbricht alifanya kazi kubwa kiasi kwamba kila nchi iliridhika na baada ya hapo hapakuwepo na kinyongo cha wanachama. Hilo lilisaidia sana akina Mkapa, Moi na Museveni kuanzisha upya hii iliyopo

Kuhusu wafanyakazi, ile ilikuwa dhulma kubwa sana waliofanyiwa. Pesa zilitolewa kwa malipo yao zikaelekezwa kwingine na kuwaacha wakiteseka. Wengi walifariki bila kupata mafao yao.

Mkapa aliamua kuanza kuwalipa kwasababu EAC ikifa alikuwepo serikali na alijua dhulma iliyofanyika.
Hili kwakweli ni moja ya mambo ambayo Mwl Nyerere aliwafanyia wafanyakazi ukatili! yes ukatili.
 
Sina uhakika kati ya Azimio la Arusha na kuvunjika kwa EAC tukio lipi lilikuwa na athari kubwa zaidi kwa uchumi wetu.

Katika kusoma-soma kwangu nimekutana na taarifa kwamba Azimio la Arusha ambalo lilileta operation vijiji na utaifishaji mali binafsi lilisababisha kilimo cha mazao ya mkonge na korosho kuanguka.

Tunaambiwa kwamba kuvunjika kwa EAC kulituathiri kiuchumi, lakini sidhani kama zipo taarifa za kutosha kuhusu athari hizo na ukubwa au madhara yake kwa uchumi wa Tz.
 
Baada ya EAC kuvunjika nchi wanachama zilimteua, Dr.Victor Umbricht, raia wa Uswizi, kuwa msuluhishi wa kugawa mali na madeni ya jumuiya.

Kwa msingi huo, siyo sahihi kusema kwa nchi fulani ilidhulumiwa, au kuwa na chuki na nchi fulani kwamba imeiba mali za jumuiya.

Kwa upande mwingine, serikali ya Tanzania ilipewa fedha za pensheni za watumishi waliokuwa wakifanya kazi ktk taasisi mbalimbali za jumuiya. kwa bahati mbaya serikali ilizipangia fedha hizo matumizi mengine na kusababisha malalamiko na mgogoro mkubwa wa "wastaafu wa jumuiya ya afrika mashariki."

cc Nguruvi3, Mohamed Said
Ule mgawanyo wa Umbritch haukuwa fair, ila nchi zililazamika kukubaliana ili mambo yaishe hasa kwa vile wakati huo Tanzania na Uganda zilikuwa zimetoka vitani; alifanya kazi ya usuluhishi kwa karibu miaka kumi akamaliza mwaka 1982 baada ya vita.

Ukisoma mahojiano yake hapa kwenye ukurasa wa 10 utaona kuwa hakukuwa na consensus kabisa kuhusu mgawanyo huo ambapo Kenya ilipata zaidi ya Tanzania wakati Uganda ndiyo iliyoonewa zaidi. Anasema mgawanyo wake ulifuata indicators za IMF, ambazo wakati huo zilikuwa zinaipendelea sana Kenya politically wakati huo kwa kuwa na uchumi ambao ni "market oriented"..
 

Attachments

Sina uhakika kati ya Azimio la Arusha na kuvunjika kwa EAC tukio lipi lilikuwa na athari kubwa zaidi kwa uchumi wetu.

Katika kusoma-soma kwangu nimekutana na taarifa kwamba Azimio la Arusha ambalo lilileta operation vijiji na utaifishaji mali binafsi lilisababisha kilimo cha mazao ya mkonge na korosho kuanguka.

Tunaambiwa kwamba kuvunjika kwa EAC kulituathiri kiuchumi, lakini sidhani kama zipo taarifa za kutosha kuhusu athari hizo na ukubwa au madhara yake kwa uchumi wa Tz.
(1)Azimio la Arusha halikuwa na athari kubwa katika uchumi wa Tanzania kabla ya EAC kuvunjika na nchi kuingia vitani. Mashirika mengi yaliyoundwa kumiliki mali zilizokuwa zimetaifishwa yalikuwa yakifanya vizuri sana; hiyo ni pamoja na STC, TCC, NDC, NMC, Mamlaka ya Mkonge, Mamlaka ya Tumbaku, mamlaka ya Pamba, etc. Athari za umiliki huo zilianza wakati wa vita baada ya uhaba wa bidhaa kutokea na kusababisha rushwa pamoja "bei za kuruka" kuanza. Ni wakati huo ambapo faida za kuwa na biashara binafsi zilianza kuonekana!

(2) Operation vijiji ilikuwa mwaka 1972-1973 hivi nikiwa primary school. Hii ilisababisha njaa kubwa sana mwaka 1974 na kuifanya serikali ipitishe sera ya Siasa ni Kilimo ili kuhamamasisha kilimo tena; njaa ile ndiyo iliyoleta mahindi ya yanga. Kufuatana na Siasa ni kilimo, mwaka 1976 nchi ilikuwa na chakula cha kutosha sana na khali ya kilimo cha mazo mbalimbali ilirudi katika msingi wake kabla ya mwaka 1973; kwa hiyo wakati EAC inavunjika mwaka 1977, Tanzania haikuwa na matatizo ya kilimo tena.

(3) Kuvunjika kwa EAC kuliathiri sana usafiri Tanzania kwa kiasi cha kutosha kuathiri uchumi. Usafiri wa ndege ulikufa kabisa kwa vile ndege zote zifungiwa Kenya kasoro ile iliyotorosha na kapteni mapunda. Usafiri wa meli kwenye ziwa Victoria ulikufa kabisa, ikabidi serikali inunue MV Butiama na MV Bukoba katika mazingira ambayo hayakuwa mipango ya serikali wakati huo, na usafiri wa reli pia uliathiriwa sana kwa vile karakana kuu ya reli ilikuwa Nairobi na mabehewa pamoja na vichwa vyote vilivyokuwa kwenye matengezo havikurudi, na mwisho hata usafiri wa barabara ulithirika sana kwa vile mabasi mengi ya masafa marefu wakati huo yalikuwa ya EAR yakisaidiwa na yale ya DMT
 
Ule mgawanyo wa Umbritch haukuwa fair, ila nchi zililazamika kukubaliana ili mambo yaishe hasa kwa vile wakati huo Tanzania na Uganda zilikuwa zimetoka vitani; alifanya kazi ya usuluhishi kwa karibu miaka kumi akamaliza mwaka 1982 baada ya vita. Ukisoma mahojiano yake hapa kwenye ukurasa wa 10 utaona kuwa hakukuwa na consensus kabisa kuhusu mgawanyo huo ambapo Kenya ilipata zaidi ya Tanzania wakati Uganda ndiyo iliyoonewa zaidi. Anasema mgawanyo wake ulifuata indicators za IMF, ambazo wakati huo zilikuwa zinaipendelea sana Kenya politically wakati huo kwa kuwa na uchumi ambao ni "market oriented"..

Nimesoma mahojiano ya Dr.Umbricht, lakini nadhani hujaelewa alichokisema, au alichomaanisha.

Of course wakati wa mchakato nchi zote zilikuwa na malalamiko ktk masuala mbalimbali, lakini Dr.Umbricht alitoa nafasi kwa nchi yenye malalamiko kuteua wataalamu watakaochunguza malalamiko yao na kupeleka mapendekezo kwa timu ya usuluhisho.

Na Dr. Umbricht amesema mara nyingi wataalamu walioteuliwa na nchi washirika waliounga mkono mapendekezo ya wataalamu walioteuliwa na msuluhishi[umbricht].
 
(1)Azimio la Arusha halikuwa na athari kubwa katika uchumi wa Tanzania kabla ya EAC kuvunjika na nchi kuingia vitani. Mashirika mengi yaliyoundwa kumiliki mali zilizokuwa zimetaifishwa yalikuwa yakifanya vizuri sana; hiyo ni pamoja na STC, TCC, NDC, NMC, Mamlaka ya Mkonge, Mamlaka ya Tumbaku, mamlaka ya Pamba, etc. Athari za umiliki huo zilianza wakati wa vita baada ya uhaba wa bidhaa kutokea na kusababisha rushwa pamoja "bei za kuruka" kuanza. Ni wakati huo ambapo faida za kuwa na biashara binafsi zilianza kuonekana!

(2) Operation vijiji ilikuwa mwaka 1972-1973 hivi nikiwa primary school. Hii ilisababisha njaa kubwa sana mwaka 1974 na kuifanya serikali ipitishe sera ya Siasa ni Kilimo ili kuhamamasisha kilimo tena; njaa ile ndiyo iliyoleta mahindi ya yanga. Kufuatana na Siasa ni kilimo, mwaka 1976 nchi ilikuwa na chakula cha kutosha sana na khali ya kilimo cha mazo mbalimbali ilirudi katika msingi wake kabla ya mwaka 1973; kwa hiyo wakati EAC inavunjika mwaka 1977, Tanzania haikuwa na matatizo ya kilimo tena.

(3) Kuvunjika kwa EAC kuliathiri sana usafiri Tanzania kwa kiasi cha kutosha kuathiri uchumi. Usafiri wa ndege ulikufa kabisa kwa vile ndege zote zifungiwa Kenya kasoro ile iliyotorosha na kapteni mapunda. Usafiri wa meli kwenye ziwa Victoria ulikufa kabisa, ikabidi serikali inunue MV Butiama na MV Bukoba katika mazingira ambayo hayakuwa mipango ya serikali wakati huo, na usafiri wa reli pia uliathiriwa sana kwa vile karakana kuu ya reli ilikuwa Nairobi na mabehewa pamoja na vichwa vyote vilivyokuwa kwenye matengezo havikurudi, na mwisho hata usafiri wa barabara ulithirika sana kwa vile mabasi mengi ya masafa marefu wakati huo yalikuwa ya EAR yakisaidiwa na yale ya DMT
Tulishindwa kuendesha makampuni mengi yaliyotaifishwa wakati wa azimio. Shirika kama NMC liliendeshwa vibaya na lilipokuja kubinafsishwa lilikuwa hoi bin taabani. Mamlaka za mazao mbalimbali nazo hazikuwa na ufanisi kama ule wa vyama vya ushirika. Na tulipogundua tumekosea na kurudia ushirika tukajikuta tumeshapoteza watendaji waliokuwa na ujuzi wa kuendesha vyama vya ushirika. Azimio la Arusha lilikuwa baya sana kwa upande wa uchumi. Uzuri wa azimio upo ktk masuala ya maadili ya viongozi.

Dr. Umbricht anasema timu yake ilitafuta mali / assets zote za zilizokuwa taasisi za East African Community na kuzigawa kwa namna ambayo nchi zote ziliridhika. Anasema alitafuta siyo mali kubwa-kubwa kama ndege, na mabehewa ya treni, bali alitafuta na kuhakiki mpaka mali ndogo kama typewriter!!

Kuhusu ndege, ni kweli Kenya walifanya hujuma wakachukua ndege 14 kati ya 17. Tanzania tulichukua ndege 3, na Uganda hakupata ndege yoyote. Pamoja na hayo, nchi zote zilipata haki yao wakati wa mgawanyo wa mali na madeni ya EAC.
 
..Tulishindwa kuendesha makampuni mengi yaliyotaifishwa wakati wa azimio. Shirika kama NMC liliendeshwa vibaya na lilipokuja kubinafsishwa lilikuwa hoi bin taabani. Mamlaka za mazao mbalimbali nazo hazikuwa na ufanisi kama ule wa vyama vya ushirika. Na tulipogundua tumekosea na kurudia ushirika tukajikuta tumeshapoteza watendaji waliokuwa na ujuzi wa kuendesha vyama vya ushirika. Azimio la Arusha lilikuwa baya sana kwa upande wa uchumi. Uzuri wa azimio upo ktk masuala ya maadili ya viongozi.

..Dr.Umbricht anasema timu yake ilitafuta mali / assets zote za zilizokuwa taasisi za East African Community na kuzigawa kwa namna ambayo nchi zote ziliridhika. Anasema alitafuta siyo mali kubwa-kubwa kama ndege, na mabehewa ya treni, bali alitafuta na kuhakiki mpaka mali ndogo kama typewriter!!

..Kuhusu ndege, ni kweli Kenya walifanya hujuma wakachukua ndege 14 kati ya 17. Tanzania tulichukua ndege 3, na Uganda hakupata ndege yoyote. Pamoja na hayo, nchi zote zilipata haki yao wakati wa mgawanyo wa mali na madeni ya EAC.
(1) Mashirika ya Umma yalikuwa yanafanya vizuri sana kabla ya vita; ni baada ya vita ndipo yalipoanza kudorora na rushwa kushamiri. Ile vita ya uhujumi uchumi ya mwaka 1982 ilitokana na uhaba wa bidhaa baada ya vita, ambapo ndipo falsafa ya "utakula kwenye meza yako" ilipoanza, na kusababisha mashirika yote ya umma yasifanye kazi kwa faida tena bali kila mfanyakazi akawa anaenda kazini ama kuiba mali za umma, au kutegemea kuomba rushwa kutoka kwa wateja.

(2) Hata kama kulikuwa na uhakiki mzuri wa mali za jumuia, ugawanyaji wake ulifuata vigezo ambavyo viliipendelea sana Kenya, yaani mali zile hazikugawanya sawasawa miongoni mwa wanachama kuwa kila mwanachama apate 1/3! haya yeye katika mahojiano hayo anaonyesha kuwa kulikuwa na vipengele ambavyo havikuwa controversial vilikubaliwa na nchi zote lakini kuna vipengele ambavyo havikukubaliwa.
 
..Nimesoma mahojiano ya Dr.Umbricht, lakini nadhani hujaelewa alichokisema, au alichomaanisha.

..Of course wakati wa mchakato nchi zote zilikuwa na malalamiko ktk masuala mbalimbali, lakini Dr.Umbricht alitoa nafasi kwa nchi yenye malalamiko kuteua wataalamu watakaochunguza malalamiko yao na kupeleka mapendekezo kwa timu ya usuluhisho.

..Na Dr.Umbricht amesema mara nyingi wataalamu walioteuliwa na nchi washirika waliounga mkono mapendekezo ya wataalamu walioteuliwa na msuluhishi[umbricht].
Kuna vipande nchi zilikubaliana na mgawanyo na kuna vipande hazikukubaliana kabisa. Ule mgawanyo uliofuata geographic location ya assets uliiependelea sana Kenya kwa vile ndiko assets nyingi zilikuwa; halafu ule mgawanyo uliofuata equality nao ulikuwa na vipengele vilivyoipendelea sana Kenya kutoka na ile ya geographic location ya assets.

Hili lililalamikiwa sana na wachumi wa Tanzania wakati huo lakini wakaamua kuliacha kwa vile Tanzania wakati huo tulikuwa kwenye majadiliano na IMF na World bank ambao walikuwa nyuma ya pazia la makubaliano yale. Hakuna mchumi wa Tanzania aliyekubaliana na mgawanyo ule; mwulize mzee Mtei hapa ambaye ndiye aliyekuwa waziri wa fedha wakati huo kama kweli tulikubaliana na mgawanyo ule kwa roho nyeupe.
 
Kuna vipande nchi zilikubaliana na mgawanyo na kuna vipande hazikukubaliana kabisa. Ule mgawanyo uliofuata geographic location ya assessts uliiependelea sana Kenya kwa vile ndiko assessts nyingi zilikuwa; halafu ule mgawanyo uliofuata equality nao ulikuwa na vipengele vilivyoipendelea sana Kenya kutoka na ile ya geographic location ya assets. Hili lililalamikiwa sana na wachumi wa Tanzania wakati huo lakini wakaamua kuliacha kwa vile Tanzania wakati huo tulikuwa kwenye majadiliano na IMF na World bank ambao walikuwa nyuma ya pazia la makubaliano yale. Hakuna mchumi wa Tanzania aliyekubaliana na mgawanyo ule; mwulize mzee Mtei hapa ambaye ndiye aliyekuwa waziri wa fedha wakati huo kama kweli tulikubaliana na mgawanyo ule kwa roho nyeupe.
Nashukuru sana mkuu

Ila kutokana na hoja hii, ilitakiwa kwenye Mkataba wa EAC2 wa 1999; Kenya ichangie zaidi kwa kuwa ilifaidika zaidi na anguko la EAC1

Kwa nini wachumi hawakulirudisha hili mezani
 
Back
Top Bottom