joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,117
- 46,617
Ukweli lazima tuuseme, Kenya ni nchi ya ajabu sana, Kenya haina uwezo wa kutekekeza jambo lolote kwa ufasaha.
Tuneshuhudia watu wakipigwa na kuuliwa na polisi katika zoezi zima la kutekeleza amri ya kutotoka nje ili kupambana na maambukizi ya Corona. Juzi hata zoezi la kugawa chakula limesababisha vifo kutokana na nchi kushindwa kujipanga katika kutekeleza majukumu yake.
Wakati Kenya ikiripoti visa vya mateso na vifo kwa wananchi kutokana na uzembe wa kutojipanga kwa serikali, nchi Jirani za Rwanda na Uganda ambazo ndio zilizoanza zoezi la kusambaza chakula bure, wamefanikiwa kusambaza vyakula kwa amani bila kuhatarisha maisha ya wananchi.
Swali la kujiuliza, hivi ni kwanini Kenya hawapendi kujifunza toka kwa majirani pamoja na ukweli kwamba Kenya ndio nchi ibayofanya vibaya katika kila mradi hapa EA?.