Wakati Uganda waki qualify AFCON sisi TFF wamelala

Hawa Uganda walijipanga muda mrefu,hata ujeruman kuchukua kombe la dunia alikuwa anasogea taratibu,kumbuka Spain walianza na kombe la ulaya ndo wakabeba kombe la dunia,huwez kuibuka tuuu,lazima kuwekeza na kujipanga.Tff iwakusanye wachezaji wa zamani hasa waliotembea kama A.China,akina Njohole,Manara family wawakutanishe na hawa wasasa kina Mbwana ,utengenezwe mpango maalumu wa maana siyo ubabaishaji otherwise sisi tutabaki hivihivi.
 
Wangefuzu tu ukweli utabakia ukweli na nyeupe itabakia kuwa nyeupe
Waganda wana maandalizi kuliko tz.na kwa wao kufuzu pia imechangiwa zaidi na bahati huo ndio ukweli. Tanzania tulipangiwa kundi gumu.ni vigumu kupenya uzipite misri na nigeria.
wao kundi lao burkina faso,botswana,comoro na uganda yenyewe.hata sisi tungeweza kuvuka hapa
 
Duh zaidi ya miaka 36. Kufuzu tu tunashidwa , kushinda kombe hadi thy kingdom come! Nadhani laana ya unafiki inatafuna nchi.
Unashangaa 36...?Hao mnaowapongeza leo wametumia miaka 38...hatuna tofauti na wao...
Nigeria
South Africa.
Hawapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…