Hijajibu swali Narudia tena Diamond aliombwa kupaform kwenye lile tamasha na waziri wa habari Mh Mwakiembe ili aliwakilishe Taifa je,ulitaka akatae?
Ahaaaaaaah mimi nilizania wewe ndiye baba yake davido maana umempamba sana balaaaDingi yake ni bilionea. Davido hajaanza kuishika hela leo labda ndiyo maana hana ushamba fulani unaotusumbua sisi. Tutafika lakini.
Uzi wa kidwanzi.Acha kuwatukuza wamarekani.
Ahaaaaaaah mimi nilizania wewe ndiye baba yake davido maana umempamba sana balaaa
Heee! We jamaa vipi?! Kama hujui namna mijadala ya kwenye forums inavyoendeshwa ngoja nikujuze! Mtu anaweza ku-comment kutokana na mada kuu au anaweza ku-comment kutokana na posts zinazochangia mada kuu!!Dah kuna watu mnapenda ubishi! Yaani umekomalia jambo nililolisema in passing (na ambalo niko sahihi) umesahau kabisa mada niliyoleta.
Ndiyo maana mnafeli kwenye mitihani halafu mnadai elimu ngumu. Yaani katika yote niliyosema, hili ndiyo umeona uliandikie insha?
Kwa hiyo mtu akipiga collabo na Fifty Cent kwako ndio mafanikio?InshAllah na mimi nitakuwa bilionea hivi karibuni.
Davido yuko juu kimuziki hahitaji kiki ili awe kwenye headlines. Ila tusiende huko tafadhali.
Mada ya leo ni ya kutoa ushauri ili muziki wetu ukue na wasanii wetu watoke kwenye makucha ya wanasiasa. Ila inaonyesha wabongo bila drama maongezi hayanogi.
Kwa hiyo mtu akipiga collabo na Fifty Cent kwako ndio mafanikio?
Kisa Fifty ni Mmarekani.Watu kama nyie ndio mnawafanya Wamarekani wajione First Class citizen.
Msanii akipiga Show kuwaburudisha Watz wenzake unamdharau, ila akiwaburudisha Wamarekani unamuona wa maana.
Una akili za kitumwa.
Kuhusu kuweka picha ya 2pac kama avatar haiwezi kuwa sababu ya kwamba nawatukuza.Ungeuliza kwa nini nimeiweka upate sababu?
Binafsi simsikilizi ila 50 bado ni msanii mkubwa sana. Usishangae siku kumuona Davido kwenye TV show ya Power. Unajua kuna wasanii wangapi DUNIANI wanaweza kuwauza mama zao kupata nafasi ya kuperform na 50 Cent?
Chini hapa ni show ya 50 Cent ambayo Davido alitokea.
Alikuwa mkubwa, not anymore. Siku hizi kabaki kusutana instagram tu
Umetema madini gani zaidi ya akili za kishamba kuamini mafanikio ni mpaka upate American appreciation.Hahahahahahahaha!!!! Dahhhhh!!!!!
We jamaa una kipaji cha kuchekesha. Sasa mada kama hii tu ya kuelimishana unatoka jasho na povu hivi je ningekuja na mada za kumteketeza na kumbomoa mtu wako hapa si ndiyo ingekuwa balaa?
Ila this is too funny!!!
NB. Wenzio wamechukua ujumbe unaowafaa wanaenda kuufanyia kazi wewe umekaa hapo unabwabwaja mambo yasiyo na kichwa wala mguu. Ila wengine mambo mengine haya tunayafanya bila kitegemea shukrani za wanadamu, bila hivyo.....
Wakati hao wasaniii wa bongo wakipiga mingo kwa kuwatumia wanasiasa, kun mtu humu jf hana lakufanya bali kutoka povu.Mimi ni mtu ninayeamini kuwa changamoto kubwa katika sanaa ya Bongo inaanzia kwa wasanii wenyewe ingawa serikali inachangia sana kwa kiwango kikubwa kuwadumaza, na hii sidhani kama wanasiasa wnafanya kwa bahati mbaya.
Hivi karibuni niliwahi kuleta uzi hapa nikimkosoa Diamond kwa mambo kadhaa, kuna watu wakanishambulia sana kuwa nina chuki binafsi. Ukweli mimi sipo kwenye 'team' yoyote, I just like good entertainment haijalishi ni nani. Ningependa niwaone Diamond, Ali Kiba, Darassa, Harmonize na wengine wanapiga shows MSG na Las Vegas. Ule uzi niliuleta ukiwa nusu ni utani lakini kuna mawazo ya msingi niliyotaka kuwayasilisha. Watu waliuchukulia too serious!
Kuna changamoto kubwa sana katika kushindana na wasanii wa Nigeria katika muziki. Ukiacha suala la uwekezaji mkubwa waliyofanya kwenye industry yao tofauti na sisi, lakini kuna suala la ukaribu kufika Marekani kutoka Nigeria (kwa maana hiyo gharama ziko chini). Wakati sisi tunakwenda Afrika Kusini kurekodi audio na video, wao wanakwenda Marekani.
Pia Sina uhakika mfumo wao wa usambazaji uko vizuri kiasi gani ila ninachojua kuna Wanigeria wengi kwenye vyombo mbalimbali vya entertainment na wanasaidiana kweli kuanzia fursa za shows zinapojitokeza, kutengeneza programs wanazoziita za muziki wa Afrika lakini kiukweli wanapiga za kwao tu, nk. Hili nakumbuka kumsikia Vanessa Mdee akiliongelea. Kuna kazi kubwa ya kufanya kwenye hili suala.
Pia binafsi sidhani kama ni mbinu nzuri kwa wasanii wetu wakubwa kujaribu kufanya kazi na wasanii wakubwa wa Marekani kama Rick Ross, Omarion. Ukiacha faida za kinyumbani za kufanya hivyo (kupata deals za Vodacom, Tigo na ASAS Dairies), sioni hili likiwasaidia kimauzo huko nje wala kuongeza kujulikana kwao. Tusiwaige kina Davido na Wiz Kid, wao wana mikakati yao, na sisi inabidi tuweke ya kwetu.
Kwa maoni yangu, wasanii wetu wangejikita kufanya kazi na underground artists wa nje (kuna ambao wana fans kibao online ila hawasikiki kwenye mainstream media na wanafanya shows nyingi). Nakumbuka Sugu aliwahi kufanya collabo na wasanii fulani underground wa Marekani. Hii kitu inabidi iwe endelevu ili iwe na matokeo chanya. Mdogo mdogo tukifanya hivyo, kwanza itawajengea wasanii wetu ufahamu fulani, network, ubunifu na asikwambie mtu hot tracks zinatengenezwa kwenye studio za kitaa. Wasanii wengi wakubwa wananunua na kuiba nyimbo na styles zilizotengenezwa na wasanii wa underground. Huko ndiyo kwenye ubunifu hasa na watu wenye njaa.
Kingine kujikita kutafuta fursa za kufanya shows kwenye festivals mbalimbali duniani. Hii ni fursa kubwa sana ambayo wasanii wangekaa chini wakaifanyia kazi. Inabidi kutengeneza Swahili Movement itakayoanzia chini chini isambae taratibu halafu ifike siku sisi ndiyo tuwe watu waku set trends kwenye muziki wa Afrika badala ya kuwa watu wa kuiga tu.
La mwisho, hakuna haja ya kuiga umarekani si katika uvaaji wala uimbaji. Inabidi tuwe na utambulisho wetu. Sishauri turudi kuvaa majani na kucheza miguu peku kama kina Mrisho Mpoto, ila tunaweza kuja na vitu fulani tofauti vitakavyotutofautisha na wanigeria na tamaduni zingine. Tuna makabila zaidi ya 100, kuna madini mengi sana ya sauti, beats, rhythm, choruses, uchezaji hadi fashion ambayo bado kabisa hatujayachimbua.
Tujadiliane kwa ustaarabu, leo sijamshambulia mtu.
Usilazimishe, fiftty aliisha toka 2010.Nature ya industry na ya ucelebrity imebadilika ila kiufupi 50 Cent bado ni msanii mkubwa kwa kila vigezo unavyoweza kuvitumia.
Ila kama nilivyokiri toka mwanzo, binafsi siyo mfuatiliaji sana wa muziki wake kwa sasa ila ukiwa mazingira ya aina fulani, muziki wake ni PERFECT kuutwanga.
Heee! We jamaa vipi?! Kama hujui namna mijadala ya kwenye forums inavyoendeshwa ngoja nikujuze! Mtu anaweza ku-comment kutokana na mada kuu au anaweza ku-comment kutokana na posts zinazochangia mada kuu!!
Nime-comment kutokana na post yako. Na hata baada ya ku-comment, ulijaribu kuijibu... kwanini basi uliendelea kujibu kama ulitaka watu wajadili mada kuu?!
Utakuwa mtu wa hovyo na wa ajabu ikiwa ulitarajia watu wasi-comment kutokana na posts zako! Btw, ina maana hilo unaliona sasa?! Au kwavile umeshindwa ku-defend hoja yako?!
Btw, ubishi ni kukuambia there's no way huyo Davido or any Nigerian Musician anaweza kushiriki kwenye Power series ambayo ipo ukingoni?! I repeat... NO WAY!!!
All in all, who are you upangie watu cha ku-comment?!
Wakati hao wasaniii wa bongo wakipiga mingo kwa kuwatumia wanasiasa, kun mtu humu jf hana lakufanya bali kutoka povu.
Niwe na multiple ID ili iweje? Au namuogopa nani?Nilikujibu kukupa heshima kama mchangiaji ila nikakujulisha tubaki kwenye hoja ya msingi. Sijashindwa kudefend jambo lolote, usilazimishe.
Wawili au watatu mnaong'ang'ania upuuzi mnaoandika mnasound kama huyo jamaa anayelike comment zenu joseph1989. Multiple IDs?
Umetema madini gani zaidi ya akili za kishamba kuamini mafanikio ni mpaka upate American appreciation.