Wakazi awatolea uvivu Wasanii adai hawajitambui, wanataka kuwa kama Diamond

Wakazi awatolea uvivu Wasanii adai hawajitambui, wanataka kuwa kama Diamond

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Rapa Wakazi ametoa kauli kali akiwakosoa wasanii kwa kutojitambua na kutojihusisha na masuala muhimu ya kijamii. Katika andiko lake, alisisitiza kuwa wasanii wengi wamepoteza dira yao ya kuwa kioo cha jamii na badala yake wanataka kuwa matajiri wakifuatilia mafanikio ya msanii maarufu Diamond. Wakazi alieleza kuwa wasanii hawapo tayari kushiriki katika mapambano ya kijamii, badala yake wanajipendekeza kwa viongozi ili kupata manufaa binafsi.
5985460445567369948.jpg
Aidha, alieleza kuwa wengi wao hawazingatii hata masuala yanayowahusu moja kwa moja, hawajiungi na vyama vya kulinda maslahi yao, na wana mikataba mibovu inayowakandamiza. Pia, aliwashauri wanaharakati kuunga mkono wasanii wanaopigania haki badala ya kuwasusia wale ambao hawasimami na jamii.
5985460445567369952.jpg
Wakazi alihitimisha kwa kusema kuwa wasanii wana nafasi kubwa katika mapambano ya mabadiliko, lakini itakuwa vigumu kufanikisha hili kama njaa itaendelea kuwa tatizo.
1726047136483.png
Soma => Nay wa Mitego: Asilimia kubwa ya wasanii ni wa Serikali. Tuache uoga wa kukemea mambo ya kikatili na kutegemea Wasanii kupaza sauti
 

Attachments

  • 5985460445567369954.jpg
    5985460445567369954.jpg
    141.5 KB · Views: 10
  • 5985460445567369940.jpg
    5985460445567369940.jpg
    61.6 KB · Views: 11
Mimi nilishaacha mambo ya kwenda kwenye Shoo za wasanii wasiojielewa.

Bora hela yangu niifanyie mambo ya maana kuliko kumpa mtu ambaye jamii ikipata shida humuoni.
 
Mimi nilishaacha mambo ya kwenda kwenye Shoo za wasanii wasiojielewa.

Bora hela yangu niifanyie mambo ya maana kuliko kumpa mtu ambaye jamii ikipata shida humuoni.
Umewapunguzia nini na wewe umeongeza nini kwenye maisha yako?
 
Back
Top Bottom