Kichuchunge
JF-Expert Member
- Dec 2, 2020
- 384
- 970
Joseph Zablon, Dar es Salaam,
Baadhi ya wakazi wa Jijini Dar es Salaam wamelalamikia bei ya Sh5,000 inayotozwa kununua kadi janja ya Mwendokasi, iliyozinduliwa jana na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya uzinduzi wa kadi hizo chini ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), baadhi ya wakazi wanaotumia mabasi hayo walisema kuwa kiwango hicho cha bei ni kikubwa na mbaya zaidi hazina salio lolote.
Mtoa huduma wa DART, alipopigiwa katika simu ya huduma kwa wateja ya 0800 110 17 leo, alithiitisha kuwa bei ya kadi janja hiyo ni Sh5,000 na mteja anaweka salio mwenyewe kwa ajili ya nauli.
”Mambo ya ajabu sana, kadi za kuvuka feri kigamboni zinauzwa Sh2,000, kadi 1,000 na 1,000 ni salio likiisha unaongeza lakini za mwendokasi 5,000 na hazina salio hivyo inabidi uweke hela ya nauli” anasema Winne Mosha, mkazi wa Kimara Suka.
Soma Pia: Mchengerwa: DART Hakikisheni Wakazi wa Dar es Salaam Wanapata Kadi Janja za Mabasi ya Mwendokasi
Anasema iwapo serikali inawapenda watu wake na imepania kuondoa tiketi za karatasi ambazo zinachangia uchafuzi wa mazingira wapunguze bei za kadi ili wengi waweze kumudu.
Tovuti ya Dart inaonyesha kiwango cha mwisho kuweka hela kwenye kadi ni Sh30,000 na cha chini ni Sh1,000 lakini haiionyeshi bei ya hizo kadi janja.
Mkazi mwingine wa Ubungo Maziwa alisema kurudishwa kadi janja kutasaidia kupunguza changamoto ya foleni lakini suala la bei inabidi litazamwe upya.
Baadhi ya wakazi wa Jijini Dar es Salaam wamelalamikia bei ya Sh5,000 inayotozwa kununua kadi janja ya Mwendokasi, iliyozinduliwa jana na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya uzinduzi wa kadi hizo chini ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), baadhi ya wakazi wanaotumia mabasi hayo walisema kuwa kiwango hicho cha bei ni kikubwa na mbaya zaidi hazina salio lolote.
Mtoa huduma wa DART, alipopigiwa katika simu ya huduma kwa wateja ya 0800 110 17 leo, alithiitisha kuwa bei ya kadi janja hiyo ni Sh5,000 na mteja anaweka salio mwenyewe kwa ajili ya nauli.
”Mambo ya ajabu sana, kadi za kuvuka feri kigamboni zinauzwa Sh2,000, kadi 1,000 na 1,000 ni salio likiisha unaongeza lakini za mwendokasi 5,000 na hazina salio hivyo inabidi uweke hela ya nauli” anasema Winne Mosha, mkazi wa Kimara Suka.
Soma Pia: Mchengerwa: DART Hakikisheni Wakazi wa Dar es Salaam Wanapata Kadi Janja za Mabasi ya Mwendokasi
Anasema iwapo serikali inawapenda watu wake na imepania kuondoa tiketi za karatasi ambazo zinachangia uchafuzi wa mazingira wapunguze bei za kadi ili wengi waweze kumudu.
Tovuti ya Dart inaonyesha kiwango cha mwisho kuweka hela kwenye kadi ni Sh30,000 na cha chini ni Sh1,000 lakini haiionyeshi bei ya hizo kadi janja.
Mkazi mwingine wa Ubungo Maziwa alisema kurudishwa kadi janja kutasaidia kupunguza changamoto ya foleni lakini suala la bei inabidi litazamwe upya.