Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, wakazi wa kata tajwa hapo juu wanaishi kwa mateso makubwa toka mwaka 2023 mpaka leo baada ya kufanyika tathmini ya uwanja wa ndege Kigoma na kutokulipwa stahiki zao.
Hadi sasa, wakazi hao waliitwa katika viwanja vya zahati ya machinjioni mnamo mwaka 2023, mwezi wa tano, na kuambiwa kuna upanuzi wa njia ya kupaa ndege, ambayo inatakiwa kuwa kubwa kwa ajili ya ndege kubwa kutua.
Hivyo, kutakuwa na wahanga watakaopaswa kupisha mradi huo na zoezi hilo ni la haraka ambalo inatakiwa wakazi hao wafanyiwe tathmini haraka wapishe upanuzi huo ili mradi uweze kukamilika.
Lakini kinyume na makubaliano hayo, ambayo aliyaleta muwakilishi kutoka Tanrodi Kigoma kwa kumuwakilisha mkurugenzi wa Tanrodi Mkoa, leo watu nyumba zao zinawadondokea na wanashindwa cha kufanya.
Maana waliishafanyiwa tathmini na hawatakiwi kuongeza kitu chochote kwenye eneo hilo. Ukiongeza, hulipwi ulichokiongeza, ni hasara kwako. Waliishawaita waandishi wa habari, wakatoa habari hiyo lakini haikuleta athari yoyote mpaka sasa.
Walimuita mbunge Ngenda Kilumbe, akaliongea bungeni, lakini ni miezi sita sasa na hawaoni utekelezaji wa malipo yao.
Hivyo, wanamuomba Waziri Mbarawa, yeye ndio mwenye dhamana ya hilo pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan kushughulikia malipo yao ili waondokane na adha hiyo.
Hadi sasa, wakazi hao waliitwa katika viwanja vya zahati ya machinjioni mnamo mwaka 2023, mwezi wa tano, na kuambiwa kuna upanuzi wa njia ya kupaa ndege, ambayo inatakiwa kuwa kubwa kwa ajili ya ndege kubwa kutua.
Hivyo, kutakuwa na wahanga watakaopaswa kupisha mradi huo na zoezi hilo ni la haraka ambalo inatakiwa wakazi hao wafanyiwe tathmini haraka wapishe upanuzi huo ili mradi uweze kukamilika.
Lakini kinyume na makubaliano hayo, ambayo aliyaleta muwakilishi kutoka Tanrodi Kigoma kwa kumuwakilisha mkurugenzi wa Tanrodi Mkoa, leo watu nyumba zao zinawadondokea na wanashindwa cha kufanya.
Maana waliishafanyiwa tathmini na hawatakiwi kuongeza kitu chochote kwenye eneo hilo. Ukiongeza, hulipwi ulichokiongeza, ni hasara kwako. Waliishawaita waandishi wa habari, wakatoa habari hiyo lakini haikuleta athari yoyote mpaka sasa.
Walimuita mbunge Ngenda Kilumbe, akaliongea bungeni, lakini ni miezi sita sasa na hawaoni utekelezaji wa malipo yao.
Hivyo, wanamuomba Waziri Mbarawa, yeye ndio mwenye dhamana ya hilo pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan kushughulikia malipo yao ili waondokane na adha hiyo.