KERO Wakazi wa Kibamba (Matembezi) wametuwekea vifusi barabarani lakini hawavisambazi

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Sisi Wakazi wa Kibamba, Mtaa wa Matembezi tuna kero, hadi kufikia jana Juni 10, 2024 ilikuwa ni zaidi ya Saa 24 zimepita tangu tulipowekewa vifusi barabarani bila kusambazwa.

Suala hilo limekuwa kero kubwa kwa kuwa tunashindwa kupita vizuri watembea kwa miguu, wanaotumia vyomvo vya usafiri ndio kabisa wanapata wakati mgumu

Diwani na Mbunge wana taarifa lakini hakuna hatua zozote ambazo zimefanywa mpaka sasa.

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) ambao wanasimamia wanajua kinachoendelea na tumewapigia simu lakini hakuna wanachofanya.

Njia ya kutokea Barabara Kuu zimezibwa na vifusi, tukiuliza wanadai Greda liko Gongo la Mboto.


TARURA WATOA UFAFANUZI
Baada ya JamiiForums kuwasiliana na Meneja wa TARURA, Sigala ambaye anasimamia mradi huo amesema "Tayari tumeanza kusambaza kifusi na kazi inaendelea hadi muda huu (Asubuhi Juni 11, 2024)."



Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…