Wakazi wa Kipunguni A Ukonga, walipwe stahiki yao ili wapishe upanuzi wa uwanja wa Mwalimu JKN

Wakazi wa Kipunguni A Ukonga, walipwe stahiki yao ili wapishe upanuzi wa uwanja wa Mwalimu JKN

davejillaonecka

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2018
Posts
697
Reaction score
749
Ni miaka 22 imepita sasa tangu Serikali ya CCM chini ya Benjamin Mkapa kutoa stop order hapo mwaka 1997 ya kuwazuia wakazi wa kipunguni A, Ukonga jijini Dar es salaam kuendeleza makazi yao ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwalimu JKN lakini wakazi hao mpaka leo hawajalipwa chochote.

Je hii ni haki? Hawa watu wanaishi vipi? Naamini kabisa serikali yeyote sikivu haiwezi fanya haya. Huu ni udhalimu dhidi ya wananchi hawa maskini.
Naomba kwa yeyote anayetaka kura za wananchi hawa zaidi ya 800 aende akawasikilize awe mgombea wa kiti cha udiwani/ubunge au Urais.

Pia naomba kuwashauri watanzania wachague CCM mwaka huu kwa kuwa wenda itatekeleza ahadi zake. Japo hii ni aibu kubwa kwa Serikali ya CCM. Kipindi hicho chote ni muda mrefu sana kusubiria hatima?

Watu wamechoka na wanataka haki zao.Watu wa Haki za binaadamu, na mashirika kama LHRC wasadieni hawa wananchi wa Kipunguni kudai haki yao ya msingi.

Naomba kuwasilisha.
 
Hamjitambui umesema toka 1997 hamjalipwa hadi leo afu unasema waichague ccm huenda ikatekeleza ahadi kweli mmezoea kudanganywa
 
Back
Top Bottom