KERO Wakazi wa Masasi tuna kero ya umeme kukatika mara kwa mara, tunapata hasara TANESCO shughulikieni hilo

KERO Wakazi wa Masasi tuna kero ya umeme kukatika mara kwa mara, tunapata hasara TANESCO shughulikieni hilo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Kayugumis

Senior Member
Joined
Jun 6, 2022
Posts
107
Reaction score
97
Mimi ni Mkazi wa Masasi, nilihamia huku miezi kadha iliyopita, moja ya changamoto ambayo niliikuta huku na wenyeji wanadai imekuwepo kwa muda sasa, ni suala la umeme kukatika mara kwa mara.

Huku Masasi kwa kweli inafikia hatua unakasirika na mwisho unaanza kucheka, kuna wakati umeme unakatika kila baada ya nusu saa, kuna wakati unakatika muda mrefu bila kujali ni mchana au usiku.

Hatuelewi tatizo ni nini, hivi sisi si ndio tuna gesi huku, sasa faida yake ni ipi kama hatupati huduma vizuri, inakuwa ni kama tunaomba msaada.

Kuna hasara nyingi zinazotokana na umeme kukatika mara kwa mara, hali hii ni hatarishi kwa kuwa juzikati kuna nyumba iliungua na ilidaiwa ni shoti iliyotokana na umeme kukatika na kurudi japokuwa hakuna uthibitisho juu ya hilo.

TANESCO Mtwara chukueni hatua, mnatuumiza Wananchi, kwani kero hii ipo sana maeneo mengi ya Masasi.

Majibu ya TANESCO ~ TANESCO yaomba radhi umeme kukatika mara kwa mara Lindi na Mtwara, yasema kuna kazi ya kufunga Mifumo Mipya
 
Niliwahi wapigia wakati Fulani nikiwa huko wakasema Kuna hitilafu Wanarekebisha. lakini ajabu imekuwa kila siku umeme unakata Kama ni lazima, kila baada ya mud flan wanakata!! Especially Mechi zikianza unakatika
 
Siyo masasi tu mkoa mzima wa mtwara umeme ni shida kubwaaa sana sana. Utadhan wameajiri mtu wa kukata umeme tu ni aibu sana alafu hawatoi taarifa hii siyo sawa. Wanafamya chochote na hakuna mtu atawafanya chochote
 
Siyo masasi tu mkoa mzima wa mtwara umeme ni shida kubwaaa sana sana. Utadhan wameajiri mtu wa kukata umeme tu ni aibu sana alafu hawatoi taarifa hii siyo sawa. Wanafamya chochote na hakuna mtu atawafanya chochote
Vipi tatizo limeisha?
 
Back
Top Bottom