Wakazi wa mbagala kizuiani wasaidiwe na janga la wadudu kunguni

Wakazi wa mbagala kizuiani wasaidiwe na janga la wadudu kunguni

kazikubwa

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2010
Posts
597
Reaction score
148
Wakazi wa Mbagala Kizuiani wametoa kilio chao kwa viongozi wa Serikali ili waweze kuwasaidia kuwaondolea janga la wadudu waitwao Kunguni. Kilio hicho wamekitoa kupitia Times Radio. Katika mahojiano yao na mwandishi walimueleza janga hilo wanalo kwa takriban mwaka mmoja na zaidi.


Hapo awali walikuwa wakiona aibu kueleza wazi tatizo hili hadharani. Kwa sasa maji yapo shingoni na wanaiomba Serikali iwasaidie. Kutokana na maelezo yao wananchi hao wanaamini kuwa Kunguni hao huenda wapo hapo kwa njia ya giza (ushirikina) wakitoa sababu mbalimbali:-
1. Wanadai wadudu hao ukithubutu kuwatia dawa ndio una wa double bora uwaache wakuchakaze wakiwa wachache.
Hawasikii dawa hata kidogo.
2. Wanadai wadudu hao ukiwaanika juani au kuwaunguza na maji ya moto hapo ndio unawaongezea ukali mara dufu.

Wanabchi hao wamedai kuwa kwa sasa wanalala nje ya nyumba zao kuwakwepa kunguni. Wanasema bora kuumwa na mbu lakini siyo kunguni maana washambulia mwanzo mwisho.

Je, Serikali itakuwa sikivu au itadai kuwa hilo halitekelezeki kama madai ya madaktari na walimu?

Tunaomba wanchi wenye imani na mapenzi kwa watanzania tuwasaidie wananchi hawa ili nao waishi kwa amani ndani ya jiji la Dar es salaam. Walitoa kilio chao kupitia kipindi cha DIDA wa Mchops na leo wameamua kurudia kupitia redio hiyo hiyo kupitia kipindi cha Bwana Mkisi cha saa 10 jioni hadi saa 1 usiku wakihisi labda redio ya Mbunge wao iliishiwa betri au mgao wa umeme uliiathiri.

Tuwasaidie watu hawa la sivyo tutapata kazi ya ziada ya kuwaongezea damu.
 
Mbagala bila kunguni inawezekana. Serikali ni sikivu kwa ushirikiano wenu na wawakilishi wenu!
 
We! Kunguni ni nouma acha mchezo. Wanashambulia kama siafu,ukiwasha taa tu wanasepa,ukizima wanazingira na kazi inaanza upyaaa. Waliwahi kusumbua lakini tuliwadhibiti kwa kupiga maji ya moto kila wakati na vile vitu vinavyowatunza tulianika juani kila wakati. Unajua tatizo ni kuwa we ni mgonjwa halaf unaona aibu. Fanya hivi kila baada ya siku4 au wikend utawamaliza wala usione aibu kwan ipo siku watakuaibisha mbele ya wageni. Kwani wanatabia kukatiza kwenye pamba mbele za watu. Poleni ndugu zanguni.
 
Wakazi wa mbagala wameiomba Serikali kuwaokoa na tatizo la wadudu aina ya kunguni ambao kwa sasa wanawafanya walale nje ya nyumba zao. Tusisubiri Serikali, shime wananchi tuwasaidie wenzetu mapema kabla ya kuombwa kuwaongezea damu
 
Aiseee baba yangu jei kei si ajarudi?? ngoja nimwambie aonganishe moja kwa moja mpaka kwa obama akaombe msaada wa kinga kama alivyofanya kwa uomba net

ngoja nipate mbege
 
Nimewasiliana na Bwana Afya wa Manispaa aweze kuwatembelea na kuwapatia ushauri wa kitaalamu.

Hili tatizo alishaambiwa hadi waziri wa afya kwa simu ya mkononi through Wapo Radio. Wakati huo tatizo lilikuwa Mtongani, mashine ya maji na Yombo akaahidi kulifanyia kazi. Sasa sijui bajeti imekuwa finyu tusubiri mwakani?
 
poleni sana SIO MBAGALA TU. shule ya GREEN ACRES YA MSINGI ILIOKO SALASALA kunguni ndio waonawamaliza watoto wanao lala mbweni FUATILIENI NAKO HUKO:flypig:
 
Nape atasema kunguni hawa wameletwa na chadema na wafadhili wao...poleni waathirika wa kunguni
 
...hapo ni mpaka "kwa hisani ya watu wa marekani"
haka kanchi bana...tunazungumzia kunguni mpaka leo...karne hii!
 
Ndugu zangu wa mbagala fanyeni fumigation bwana bila hivyo hamtawamaliza watawatia aibu tu. Imagine una mgeni unamtandikia shuka safi analala halafu usikua anaamshwa na kunguni, ee bwana asubuhi tu anaaga kuondoka yaani kunguni sio mchezo.
 
Back
Top Bottom