KERO Wakazi wa Mbezi Msakuzi kaskazini(kwa lubaba hadi pande) hatuna huduma ya uzoaji TAKA tangu february 2024

KERO Wakazi wa Mbezi Msakuzi kaskazini(kwa lubaba hadi pande) hatuna huduma ya uzoaji TAKA tangu february 2024

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

winky

Senior Member
Joined
May 8, 2013
Posts
140
Reaction score
111
Yapata miezi 7(saba) sasa tangia taka zitolewe mara ya mwisho Wakazi wa eneo hili la mbezi msakuzi kaskazini ambayo ni kata ya mbezi na wilaya ya ubungo hatujapata huduma hii ya kuzolewa taka.

Licha ya kuwa mara ya mwisho Mtendaji na timu yake walipita kila nyumba na kukusanya shilingi 10,000 na kuhaidi watapita mara 3 lakini cha kusikitisha hawajawahi kurudi ( walipita zaidi ya nyumba 100 na ilikuwa ni lazima usipotoa hawabebi taka)

baada ya kufatlia ofisi ya mwenyekiti wa serikali za mtaa majibu yalikuwa
1.pesa zimeenda halmashauri hawajamlipa mkandarasi so mkandarasi kavunja mkataba
2.mtendaji huyo kafukuzwa kaletwa mwingine
3.tunasubiri halmashauri watoe fungu na kutafuta mkandarasi.

leo ni miezi 7 bado tunasubiri hali ni mbaya taka taka zinatupwa kila kona kila bara bara ni harufu mbaya na mazingira hatarishi saana.

tunaomba mamlaka husika zitusaidie
 
Yapata miezi 7(saba) sasa tangia taka zitolewe mara ya mwisho Wakazi wa eneo hili la mbezi msakuzi kaskazini ambayo ni kata ya mbezi na wilaya ya ubungo hatujapata huduma hii ya kuzolewa taka.

Licha ya kuwa mara ya mwisho Mtendaji na timu yake walipita kila nyumba na kukusanya shilingi 10,000 na kuhaidi watapita mara 3 lakini cha kusikitisha hawajawahi kurudi ( walipita zaidi ya nyumba 100 na ilikuwa ni lazima usipotoa hawabebi taka)

baada ya kufatlia ofisi ya mwenyekiti wa serikali za mtaa majibu yalikuwa
1.pesa zimeenda halmashauri hawajamlipa mkandarasi so mkandarasi kavunja mkataba
2.mtendaji huyo kafukuzwa kaletwa mwingine
3.tunasubiri halmashauri watoe fungu na kutafuta mkandarasi.

leo ni miezi 7 bado tunasubiri hali ni mbaya taka taka zinatupwa kila kona kila bara bara ni harufu mbaya na mazingira hatarishi saana.

tunaomba mamlaka husika zitusaidie
Subirini msaada wa Marekani.
 
Namna ya magari kuingia huko labda ndiyo shida

Ova
 
Ondoeni viongozi wote wa huko wekeni uongozi mpya. Uchaguzi wa serekali za mitaa si unakuja. Pia msisahau kuondoa mbunge wenu amezubaa sana
 
hapana njia nzuri tu na zimechongwa ni sisi tu mitaa mingine wanapata huduma
 
hapana njia nzuri tu na zimechongwa ni sisi tu mitaa mingine wanapata huduma
Njia ipi imechongwa huko
Njia mbovu, sema hicho kipande
Cha lami anaweka huyo mkandarasi mhuni nusu nusu tu

Ova
 
Back
Top Bottom